RAIS WA ZANZIBAR MHE.DK.HUSSEIN MWINYI AKIZUNGUMZA NA VIONGOZI WA JUMUIYA YA WASTAAFU NA WAZEE ZANZIBAR (JUWAZA) IKULU JANA
Zanzibar,
07 Juni, 2023
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi amezitaka mamlaka husika zinazoshughulika na masuala ya pechni na penchini jamii kwa wazee, kurekebisha na kuboresha mifumo yao ili zoezi la utoaji wa penchi kwa mwezi Julai mwaka huu kuanza bila ya kikwazo chochote.
Alizitaka mamlaka hizo kujitahidi kumaliza zoezi la usajili na uhakiki wa masuala yote muhimu yanayowahusu wazee hao yakamike ndani ya mwezi huu wa Juni ili ifikapo Julai kusiwe na kasoro zozote zitakazowakosesha wazee kupata haki yao ya pencheni.
“Nisingependa hata kidogo kwa nia njema tuliyokuwa nayo ya kuwasaidia wazee, halafu usikie Julai imefika, huyu hajapata, huyu kakosa kitambulisho, itakua hatuja wasaidia wazee” Alitahadharisha Dk. Mwinyi.
Dk. Mwinyi alitoa maagizo hayo alipozungumza na Jumuiya ya Wazee na Wastaafu, Zanzibar (JUWAZA), Ikulu – Zanzibar waliofika kumpongeza kwa hatua yake ya kuwajali na kuwaongezea pencheni na pencheni jamii.
Akizungumia changamoto ya vitambulisho kwa wazee hao hasa wakati wakupata haki zao za msingi, Rais Dk. Mwinyi alizishauri mamlaka husika kurasimisha baadhi ya vitambulisho kwa wazee hao ili wapate haki zao zote kwa wakati yakiwemo masuala ya jamii.
Alishauri kuwe na utaratibu mzuri kwa wazee hao kupata haki zao kwa wakati kusiwe na urasimu na kuwanyima haki zao za msingi.
“Hakuna ubaya wa kurasimisha vitambulisho, sio lazima vitumike “ZAN ID” au “NIDA” katika kuwapatia wazee haki zao, kama wengine hawana vitambulisho hivyo, kuwe na utaratibu kurasimisha ama kuanzishwe vitambulisho maalumu vya wazee vitakavyowaunganisha na huduma zao zote zikiwemo pensheni, pencheni jamii na masuala ya kijamii ikiwemo usafiri, afya na wepesi wa kupata huduma nyengine” alifafanua Dk. Mwinyi.
Pia Rais Dk. Mwinyi, alizishauri mamlaka zinazosimamia pencheni za wazee kushirikiana na jumuiya hiyo ya Wazee ili kubaini wazee wanaozidi ama kupungua kwenye uhakiki wao.
Alieleza kuna haja ya Taasisi za Serikali zinazoshughulikia masuala ya wazee, kukaa pamoja na kuongeza ushirikiano baina yao na JUWAZA ili kupata takwimu sashihi zinazowahusu wazee wote nchini.
Aidha, aliwaahidi wazee hao kwamba atatoa maagizo kwa uongozi wa Wizara tatu za Serikali zikiwemo Fedha, Ustawi wa Jamii na Afya, ili kwakae pamoja na wazee hao kwa lengo la kujadiliana na kuondoka na mipango mizuri Imarisha ustawi wa wazee hao kwa sasa na baadae.
“Niombe na maelekezo nitatoa, kwa Wizara tatu za Serikali, mukutane na tumu za uongozi wa Wizara ya Fedha, Ustawi wa Jamii na Afya, mjadiliane ili muondoke na mpango mzuri wa kuyafabya haya” Alisisitiza Dk. Mwinyi.
Akizungumza kwenye hafla hiyo, Katibu wa (JUWAZA) Salma Kombo Khamis aliiomba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuwapatia wazee wa Zanzibar daktari maalum atakaeshughulikia masuala ya wazee kwenye hospitali kuu ya Mnazi Mmoja (Geriatrician) pamoja na wauguzi wa masuala ya wazee tu, ili kuwaondoshea usumbufu wazee wengi wanaotibiwa kwa kuondoshwa njiani tu bila ya uangalizi wa kina kwa mujibu wa hali zao.
