RAIS WA ZANZIBAR ALHAJJ HUSSEIN MWINYI AMEHIMIZA JAMII KUENDELEA KUDUMISHA UMOJA NA MSHIKAMANO ILI KUJENGA TAIFA LA MAENDELEO NA UCHUMI
Al hajj Dk. Mwinyi, alitoa nasaha hizo kwenye Msikiti wa Ijumaa Miembeni Mkoa wa Mjini Magharibi, alikojumuika pamoja na waumini wa dini ya Kiislamu kwenye ibada ya sala ya Ijumaa. Rais, Al hajj Mwinyi, aliieleza jamii kadri inavyokusanyika pamoja kwenye shughuli mbalimbali za maisha ya kila siku, wasichoke kuhimizana umuhimu wa amani ya nchi, kwani kufanya hivyo ni kutimiza malengo mazuri waliyoyakusudia ya ustawi wa jamii bora na maendeleo ya uchumi. “Haya yote tunayoyafanya, yawe ya maendeleo, jamii au ibada misikitini yanategemea amani ya nchi” Alisisitiza Al hajj Dk. Mwinyi. Al hajj Dk. Mwinyi alieleza umoja na mshikamano wa jamii ndio msingi wa kufikia malengo iliyojiwekea, kwa ajili ya maendeleo ya Zanzibar”. Hata hivyo, aliwataka waumini hao waendelee kuombeana du’a na kuliombea taifa katika kufanikisha maleongo yake. Akihutubu kwenye sala hiyo, Khatibu Sheikh Khalid Ali Mfaume alieleza umuhimu wa siku ya Ashura kwenye historia ya uislam na kusisitiza jamii ya waislam
kuendelea kukithirisha ibada hasa kwenye mwezi mtukufu wa Muharam.Sheikh Khalid ambae pia ni Katibu Mtendaji kutoka Ofisi ya Mufti Zanzibar, alisema, Mwezi wa Mfunguo nne (Muharami) ni miongoni mwa miezi minne mitukufu ya Mwenyezi Mungu kwenye kalenda ya uislam pia alieleza mwezi 10 Muharam ni sunna kufunga funga ya Ashura kwa waumini wa dini ya kiislam. Alisema, funga hiyo ni bora baada ya Ramadhani ambayo Mtume (SAW) aliifunga mara baada ya kuhamia Madina.
Hivyo, aliihimiza jamii ya waislam kuzitumia vyema siku tukufu za mwezi wa Muharam kwa kuendelea kukithirisha ibada na kuacha mabaya yote aliyoyakata Mwenyezi Mungu (S.W).
Mara baada ya sala ya Ijuma, Rais Al hajj Dk. Mwinyi alimtembelea kwa kumjuulia hali Bi. Khadija Abass Rashid, mkaazi wa Rahaleo Wilaya ya Mjini alieshiriki kwenye tukio la historia la kuchanganya udongo wa Tanganyika na Zanzibar mwaka 1964 wakati wa kuasisiwa kwa taifa la Jamhuri ya Muungano ya Tanzania.
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
01-01-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
01-01-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
01-01-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
01-01-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
01-01-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
01-01-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
01-01-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
01-01-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
01-01-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
01-01-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
01-01-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
01-01-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
01-01-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
01-01-2026
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
01-01-2026
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
01-01-2026
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
01-01-2026
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
01-01-2026
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
01-01-2026
TAARIFA KWA UMMA
01-01-2026