ALHAJJ.DKT HUSSEIN ALI MWINYI AMESEMA NIDHAMU, UADILIFU NA UWAJIBIKAJI NDIO SUALA LA MSINGI NA MUSTAKABLI MWEMA KWA WATUMISHI WA SERIKALI NA TAASISI BINAFSI KWA KUTARAJIA RADHI KUTOKA KWA ALLAH (S.W)
Ameyasema hayo katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar ALHAJJ HEMED SULEIMAN ABDULLA katika Kongmano la TISA (9) la kuukaribisha Mwezi Mtukufu wa Ramadhan lililofanyika katika Ukumbi wa Sheikh Idris Abdulwakil Kikwajuni jijini Zanzibar.
Alhajj Dkt Mwinyi amesema kuwa dini ya Kiislam imehimiza suala la uwajibikaji na ufanisi kwa kila mtu kwani ndani yeke hupatikana maendeleo kwa mtu moja moja na taifa kwa ujumla.
Aidha amewakumbusha waumini wa dini ya kiislamu juu ya umuhimu wa suala uadilifu sio la viongozi tu kwa raia zao bali hata raia anapaswa kumfanyia uadilifu mwenzake kwani kufanya hivyo kutapelekea mapenzi makubwa baina yao.
Sambamba na hayo Alhajj Dkt Hussen Mwinyi amewataka wafanya biashara wakubwa na wadogo kuwafanyia tahfif wananchi katika kuwauzia bidhaa mbali mbali ili kila mmoja aweze kujikimu na maisha hasa katika Mwezi wa Ramadhani ambao unafadhila nyingi ndani yake.
Amesema kwa upande wa Serikali itahakikisha bidhaa za vyakula zinapatikana nchi nzima na zinaingia kwa wakati sambamba na kufuatilia na kusimamia bei elekezi zilizotolewa na Serikali ili kuwasaidia wananchi kuweza kufunga kwa salama na kupata futari kwa wakati bila ya usumbufu wowote.
Akimkaribisha mgeni rasmi Waziri Wa Katiba Sheria Utumishi Na Utawala Bora Mhe. HAROUN ALI SULEIMAN amesema umefika wakati taasisi kuzihifadhi hutuba zote zinazotolewa na viongozi wakiwemo viongozi wa dini kwa faida ya vizazi vya sasa na vya baadae.
Amesema kuhifadhiwa kwa hutuba zinazotolewa na Mashekhe hasa katika makongamano ya dini kutazisaidia sana jamii kuweza kujifunza na kuwaenzi wanazuoni hao pindi watakapokuwa wametangulia mbele ya haki.
Akitoa salamu kutoka ofisi ya Mufti Mkuu Zanzibar KATIBU MTENGAJI kutoka ofisi hio SHEH HALID ALI MFAUME amesema Ofisi itaendelea kutoa miongozo kwa taasisi zote za kidini kwa lengo la kuupeleka uislamu mbele pamoja na kulinda mila na silka za wazanzibari ambao wamerithi kutoka kwa wazee wetu.
Sheh Halid amesema ni lazima waumini kuendelea kuunga mkono juhudi zinazochukuliwa na viongozi wakuu wa nchi za kuwaletea maendeleo wananchi wake sambamba na kuwaombea dua hasa katika kipindi cha mwezi mtukufu wa ramadhan ili kuweza kutimiza yale yote walio yaahidi kwa wananchi kwa faida ya sasa na baadae.
Mapema Katibu wa Taasisi ya ZANZIBAR WELCOMING RAMADHAN CONFERENCE ambao ndio waandalizi wa kongamano hilo linalofanyika kila mwaka Ndugu ALI MOH’D HAJI amesema taasisi huandaa kongamano hilo kwa lengo la kuwakumbusha waumini wa dini ya kiislam juu ya kuukaribisha mwezi mtukufu wa Ramadhan kwa kufanya yale yote yanatakiwa kufanywa sambamba na kuunga mkono juhudi zinazochukuliwa na serikali kuu.
Hata hivyo ametowa wito kwa viongozi wa serikali na wa sekta binafsi kuwajibika ipasavyo katika kutoa haki kwa kila mwananchi kwani kufanya hivyo ndio kutapelekea kuupeleka mbele uislamu sambamba na kumsaidia kwa vitendo rais wa Zanzibar na rais wa jamuhuri ya muungano kufikia malengo waliojiwekea kwa wananchi na taifa kwa ujumla.
Kwa upande wao watoa maaada katika kongomano hilo wamewaasa waumini wa dini ya kiislamu kuwatii na kuwahashimu viongozi wa nchi kwa dhamana zao walizonazo sambamba na kuthamini jitihada zao wanazozifanya katika kuwaletea maendeleo wananchi wake.
Wamesema waislamu wanapaswa kujisahihisha katika uwajibikaji kwa kuwa wadilifu katika maeneo yao ya kazi na hata katika jamii zinazowazunguka kwa kutendeana haki, kushajihishana katk kutenda mema na kukatazana mabaya ili kuweza kupata Radhi za Allah hasa katika mwezi Mtuku wa ramadhani.
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
09-12-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
09-12-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
09-12-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
09-12-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
09-12-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
09-12-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
09-12-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
09-12-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
09-12-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
09-12-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
09-12-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
09-12-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
09-12-2025
TAARIFA KWA UMMA
09-12-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
09-12-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
09-12-2025