Aidha, waliiomba Serikali kupitia vyuo vya Afya nchini kuona umuhimu wa kuongezwa kufundishwa kozi maalumu ya kada ya utaalamu wa kuwatibu na kuwashuighulikia wazee na iwe endelevu kwa manufaa ya wazee wa sasa na wabaadae.
Pamoja na kuangalia upya kada ya uzazi ambayo alieleza vyuoni inafundishwa kwa kiwango kidogo sana, hivyo aliziomba mamlaka husika kuona haja ya kuongezewa muda ili kuepusha changamoto zinazowakabili mama wajawazito kwa uchache wa wataalamu.
Pia Katibu huyo aliiomba Serikali kupitia mamlaka husika kuangalia uwezekano wa wazee kuwekwa kwenye mfumo wa mpya wa Afya ambao utawatambua rasmi Wazee, wanawake na watoto ili kuwaepushia kuwakosesha haki zao za msingi ambapo walilaumu kwamba kuna baadhi ya mifumo ya afya haiwatambui wazee hao.
Hata hivyo, wazee hao walimshukuru Dk. Mwinyi kwa uamuzi wake wakuwaongezea pencheni na pencheni Jamii kutoka kima cha chini hadi asilimia 100 na 150 kwa pencheni jamii na wastaafu.
Kwa mujibu wa Jumuiya ya Wazee na Wastaafu, Zanzibar (JUWAZA), ilianzishwa wakati wa awamu ya tano ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na mwaka 2016 ilianzishwa pencheni jamii. Wazee wote tangu mwaka 1960 ni 57,000 na wazee wa penche ni 28,000 kwa mujibu wa jumuiya hiyo.
𝐂𝐂𝐌 𝐘𝐀𝐓𝐇𝐈𝐁𝐈𝐓𝐈𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐒𝐈𝐍𝐆𝐈 𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐇𝐔𝐃𝐔𝐌𝐈𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐕𝐘𝐀𝐌𝐀 𝐓𝐀𝐖𝐀𝐋𝐀 𝐀𝐅𝐑𝐈𝐊𝐀
22-07-2026
𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐍𝐀𝐈𝐅𝐔𝐍𝐆𝐔𝐀 𝐄𝐍𝐙𝐈 𝐌𝐏𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐆𝐎𝐌𝐀!
22-07-2026
🚆 𝐓𝐔𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐄 𝐊𝐈𝐆𝐎𝐌𝐀!
22-07-2026
ZIARA YA RAIS WA MISRI-TANZANIA
22-07-2026
🔰 CCM NA ACT-WAZALENDO WASAINI MARIDHIANO YA PAMOJA YA KISIASA ZANZIBAR
22-07-2026
🎉 𝐇𝐄𝐑𝐈 𝐘𝐀 𝐒𝐈𝐊𝐔 𝐘𝐀 𝐊𝐔𝐙𝐀𝐋𝐈𝐖𝐀, 𝐃𝐊𝐓. 𝐀𝐒𝐇𝐀-𝐑𝐎𝐒𝐄 𝐌𝐈𝐆𝐈𝐑𝐎! 🔰
22-07-2026
🔰𝐍𝐀𝐈𝐁𝐔 𝐊𝐀𝐓𝐈𝐁𝐔 𝐌𝐊𝐔𝐔 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐁𝐀𝐑𝐀 𝐀𝐒𝐇𝐈𝐑𝐈𝐊𝐈 𝐊𝐈𝐊𝐀𝐎 𝐂𝐇𝐀 𝐇𝐀𝐋𝐌𝐀𝐒𝐇𝐀𝐔𝐑𝐈 𝐊𝐔𝐔 𝐘𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐌𝐖𝐀𝐍𝐙𝐀
22-07-2026
🔰𝐇𝐄𝐑𝐈 𝐘𝐀 𝐌𝐀𝐀𝐃𝐇𝐈𝐌𝐈𝐒𝐇𝐎 𝐘𝐀 𝐒𝐀𝐁𝐀 𝐒𝐀𝐁𝐀 𝟐𝟎𝟐𝟔!
