NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dkt.Mohamed Said Dimwa,amesema Chama Cha Mapinduzi hakitofanya upendeleo wa kutoa nafasi za kugombea uongozi kwa kigezo cha fedha na utajiri bali kitaweka mbele maslahi ya wanachama wote bila kujali hali zao za maisha.
Kauli hiyo ametoa wakati akiwahutubia viongozi na wanachama wa CCM katika Mkutano Mkuu Maalum wa Jimbo la Pangawe huko Wilaya ya Dimani Kichama Unguja.
Dkt.Dimwa,alisema kila mwanachama ana haki ya kuchagua na kuchaguliwa hivyo ni lazima waondoshe dhana iliyojengeka siku za hivi karibuni kuwa wenye haki ya kugombea na kupata nafasi za uongozi ni watu wenye fedha na matajiri wakati Chama hicho kimetokana na wakwezi,wakulima na wafanyakazi.
Katika maelezo yake Naibu Katibu Mkuu huyo Dkt.Dimwa,alisema CCM itaendelea kusimamia kikamilifu misingi ya usawa,haki,uhuru na demokrasia pana ndani na nje ya Chama ili kutoa nafasi ya wanachama kunufaika na fursa mbalimbali zinazipatikana ndani ya Chama hicho.
“Wapo baadhi ya watu kila ikikaribia wakati wa Uchaguzi Mkuu wa Dola wanawahadaa kwa fedha na vitu vya thamani wanachama wetu ili wawachague na wakisha pata uongozi wanapandisha mabega na wanajisifu kuwa tulipata Ubunge,Uwakilishi na Udiwani kwa sababu ya fedha zetu hivyo mtuache turejeshe fedha zetu kwanza maendeleo baadae.
Awamu hii watu wa aina hiyo mkiwaleta basi mjue hawatovuka kwani kigezo chetu ni kuangalia sifa za msingi za mgombea na tukiridhika naye hata akiwa mnyonge na maskini huyo huyo ndo tutaenda naye.”,alisema na kuongeza kuwa CCM sio mali ya matajiri bali ipo kwa manufaa ya wananchi wote.
Kupitia hotuba yake Naibu Katibu huyo,aliwapongeza Mwakilishi,Mbunge na Madiwani wa Jimbo la Pangawe kwa kazi nzuri wanayofanya ya kushirikiana katika kutatua changamoto za wananchi wa jimbo hilo ikiwemo zoezi la kutoa sadaka ya futari kwa wananchi wenye mahitaji ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya CCM.
Pamoja na hayo amewapongeza waumini wa dini ya kikiristo kwa kuathimisha siku kuu ya Pasaka pamoja kuwasihi waumini wa dini ya kiislamu kuendelea kufanya ibada kwa wingi,kujikataza na maasi na kutoa sadaka ili funga zao katika mwezi huu Mtukufu wa Ramadhani zikubaliwe na Mwenyezi Mungu.
Aliwasihi wanachama hao kuendelea kuthamini na kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan pamoja na Rais wa Zanzibar Dk.Hussein Mwinyi kwa kutekeleza llani ya CCM ya mwaka 2020/2025 kwa ufanisi mkubwa.
Naibu Katibu mkuu huyo Dkt.Dimwa, alizindua rasmi zoezi la ugawaji wa vitambulisho vya kisasa kwa Mabalozi wa mashina wa CCM pamoja na kuwapatia posho la shilingi 20,000 ikiwa ni utekelezaji wa ahadi ya Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Hussein Mwinyi litakalofanyika katika majimbo yote ya Zanzibar.
Pia Dkt.Dimwa, aligawa sadaka ya futari kwa niaba ya uongozi wa jimbo zikiwemo sukari,mchele,mafuta ya kula na unga wa ngano kwa makundi mbalimbali ya Watu wenye mahitaji Maalum,Wazee,Wajane,Masheha na Mabalozi wa Jimbo la hilo.
Akizungumza Mwakilishi wa Jimbo la Pangawe Ali Suleiman Mrembo,amesema lengo la Mkutano huo Maalum wa Jimbo ni viongozi hao kurejesha shukrani kwa wanachama wa CCM wa ngazi mbalimbali kutokana na kazi nzuri waliyofanya ya kuvuka malengo katika awamu ya kwanza ya zoezi la uhakiki wa Daftari la kudumu la uandikishaji wa wapiga kura.
Naye Mbunge wa Jimbo la Pangawe Haji Amour Haji,amesema mafanikio yaliyofikiwa ndani ya jimbo hilo yametokana na dhamira ya dhati ya viongozi hao ya kuleta maendeleo kwa kila mwananchi inayochechewa na ushirikiano kutoka kwa Wanaccm na wananchi wenyewe.
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
09-12-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
09-12-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
09-12-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
09-12-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
09-12-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
09-12-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
09-12-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
09-12-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
09-12-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
09-12-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
09-12-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
09-12-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
09-12-2025
TAARIFA KWA UMMA
09-12-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
09-12-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
09-12-2025