RAIS SAMIA: TANZANIA IMEPIGA HATUA KUBWA KATIKA USAWA WA KIJINSIA
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa kupitia utekelezaji wa Ilani ya CCM, Serikali imepiga hatua kubwa katika kufanikisha malengo ya kuhakikisha kesho bora na njema zaidi kwa vijana wa Kitanzania, wa kike na wa kiume.
Akizungumza katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Mwanamke, yaliyofanyika leo Jumamosi, tarehe 8 Machi 2025, katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, jijini Arusha, Mhe. Rais Dkt. Samia alieleza kuwa Tanzania ina mengi ya kujivunia katika kuboresha mazingira yanayohakikisha ndoto ya usawa wa kijinsia inafikiwa nchini.
“Tunapoadhimisha miaka 30 tangu Tamko la Umoja wa Mataifa la Mkutano wa Beijing, miaka 10 ya Malengo Endelevu ya Dunia na miaka 5 ya Jukwaa la Kizazi Chenye Usawa, ni fursa ya kutathmini mafanikio makubwa yaliyofikiwa na kutambua hatua zaidi zinazohitajika ili kuhakikisha kila msichana na mwanamke hapa nchini anapata nafasi ya kufikia ndoto zake,” alisema Mhe. Rais Dkt. Samia.
Aidha, alisisitiza kuwa hatua mbalimbali za kisera na kisheria zimechukuliwa na zinaendelea kuchukuliwa ili kupambana na mila kandamizi na ubaguzi dhidi ya wanawake na watoto wa kike.
“Watanzania, wake kwa waume, wameunga mkono maamuzi na hatua mbalimbali za kumwezesha mwanamke, hali ambayo imewezesha nchi yetu kupiga hatua kubwa katika usawa wa kijinsia,” aliongeza.
Akifafanua maendeleo yaliyopatikana, Rais Dkt. Samia alitaja hatua kubwa zilizochukuliwa katika sekta mbalimbali za maendeleo nchini, sambamba na Malengo 17 ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa. Alisema kuwa Tanzania imepiga hatua kubwa katika kupunguza umaskini, kukomesha njaa, kuboresha afya na ustawi, elimu bora, usawa wa kijinsia, maji safi na usafi, nishati mbadala, kazi zenye staha, ukuaji wa viwanda, ubunifu na miundombinu, pamoja na kuimarisha amani, haki na taasisi madhubuti.
“Hadi tunapofanya tathmini ya mpango wa tatu wa maendeleo katika Dira ya Taifa ya Maendeleo, tayari tumepunguza umaskini kwa asilimia 26 kutoka kiwango cha awali tulipoanza utekelezaji wa dira. Leo hii, pamoja na jitihada zinazoendelea, tunakaribia kufikia asilimia 30,” alisema.
Kwa upande wa uhakika wa chakula, Rais Dkt. Samia alifafanua kuwa Tanzania imejitegemea kwa chakula kwa asilimia 128 na imefanikiwa kuondoa njaa kwa asilimia 100.
Akihitimisha hotuba yake, Mhe. Rais Dkt. Samia aliwataka Watanzania wote—wanawake na wanaume—kuendelea kujenga jamii makini yenye maadili ya Kitanzania, kuanzia ngazi ya familia, ambayo ndiyo msingi wa taifa imara.
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
26-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
26-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
26-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
26-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
26-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
26-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
26-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
26-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
26-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
26-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
26-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
26-05-2026
𝗞𝗜𝗦𝗛𝗜𝗡𝗗𝗢 𝗖𝗛𝗔 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗖𝗛𝗔𝗣𝗢𝗞𝗘𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗛𝗔𝗡𝗚𝗪𝗘 𝗗𝗔𝗥 𝗘𝗦 𝗦𝗔𝗟𝗔𝗔𝗠
26-05-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
26-05-2026
𝗩𝗜𝗝𝗔𝗡𝗔 𝗧𝗨𝗜𝗟𝗜𝗡𝗗𝗘 𝗔𝗠𝗔𝗡𝗜 𝗬𝗔 𝗡𝗖𝗛𝗜 𝗬𝗘𝗧𝗨 - 𝗠𝗪𝗘𝗡𝗘𝗭𝗜 𝗞𝗘𝗡𝗔𝗡𝗜
26-05-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
26-05-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
26-05-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
26-05-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
26-05-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
26-05-2026