RAIS SAMIA: TANZANIA IMEPIGA HATUA KUBWA KATIKA USAWA WA KIJINSIA
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa kupitia utekelezaji wa Ilani ya CCM, Serikali imepiga hatua kubwa katika kufanikisha malengo ya kuhakikisha kesho bora na njema zaidi kwa vijana wa Kitanzania, wa kike na wa kiume.
Akizungumza katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Mwanamke, yaliyofanyika leo Jumamosi, tarehe 8 Machi 2025, katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, jijini Arusha, Mhe. Rais Dkt. Samia alieleza kuwa Tanzania ina mengi ya kujivunia katika kuboresha mazingira yanayohakikisha ndoto ya usawa wa kijinsia inafikiwa nchini.
“Tunapoadhimisha miaka 30 tangu Tamko la Umoja wa Mataifa la Mkutano wa Beijing, miaka 10 ya Malengo Endelevu ya Dunia na miaka 5 ya Jukwaa la Kizazi Chenye Usawa, ni fursa ya kutathmini mafanikio makubwa yaliyofikiwa na kutambua hatua zaidi zinazohitajika ili kuhakikisha kila msichana na mwanamke hapa nchini anapata nafasi ya kufikia ndoto zake,” alisema Mhe. Rais Dkt. Samia.
Aidha, alisisitiza kuwa hatua mbalimbali za kisera na kisheria zimechukuliwa na zinaendelea kuchukuliwa ili kupambana na mila kandamizi na ubaguzi dhidi ya wanawake na watoto wa kike.
“Watanzania, wake kwa waume, wameunga mkono maamuzi na hatua mbalimbali za kumwezesha mwanamke, hali ambayo imewezesha nchi yetu kupiga hatua kubwa katika usawa wa kijinsia,” aliongeza.
Akifafanua maendeleo yaliyopatikana, Rais Dkt. Samia alitaja hatua kubwa zilizochukuliwa katika sekta mbalimbali za maendeleo nchini, sambamba na Malengo 17 ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa. Alisema kuwa Tanzania imepiga hatua kubwa katika kupunguza umaskini, kukomesha njaa, kuboresha afya na ustawi, elimu bora, usawa wa kijinsia, maji safi na usafi, nishati mbadala, kazi zenye staha, ukuaji wa viwanda, ubunifu na miundombinu, pamoja na kuimarisha amani, haki na taasisi madhubuti.
“Hadi tunapofanya tathmini ya mpango wa tatu wa maendeleo katika Dira ya Taifa ya Maendeleo, tayari tumepunguza umaskini kwa asilimia 26 kutoka kiwango cha awali tulipoanza utekelezaji wa dira. Leo hii, pamoja na jitihada zinazoendelea, tunakaribia kufikia asilimia 30,” alisema.
Kwa upande wa uhakika wa chakula, Rais Dkt. Samia alifafanua kuwa Tanzania imejitegemea kwa chakula kwa asilimia 128 na imefanikiwa kuondoa njaa kwa asilimia 100.
Akihitimisha hotuba yake, Mhe. Rais Dkt. Samia aliwataka Watanzania wote—wanawake na wanaume—kuendelea kujenga jamii makini yenye maadili ya Kitanzania, kuanzia ngazi ya familia, ambayo ndiyo msingi wa taifa imara.
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
24-12-2025
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
24-12-2025
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
24-12-2025
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
24-12-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
24-12-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
24-12-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
24-12-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
24-12-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
24-12-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
24-12-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
24-12-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
24-12-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
24-12-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
24-12-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
24-12-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
24-12-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
24-12-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
24-12-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
24-12-2025
TAARIFA KWA UMMA
24-12-2025