RAIS WA ZANZIBAR ALHAJJ HUSSEIN MWINYI AMEHIMIZA JAMII KUENDELEA KUDUMISHA UMOJA NA MSHIKAMANO ILI KUJENGA TAIFA LA MAENDELEO NA UCHUMI
Al hajj Dk. Mwinyi, alitoa nasaha hizo kwenye Msikiti wa Ijumaa Miembeni Mkoa wa Mjini Magharibi, alikojumuika pamoja na waumini wa dini ya Kiislamu kwenye ibada ya sala ya Ijumaa. Rais, Al hajj Mwinyi, aliieleza jamii kadri inavyokusanyika pamoja kwenye shughuli mbalimbali za maisha ya kila siku, wasichoke kuhimizana umuhimu wa amani ya nchi, kwani kufanya hivyo ni kutimiza malengo mazuri waliyoyakusudia ya ustawi wa jamii bora na maendeleo ya uchumi. “Haya yote tunayoyafanya, yawe ya maendeleo, jamii au ibada misikitini yanategemea amani ya nchi” Alisisitiza Al hajj Dk. Mwinyi. Al hajj Dk. Mwinyi alieleza umoja na mshikamano wa jamii ndio msingi wa kufikia malengo iliyojiwekea, kwa ajili ya maendeleo ya Zanzibar”. Hata hivyo, aliwataka waumini hao waendelee kuombeana du’a na kuliombea taifa katika kufanikisha maleongo yake. Akihutubu kwenye sala hiyo, Khatibu Sheikh Khalid Ali Mfaume alieleza umuhimu wa siku ya Ashura kwenye historia ya uislam na kusisitiza jamii ya waislam
kuendelea kukithirisha ibada hasa kwenye mwezi mtukufu wa Muharam.Sheikh Khalid ambae pia ni Katibu Mtendaji kutoka Ofisi ya Mufti Zanzibar, alisema, Mwezi wa Mfunguo nne (Muharami) ni miongoni mwa miezi minne mitukufu ya Mwenyezi Mungu kwenye kalenda ya uislam pia alieleza mwezi 10 Muharam ni sunna kufunga funga ya Ashura kwa waumini wa dini ya kiislam. Alisema, funga hiyo ni bora baada ya Ramadhani ambayo Mtume (SAW) aliifunga mara baada ya kuhamia Madina.
Hivyo, aliihimiza jamii ya waislam kuzitumia vyema siku tukufu za mwezi wa Muharam kwa kuendelea kukithirisha ibada na kuacha mabaya yote aliyoyakata Mwenyezi Mungu (S.W).
Mara baada ya sala ya Ijuma, Rais Al hajj Dk. Mwinyi alimtembelea kwa kumjuulia hali Bi. Khadija Abass Rashid, mkaazi wa Rahaleo Wilaya ya Mjini alieshiriki kwenye tukio la historia la kuchanganya udongo wa Tanganyika na Zanzibar mwaka 1964 wakati wa kuasisiwa kwa taifa la Jamhuri ya Muungano ya Tanzania.
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐌𝐏𝐀 𝐁𝐀𝐉𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐒𝐈𝐇𝐀 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐘𝐄 𝐔𝐋𝐄𝐌𝐀𝐕𝐔 𝐖𝐀 𝐌𝐈𝐆𝐔𝐔
31-05-2026
MAWENZI YAVUNJA REKODI: MITUNGI 3,313 YA OKSIJENI YAZALISHWA KWA MIEZI 6, ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 126 ZAOKOLEWA!
31-05-2026
MAFURIKO YA WANANCHI WA SIHA KWENYE MKUTANO MKUBWA WA HADHARA
31-05-2026
MAPOKEZI YA KATIBU MWENEZI WA CCM NDUGU KENANI L KIHONGOSI MKOANI KILIMANJARO
31-05-2026
🔰 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐒𝐇𝐈𝐍𝐃𝐎 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
31-05-2026
CCM INAWATAKIA HERI YA SIKUKUU YA EID AL ADHA
31-05-2026
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
31-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
31-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
31-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
31-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
31-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
31-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
31-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
31-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
31-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
31-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
31-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
31-05-2026
𝗞𝗜𝗦𝗛𝗜𝗡𝗗𝗢 𝗖𝗛𝗔 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗖𝗛𝗔𝗣𝗢𝗞𝗘𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗛𝗔𝗡𝗚𝗪𝗘 𝗗𝗔𝗥 𝗘𝗦 𝗦𝗔𝗟𝗔𝗔𝗠
31-05-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
31-05-2026