RAIS SAMIA AMETOA FEDHA KUJENGA BARABARA SAME - KISIWANI - MKOMAZI
SAME MASHARIKI: SERIKALI imetoa jumla ya kiasi cha Sh bilioni 59 kwa ajili ya kutekeleza ujenzi wa barabara kutoka Same. -Kisiwani- Mkomazi yenye urefu wa kilometa 35.
Katibu wa Halmashauri Kuu (NEC), Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Amos Makalla ameeleza hayo leo Juni 11, wakatika kuzungumza na wananchi kwenye mkutano uliofanyika katika Kata ya Ndungu Jimbo la Same Mashariki wilayani Same mkoani Kilimanjaro.
Makallaameeleza hayo akigusua taarifa ya Mbunge wa Jimbo la Same Mashariki, Anna Kilango Malecela iliyoainisha miradi ya mendeleo iliyotekelezwa katika jimbo hilo katika maeneo mbalimbali na ujenzibwa barabara hiyo ni sehemu ya miradi iliyopo katika utekelezaji.
“Changamoto ya barabara ya Same-Kisiwani moaka Mkomazi ambayo tulipokuja mwaka 2005 na haikutekelezwa ndani ya uongozi Rais Samia Suluhu Hassan ametoa Sh bilioni 59 kilometa 35 inajengwa,” amesema Makalla.
Ameongeza kuwa ni kilometa 100 zinazohitajika kujengwa lakini zinajengwa kwa awamu na barabara hiyo imepigiwa kelele kwa miaka mingi ameipigia kelele ndani ya uongozi wa Rais Samia amemsikiia na kutoa fedha ujenzi umeanza