22-07-2026
𝐒𝐀𝐒𝐀 𝐍𝐈 𝐙𝐀𝐌𝐔 𝐘𝐀 𝐏𝐖𝐀𝐍𝐈; 𝐀𝐑𝐃𝐇𝐈 𝐘𝐀 𝐇𝐈𝐒𝐓𝐎𝐑𝐈𝐀, 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐀𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀!!!!!
22-07-2026
𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈 𝐘𝐀𝐌𝐏𝐀 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐌𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐇𝐈𝐒𝐓𝐎𝐑𝐈𝐀
22-07-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐙𝐈𝐍𝐃𝐔𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐋𝐀 𝐖𝐀𝐊𝐄𝐑𝐄𝐊𝐄𝐓𝐖𝐀 𝐌𝐋𝐀𝐍𝐃𝐄𝐆𝐄, 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐒𝐀-𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀
22-07-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐍𝐀. 𝟏𝟎 𝐌𝐀𝐅𝐈𝐅𝐈, 𝐀𝐒𝐈𝐒𝐈𝐓𝐈𝐙𝐀 𝐀𝐌𝐀𝐍𝐈, 𝐔𝐌𝐎𝐉𝐀 𝐍𝐀 𝐌𝐒𝐇𝐈𝐊𝐀𝐌𝐀𝐍𝐎
22-07-2026
𝐌𝐑𝐀𝐃𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐎 𝐘𝐀 𝐔𝐅𝐔𝐍𝐃𝐈 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎 𝐊𝐔𝐅𝐔𝐍𝐆𝐔𝐀 𝐅𝐔𝐑𝐒𝐀 𝐙𝐀 𝐀𝐉𝐈𝐑𝐀 𝐊𝐖𝐀 𝐕𝐈𝐉𝐀𝐍𝐀
22-07-2026
𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎, 𝐙𝐀𝐌𝐔 𝐘𝐄𝐍𝐔 𝐍𝐈 𝐋𝐄𝐎!
22-07-2026
𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀: 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐒𝐔𝐋𝐔𝐇𝐔 𝐇𝐀𝐒𝐒𝐀𝐍 𝐍𝐈 𝐌𝐓𝐄𝐊𝐄𝐋𝐄𝐙𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐀𝐇𝐈𝐑𝐈 𝐖𝐀 𝐀𝐇𝐀𝐃𝐈 𝐙𝐀 𝐂𝐂𝐌
22-07-2026
𝐒𝐈𝐌𝐔 𝐈𝐌𝐄𝐈𝐓𝐀, 𝐍𝐄𝐄𝐌𝐀 𝐘𝐀 𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐙𝐈 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎!
22-07-2026
𝐑𝐔𝐀𝐇𝐀 𝐌𝐁𝐔𝐘𝐔𝐍𝐈 𝐘𝐀𝐅𝐔𝐑𝐈𝐊𝐀; “𝐂𝐇𝐈𝐄𝐅 𝐂𝐇𝐎𝐆𝐀𝐕𝐀𝐓𝐀𝐌𝐁𝐔𝐋𝐄” 𝐀𝐊𝐈𝐓𝐄𝐊𝐀 𝐌𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐎 𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐀!
22-07-2026
𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐎 𝐂𝐇𝐀 𝐔𝐌𝐖𝐀𝐆𝐈𝐋𝐈𝐀𝐉𝐈 𝐍𝐈 𝐔𝐅𝐔𝐍𝐆𝐔𝐎 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐏𝐈𝐍𝐃𝐔𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐔𝐂𝐇𝐔𝐌𝐈 𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈: 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈
22-07-2026
𝐂𝐂𝐌 𝐘𝐀𝐔𝐍𝐆𝐀 𝐌𝐊𝐎𝐍𝐎 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐖𝐀 𝐍𝐉𝐎𝐌𝐁𝐄 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐙𝐀 𝐔𝐙𝐀𝐋𝐈𝐒𝐇𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐀𝐋𝐈
22-07-2026
𝐀𝐌𝐀𝐍𝐈 𝐍𝐈 𝐌𝐒𝐈𝐍𝐆𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐎: 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈
22-07-2026