DKT.DIMWA ATOA MKONO WA POLE KWA FAMILIA ZA MAKADA WA CCM WALIOFARIKI PEMBA
NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dkt Mohamed Said Dimwa,ametoa mkono wa pole na kuzifariji familia za Viongozi na Makada wa CCM waliofariki Dunia siku za hivi karibuni katika maeneo mbali mbali ya Kisiwa cha Pemba.
Kupitia ziara hiyo Dkt.Dimwa amewasihi,ndugu wa familia,marafiki na jamaa wa karibu kuendelea kuwa wavumilivu na wawaombee dua ndugu zao waliofariki ili wawe na makaazi mema katika pepo ya Mwenyezi Mungu.
Amesema Chama Cha Mapinduzi kilipokea kwa majonzi na mshituko mkubwa taarifa za vifo hivyo vilivyowapoteza makada waliokuwa mstari wa mbele katika kulinda,kutetea na kusimamka kwa vitendo maslahi ya CCM.
Katika ziara hiyo Dkt.Dimwa,alifika Jimbo la Kiwani kuifariji na kutoa mkono wa pole kwa familia ya aliyekuwa Katibu mstaafu wa Siasa na Uenezi wa CCM Mkoa wa Kusini Pemba Marehemu Mwl.Khatib Haji Khalid aliyeacha wajane wawili ambao ni Bi.Kazija Faki Abdalla na Bi.Mwanamiza Jape Khatib na kueleza kuwa CCM itaendeleza kuwa karibu na familia hiyo katika masuala ya Kijamii.
Wakati huo huo alitoa mkono wa pole kwa familia ya aliyekuwa kada wa CCM Tawi la Ukutini Jimbo la Chambani, Marehemu Hassan Ali Faki na kuwasihi waendelee kuwa wavumilivu na wamuombee dua nyingi kada huyo.
"Tumepoteza nguvu kazi na watu muhimu sana waliojitolea kufanya mambo yenye tija ndani ya Chama chetu hivyo nasaha zangu kitu pekee cha kuwalipa ni kuwaombea dua nyingi Mwenyezi Mungu awajaalie nafasi katika pepo ya Firidausi",alieleza Dkt.Dimwa.
Amewaka Wanachama wa CCM nchini kuenzi kwa vitendo historia nzuri za kiutendaji,uadilifu,misimamo na uaminifu usiyoyumba ulioasisiwa na makada hao katika kukitumikia Chama na Jumuiya zake.
Katika maelezo yake Naibu huyo Dkt.Dimwa,alitoa wito kwa waumini wa dini ya kiislamu nchini kutumia vizuri fursa ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhan kufanya ibada,kutoa sadaka na kuwaombea dua ndugu na jamii waliofariki.
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
24-03-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
24-03-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
24-03-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
24-03-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
24-03-2026
πππ¦πππ‘ππ’ πππ πππ§. π ππππ₯π’ ππππ£π’πππππͺπ ππͺπ π¦πππ‘ππͺπ πππ₯ ππ¦ π¦πππππ
24-03-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
24-03-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
24-03-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
24-03-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
24-03-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
24-03-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
24-03-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
24-03-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
24-03-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
24-03-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
24-03-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
24-03-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
24-03-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
24-03-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
24-03-2026