BUKOMBE WANATAKA MAENDELEO NA MAENDELEO NI CCM - DKT. BITEKO
π Asema Vyama Vishindane kwa Sera na Utekelezaji wa Ahadi
πWanaCCM Bukombe Waaswa Kuimarisha Ushirikiano
π Azindua Kampeni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Bukombe
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Bukombe, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa kwa miaka yote wananchi wa Wilaya ya Bukombe wamekuwa na imani na Chama Cha Mapinduzi (CCM) pamoja na kiu ya maendeleo.
Amesema wananchi hao wana haki ya kuchagua kati ya maneno au maendeleo na wamekuwa wakitamani maendeleo kwa kuwa na shule, barabara na zahanati.
Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 21, 2024 wakati akifungua Kampeni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa Wilaya ya Bukombe zilizofanyika katika Kata ya Igulwa, Wilaya ya Bukombe Mkoa wa Geita.
“ Tunapozindua kampeni zetu tuna wajibu wa kuchagua maneno au maendeleo, tutashindanisha vyama kwa sera na kuonesha tuliyofanya kwa kipindi kilichopita. Tumekuja leo kuwaambia sisi tuko upande wa maendeleo na wengine wako upande wa maneno kama mwakilishi wenu nimekuja kuwaambia tuchague maendeleo, tuchague CCM,” amesema Dkt. Biteko.
Amesisitiza “ Tuliwahi kupata viongozi wa chama kingine na sasa tuna wajibu wa kupima kati yao na CCM mabadiliko yako chama gani,”
Akielezea hali ya uandikishaji wapiga kura katika Uchaguzi wa Serikali za Mtaa, amesema kuwa mwaka 2024 Bukombe imefanikiwa kuandikisha idadi kubwa ya wapiga kura ambayo ni 228,659 ikiwa ni rekodi ya juu katika mkoa na ukanda huo hali inayodhihirisha ushindi kwa CCM na hasa kutokana na utekelezaji wa ilani yake.
Halikadhalika, Dkt. Biteko amesema asilimia 70 ya vitongoji vina wagombea wa CCM huku vyama vingine vikishindwa kuweka wagombea.
“ Novemba 27, 2024 wote tukapige kura tunatakiwa kumshukuru Rais Samia kwa upendo na kwa kufanya jitihada nyingi za kutujengea barabara, shule za msingi na sekondari, vyuo vya VETA, shule ya amali na mengineyo kwa haya yote twende tukawapigie kura wagombea wa CCM,” amesema Dkt. Biteko.
Pamoja na hayo amewaasa wananchi wa Bukombe kuhubiri umoja, amani na upendo hata baada ya uchaguzi kuisha sambamba na wagombea hao kuhudumia wananchi wa Bukombe.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Geita, Nicholaus Kasendamila amesema kuwa kazi ya CCM katika uchaguzi ni kushinda kwa ngazi zote za kata, vijiji, vitongozi.
Katibu wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Geita, Alexandrina Katabi amewataka wanachama wa CCM Wilaya ya Bukombe kuendelea kuimarisha umoja na ushirikiano wao hasa wakati huu wa kuelekea katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.
Diwani wa Kata ya Bugelenga, Leonard Lubigisa akizungumza kwa niaba ya madiwani amewataka wanachama wa CCM kupiga kura ifakapo Novemba 27, 2024.
Aidha, ameipongeza Serikali kwa kuendelea kupelekea maendeleo katika Jimbo hilo na kuhamasisha wananchi kuichagua CCM kwa jitihada zake za ujenzi wa barabara pamoja na miradi mingine.
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
05-11-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
05-11-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
05-11-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
05-11-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
05-11-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
05-11-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
05-11-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
05-11-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
05-11-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
05-11-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
05-11-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
05-11-2025
TAARIFA KWA UMMA
05-11-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
05-11-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
05-11-2025
MONGELLA AONGOZA MAZISHI YA KADA WA CCM JIJINI MWANZA
05-11-2025
ASIYETII SHERIA, KATIBA NA KUWA TAYARI KUUA KWA MASLAHI BINAFSI HUO NI UGAIDI’
05-11-2025
πππ π¬ππ¦ππ¦ππ§πππ πͺπππ’π πππ ππ¨πππππππͺπ ππͺπ ππ¨πππ‘πππ§ππ π¨πͺπππ’, π¨πππππ‘ππ’ π‘π π¨πππππππ¨, π¬ππππ ππ π πππ¨π‘ππ - πππ. πππ©π¨
05-11-2025
KAENI KIMYA KAMA HAMJUI NCHI ILIKOTOKA - WASIRA
05-11-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amefungua kiwanda cha kutengeneza mabomba ya maji na uchakataji pamba cha MOLI Oil Mills Co. Ltd kilichopo Bariadi Mkoani Simiyu tarehe 16 Juni, 2025.
05-11-2025