CHAMA CHA MAPINDUZI ZANZIBAR CHAFARIJI FAMILIA ZA WALIOKULA KASA KISIWA PANZA.
Chama Cha Mapinduzi(CCM) Zanzibar,kimewasihi wananchi visiwani humo kufuata maelekezo na wito unaotolewa na Serikali juu ya kuacha kula nyama ya kasa wanaodhaniwa kuwa na sumu.
Nasaha hizo zimetolewa na Katibu wa Kamati Maalum ya NEC,Idara ya Itikadi,Uenezi na Mafunzo Khamis Mbeto Khamis alipokwenda kutoa pole na kuzifariji familia za watu tisa waliofariki dunia hivi karibuni kwa ulaji wa kasa Kisiwa Panza Mkoa wa Kusini Pemba.
Alisema Chama Cha Mapinduzi Zanzibar kimepokea kwa huzuni na masikitiko makubwa taarifa za misiba hiyo ya wananchi na kwamba Chama na Serikali zitakuwa karibu na familia za marehemu hao kwa kuhakikisha wanapata huduma muhimu za kijamii kama zilivyo familia zingine nchini.
Alisema Serikali haipendi kuona wananchi wake wanapoteza maisha kwani kila mtu ana mchango wake katika ustawi wa maendeleo ya familia yake na Taifa kwa ujumla.
Katika maelezo yake Mbeto,amesema wananchi hasa wavuvi wanatakiwa kuacha kuvua kasa kwani tayari ameonekana sio samaki salama kwa matumizi ya binadamu.
Alieleza kuwa Zanzibar imebarikiwa kuwa na bahari yenye samaki wa aina mbali mbali wanaofaa kuliwa na binadamu hivyo ni muhimu wananchi kujali afya zao kwa kuacha kula kasa wenye sumu.
“Nimekuja kutoa pole kwa niaba ya Makamu Mwenyekiti ambaye pia ni Rais wa Zanzibar Dk.Hussein Mwinyi anawapa pole na kuwasihi muendelee kuwa wavumilivu kwa kipindi hiki kizito cha misiba hii.”,alisema Mbeto.
Amefafanua kuwa miaka ya hivi karibu Serikali ilipiga marufuku na kuwataka wavuvi kuacha kuvua kasa kwa kile kilichoelezwa kuwa viumbe hao kutokuwa salama kutokana na mabadiliko ya vyakula wanavyokula na kusababisha sumu ya mwili na kuhatarisha uhai kwa binadamu anayekula nyama husika.
Alisema utafiti mdogo uliofanywa umebaini kwamba kasa wamekuwa wakila chakula aina ya majani yenye mchanganyiko wa sumu ambayo binadamu akila nyama yake husababisha kifo.
Pamoja na hayo pia Katibu huyo wa NEC Mbeto,aliwatembelea wananchi walionusurika vifo kutokana na ulaji wa kasa huko Hospitali ya Abdallah Mzee Pemba na kuutaka Uongozi wa Hospitali hiyo kuendelea kuwapatia matibabu ili wapone na kuendea na majukumu yao.
Inadaiwa watu hao waliokula kasa walianza kupata matokeo ya kuumwa na tumbo kwanzia siku chache ,walioathirika na ulaaji huo na kupelekea kupata dalili za Kulegea mwili ,kutapika, kuharisha na tumbo kuuma hadi kupelekea vifo 9 kwa watoto chini ya miaka 10 na wengine 34 wanaendelea kupatiwa matibabu.
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
09-12-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
09-12-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
09-12-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
09-12-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
09-12-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
09-12-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
09-12-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
09-12-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
09-12-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
09-12-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
09-12-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
09-12-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
09-12-2025
TAARIFA KWA UMMA
09-12-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
09-12-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
09-12-2025