WASIRA ATOA ANGALIZO KWA WANAOCHOCHEA KUVURUGA AMANI.
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara Stephen Wasira amesema Chama hakitakuwa tayari kumvumilia mtu yeyote ambaye atabainika kutaka kuvuruga amani na umoja nchini.
Wasira alitoa kauli hiyo leo alipokuwa akizungumza na wana CCM na wananchi wilayani Mbozi, Mkoa wa Songwe ambako ameanza ziara ya kikazi ya siku tatu yenye lengo la kupokea taarifa za utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi na kuzungumza na wana CCM.
“Msingi wa CCM ni umoja na mshikamano na hata vyama vya TANU na Afro Shiraz Part (ASP) vilipoamua kuanzisha Chama hiki pamoja na mambo mengine waliweka msingi wa kuwa wamoja.
“Sisi ni Chama Cha Mapinduzi, sijui hawaelewi? CCM ni muunganiko wa vyama viwili. Ni vyama ambavyo vimetuletea msingi wa umoja na tulileta uhuru na umoja. Hata maneno yaliyopo katika nembo ni Uhuru na Umoja, hivyo tunataka nchi yetu iendelee kuwa huru lakini wawe wamoja na katika kipindi cha miaka 60 ya uhuru wetu tumesimamia amani ya nchi yetu. Ndio maana sisi ni tofauti na nchi nyingine ambazo zimepigana na nyingine bado zinaendelea kupigana,” alisema.
Alisisitiza kuwa ukiona vinaelea ujue vimeundwa na umoja na amani iliyopo nchini imeundwa na TANU pamoja na Afro Shiraz Party, lakini pamoja na waasisi wa taifa hili na kuongeza hata maendeleo yaliyopo nchini yametokana na umoja uliopo.
“Tunaweza kuvumilia yote lakini kwa mtu anayetaka kuvunja umoja hatutamvumilia, mtu anayetaka kuvunja amani ya nchi hatutamvumilia. Tunaotawala ni CCM na tunawaambia hatutavumilia, hatuna Polisi lakini tunayo serikali na haitakuwa tayari kuona amani, umoja na mshikamano wetu unatoweka kwa namna yoyote.
“Tunayasema haya kwa sababu tunajua wapo watu ambao wapo nje ya Tanzania na wengine ni wajukuu wa waliotutawala. Hatuwezi kukubali umoja wetu uharibiwe na mtu ama kikundi cha watu wachache,” alieleza.
Kuhusu wanaosema CCM imekaa sana madarakani aliwajibu kuwa hakuna mahali ambapo walikubaliana nao kwamba CCM itakaa kwa muda gani na kwamba kazi ya kuleta maendeleo ya wananchi haina ukomo, hivyo wataendelea kuwepo kwa ajili ya kuwatumikia wananchi.
“Nataka tuelewane, wanaosema tunakaa sana watujibu tulipatana tutakaa kwa muda gani. Tulidai uhuru ili kubadilisha maisha ya watu, na maisha hayana mwisho anakufa mmoja na maisha yanaendelea, hiyo ndio kazi yetu
“Tulipotangaza maadui watatu ujinga, umasikini na maradhi maana yake tulitangaza vita ya kudumu. Kwa hiyo nadhani wasituulize ilimradi Watanzania wanatuamini tutaendelea kuwepo, ma hakuna dalili za sisi kutoaminika, kwa hiyo tunawambia mambo tunayofanya sasa hivi lengo lake ni maendeleo ya watu,” alisema.
Kuhusu uchaguzi mkuu mwaka huu, Wasira alisema uchaguzi utakuwepo kama Katiba inavyoelekeza na mtu anayeweza kuzuia uchaguzi usifanyike kwani itakuwa ni kinyume na Katiba ya nchi.
“Huu ni mwaka 2025 na ndio maana tutakwenda kuomba ridhaa kwa wananchi. Kuna watu sijui wametumwa au wamejituma wana kaulimbiu yao ‘No reform no election’. Sijui haina tafsiri yake ni ya hapa au ni Ulaya. Wanaosema hiki Kingereza cha ‘No Reform No Election’ walikimbia nchi.
