Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Ali Mwinyi amesema Serikali itaendelea kuweka mazingira rafiki na wezeshi ya kiuchumi ili kukuza Sekta ya Fedha nchini
Ameyasema hayo katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdalla katika Uzinduzi wa ripoti ya Utafiti Finscope Tanzania 2023 kwa upande wa Zanzibar katika ukumbi wa Hotel ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege jijini Zanzibar.
Rais Dkt Mwinyi amesema kuwa Serikali itaendelea kuweka mazingira rafiki ya kiuchumi ikiwemo kuunda Sera zinazozingatia mahitaji ya sekta, kuweka mfumo na kanuni wezeshi za udhibiti pamoja na kushirikiana kwa karibu na wadau wote wa sekta ya fedha ili kushuhulikia changamoto zinazokwamisha mafanikio kwenye utendaji.
Amesema kuwa wakati Serikali ikiendelea kuweka mikakati jumuishi pamoja na kuboresha miundombinu ya Msingi, FSDT ina wajibu wa kupanua wigo wa huduma za kifedha, kusaidia ukuwaji wa kampuni na Sekta binafsi pamoja na kuchangia ukuaji wa uchumi na maendeleo ya nchi.
Aidha Rais Dkt Mwinyi amesema Ripoti ya FinScope itasaidia katika kubuni mbinu zitakazotumika katika utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Zanzibar (2023-2050) Mpango Mkakati wa Taifa wa huduma jumuishi za fedha (2023- 2028) na mipango mengine yakimaendeleo pamoja na kutatua changamoto zilizopo, hivyo amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imejipanga kuhakikisha kuwa maendeleo ya sekta ya fedha na hali ya huduma jumuishi za fedha nchini ziinaimarika.
Dkt. Mwinyi amesema bado kuna kazi kubwa ya kuhakikisha Wazanzibari wenye umri wa kufanya kazi, hususan wanawake, wanafanikiwa kupata kipato binafsi ili kupunguza hali tegemezi na kuongeza matumizi ya bidhaa na huduma mbalimbali za fedha ili kuboresha ustawi wa maisha yao ya kila siku pamoja na kukuza uchumi wa nchi.
Sambamba na hayo amewataka wadau wa Sekta ya fedha kuendelea kuunga mkono jitihada za Serikali za kuboresha hali ya huduma ya jumuishi za kifedha kama zilivyoainishwa katika Dira ya Maendeleo ya Zanzibar na kuwahakikishia kuwa Serikali iko tayari kushirikiana na wadau wa maendeleo nchini kwa lengo la kukabiliana na vikwazo vya maendeleo katika sekta ya fedha kwa kuzingatia Sera, kanuni na miongozo ya nchi
Nae Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, fedha na Mipango Dkt Saada Mkuya Salum amesema bado kuna matumizi finyu ya bima ya afya nchini hivyo Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeona umuhimu wa kuanzisha mfuko wa bima ya afya Zanzibar pamoja na kuyataka mabenki kutafuta utaratibu mwengine wa kufungua huduma za fedha kwa jamii ili kurahisisha upatikanajiwa kuweka fedha benki kwa urahisi na kupunguza gharama.
Dk. Mkuya amesema katika kutekeleza hilo kuna haja ya kusambaza matokeo ya utafiti huu kupitia njia sahihi ili kuhakikisha kunafanyika maamuzi na kubuni bidhaa na huduma zinazopatikana kirahisi, kwa gharama nafuu, na kuzingatia mapendekezo na matakwa ya watumiaji ili kuwafikia watu wengi zaidi.
Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi mfuko wa kuendeleza sekta ya fedha Tanzania Ndugu Erick Masinde amesema ripoti hii imekuwa na lengo la kuikuza sekta ya fedha na kuimarisha upatikanaji wa huduma za fedha ili kuwa jumuishi na endelevu na hatimae kurahisisha shughuli za kiuchumi, kuboresha maisha ya watanzania na kupunguza umasikini..
Mapema watoa mada katika uzinduzi wa riport hio wamesema kupitia ripoti hio kutazisaidia Serikali zote mbili kukuwa kiuchumi na kimaendeleo hivyo wameiomba serikali ya Zanzibar kuitumia ripoti hio kama ni kielelezo kikubwa cha kuondoa upatikanaji wa fedha kwa wananchi wake sambamba na kukuwa kwa maendeleo endelevu nchini.
Ripoti kama hii imekuwa ikitolewa kila baada ya miaka minne (4) kwa kushirikiana na wadau mbali mbali wa fedha hivyo ripoti hii inataarifa muhimu zinazohusu Zanzibar na upatikanaji wa wa fedha
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐌𝐏𝐀 𝐁𝐀𝐉𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐒𝐈𝐇𝐀 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐘𝐄 𝐔𝐋𝐄𝐌𝐀𝐕𝐔 𝐖𝐀 𝐌𝐈𝐆𝐔𝐔
30-05-2026
MAWENZI YAVUNJA REKODI: MITUNGI 3,313 YA OKSIJENI YAZALISHWA KWA MIEZI 6, ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 126 ZAOKOLEWA!
30-05-2026
MAFURIKO YA WANANCHI WA SIHA KWENYE MKUTANO MKUBWA WA HADHARA
30-05-2026
MAPOKEZI YA KATIBU MWENEZI WA CCM NDUGU KENANI L KIHONGOSI MKOANI KILIMANJARO
30-05-2026
🔰 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐒𝐇𝐈𝐍𝐃𝐎 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
30-05-2026
CCM INAWATAKIA HERI YA SIKUKUU YA EID AL ADHA
30-05-2026
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
30-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
30-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
30-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
30-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
30-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
30-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
30-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
30-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
30-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
30-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
30-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
30-05-2026
𝗞𝗜𝗦𝗛𝗜𝗡𝗗𝗢 𝗖𝗛𝗔 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗖𝗛𝗔𝗣𝗢𝗞𝗘𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗛𝗔𝗡𝗚𝗪𝗘 𝗗𝗔𝗥 𝗘𝗦 𝗦𝗔𝗟𝗔𝗔𝗠
30-05-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
30-05-2026