ASIYETII SHERIA, KATIBA NA KUWA TAYARI KUUA KWA MASLAHI BINAFSI HUO NI UGAIDI’
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara Stephen Wasira, amesema utawala bora ni kutii Katiba na Sheria za nchi, hivyo mtu yeyote asiyetii na anataka kufanikisha mambo yake binafsi kwa kuua watu huo ni gaidi.
Wasira ameyasema hayo leo Juni 22,2025 alipokuwa akizungumza katika kikao cha ndani na viongozi na wanachama wa Chama hicho Wilaya ya Ukerewe mkoani Mwanza , ambapo amesisitiza utawala bora kwa kutii katiba na sheria za nchi badala ya kuvunja sheria kwa kisingizio cha uhuru wa demokrasia.
Wakati akieleza hayo Wasira alionesha kukishangaa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)ambacho kimekuwa na kauli mbiu yake ya 'No Reform No Election' yenye lengo la kuvuruga uchaguzi mkuu mwaka huu na kuhoji kama hawataki kupiga kura kwanini walijiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura.
“Asiyetii Katiba na sheria maana yake anataka nchi isitawalike, watu wapigane wenyewe kwa wenyewe, halafu wewe eti haki yako unaitaka katika mazingira ya mauaji bila kujali matokea yake, hilo haliwezekani".
Wasira alifafanua kwamba kwa akili ya kawaida unaweza kujiuliza Katiba ipo inasema kila baada ya miaka mitano unafanyika Uchaguzi Mkuu halafu anatokea mtu anasema hakuna uchaguzi.
“Anasema hivyo kwa kutumia Katiba ipi? Katiba inaeleza wazi huwezi kughairisha uchaguzi alafu wewe unasema lazima usiwepo,kutaka kuzuia uchaguzi ni kinyume na Katiba na ni kutaka kuanzisha fujo…
“Je huo ndio utawala bora? Katiba inasema kila baada ya miaka mitano tunafanya uchaguzi wewe unasema hautafanyika…utawala bora ni kutii katiba na sheria na sio kutaka kukamilisha mambo binafsi kwa kukiuka sheria za nchi.”
Wasira alisema sababu inayoweza kufanya uchaguzi usifanyike ni vita na katika nchi yetu hakuna vita,hivyo hakuna anayeweza kuzuia uchaguzi na kuwahakikishia wananchi kuwa uchaguzi mkuu uko pale pale na tayari uchaguzi ulishaanza kwa wananchi kujiandikisha katika daftari la kupiga kura.
Pia alisema kaulimbiu ya ‘No Reform No Election' inaenda kufa muda si mrefu kwasababu tayari imezidiwa nguvu na Oktoba Tunatiki, na ushahidi wa hilo Watanzania wako tayari kwenda kupiga kura kwani wamejiandikisha.
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
11-03-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
11-03-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
11-03-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
11-03-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
11-03-2026
πππ¦πππ‘ππ’ πππ πππ§. π ππππ₯π’ ππππ£π’πππππͺπ ππͺπ π¦πππ‘ππͺπ πππ₯ ππ¦ π¦πππππ
11-03-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
11-03-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
11-03-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
11-03-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
11-03-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
11-03-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
11-03-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
11-03-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
11-03-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
11-03-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
11-03-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
11-03-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
11-03-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
11-03-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
11-03-2026