“Rais Samia aliwaambia njooni mtakuwa salama. Rais Samia alipopata madaraka aliwapa nafuu na ninachotaka kuwaambia vyama vyote vilijadili kuhusu Sheria ya Tume ya Uchaguzi, Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani pamoja na Sheria ya Vyama vya siasa. Katiba mpya tulikubaliana isubiri kwanza.”
Kuhusu CCM alisema kuwa nguvu yao ni umoja wao na Chama lazima kiwe na nguvu na kusisitiza kikiwa na nguvu kikitoka kinaenda kwa wanachi kwa sababu ndilo daraja kati ya wananchi na serikali.
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐑𝐀𝐒𝐌𝐈 𝐔𝐑𝐔𝐒𝐈, 𝐀𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐀 𝐍𝐀 𝐏𝐔𝐓𝐈𝐍
04-06-2026
𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎, 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀
04-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐌𝐎𝐒𝐂𝐎𝐖, 𝐔𝐑𝐔𝐒𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀
04-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐒𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐈𝐑𝐎 𝐊𝐖𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐊𝐀𝐙𝐈
04-06-2026
𝐅𝐔𝐍𝐆𝐀 𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐍𝐘𝐀𝐑𝐀 𝐋𝐄𝐎!!!
04-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐍𝐀. 𝟐 𝐊𝐀𝐓𝐀 𝐘𝐀 𝐁𝐎𝐍𝐆𝐀
04-06-2026
𝐁𝐀𝐁𝐀𝐓𝐈 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈 𝐋𝐄𝐎 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐈𝐅𝐔𝐍𝐈𝐊𝐀!!!
04-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐀 𝐍𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐇𝐀𝐍𝐀𝐍𝐆, 𝐀𝐒𝐈𝐊𝐈𝐋𝐈𝐙𝐀 𝐍𝐀 𝐊𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐀 𝐊𝐄𝐑𝐎 𝐙𝐀𝐎
04-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐋𝐄𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐍𝐀𝐍𝐆’-𝐌𝐀𝐍𝐘𝐀𝐑𝐀
04-06-2026
𝐍𝐈 𝐍𝐙𝐀𝐌𝐔 𝐘𝐀 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐍𝐘𝐀𝐑𝐀!
04-06-2026
🔰𝐀𝐒𝐀𝐍𝐓𝐄𝐍𝐈 𝐒𝐀𝐍𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎!
04-06-2026
𝐒𝐇𝐔𝐋𝐄 𝐘𝐀 𝐌𝐒𝐈𝐍𝐆𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐒𝐀𝐃𝐀𝐋𝐀 𝐘𝐀𝐎𝐍𝐃𝐎𝐀 𝐊𝐄𝐑𝐎 𝐘𝐀 𝐊𝐔𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐀 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐌𝐄𝐓𝐀 𝟏𝟐 𝐊𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐈
04-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐀𝐀𝐍𝐙𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀𝐍𝐈 𝐇𝐀𝐈, 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
04-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐀𝐀𝐍𝐙𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐇𝐀𝐈 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
04-06-2026
𝐍𝐈 𝐌𝐔𝐃𝐀 𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐇𝐀𝐈-𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎 𝐒𝐀𝐒𝐀
04-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐌𝐏𝐀 𝐁𝐀𝐉𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐒𝐈𝐇𝐀 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐘𝐄 𝐔𝐋𝐄𝐌𝐀𝐕𝐔 𝐖𝐀 𝐌𝐈𝐆𝐔𝐔
04-06-2026
MAWENZI YAVUNJA REKODI: MITUNGI 3,313 YA OKSIJENI YAZALISHWA KWA MIEZI 6, ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 126 ZAOKOLEWA!
04-06-2026
MAFURIKO YA WANANCHI WA SIHA KWENYE MKUTANO MKUBWA WA HADHARA
04-06-2026
MAPOKEZI YA KATIBU MWENEZI WA CCM NDUGU KENANI L KIHONGOSI MKOANI KILIMANJARO
04-06-2026
🔰 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐒𝐇𝐈𝐍𝐃𝐎 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
04-06-2026