NAIBU Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Zanzibar Dkt.Mohamed Said Dimwa amewasisitiza Viongozi na Watendaji wa CCM kufanya vikao kwa kufuata miongozo na Katiba ya CCM ya mwaaàka 1977 toleo la mwaka 2022.
Maelekezo hayo ameyatoa katika mwendelezo wa ziara yake na Wajumbe wa Sekretarieti ya Kamati Maalum ya NEC,CCM Taifa Zanzibar wakati akizungumza na Kamati ya siasa ya Wilaya ya Mjini Kichama.
Amesema Chama Cha Mapinduzi kimeweka utaratibu wa vikao ili Uongozi wa ngazi mbalimbali wapate nafasi ya kujadiliana masuala ya kiutendaji,mikakati na changamoto za maeneo husika ya kiutawala ndani ya Chama na Serikali zake.
Alisema Viongozi hao wanatakiwa kuendeleza mikakati mbalimbali ya kuimarisha Chama ili kuandaa mazingira rafiki ya upatikanaji wa ushindi katika Uchaguzi Mkuu ujao wa mwaka 2025.
Dkt.Dimwa, amesema lengo la ziara hiyo ni kuimarisha uhai wa Chama ikiwemo kukagua miradi ya Chama Cha Mapinduzi na kuzungumza na wanachama wa ngazi mbalimbali hasa wa ngazi za Mashina na Matawi.
"Fanyeni vikao kwa kufuata Katiba na miongozo yetu ili kuepuka migogoro na maamuzi yasiyofaa kwani Chama chetu kimeweka utaratibu wa kuhakikisha kila jambo linatafutiwa ufumbuzi kupitia vikao vya pamoja.
Pia nakupongezeni kwa kazi nzuri ya kuimarisha Chama chetu ndani ya Wilaya hii hasa kusimamia vizuri utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2020/2025."alisema Dkt.Dimwa.
Akizungumza na wanachama katika maeneo mbalimbali ya Wilaya hiyo alisisitiza ulipaji wa ada ili kupata Wanachama hai.
Alisema CCM inaelekea katika Uchaguzi Mkuu ujao wa mwaka 2025 hivyo kila mwanachama anatakiwa kujiandaa kwa kuhakikisha anakuwa na kitambulisho Cha kupigia kura.
Naibu Katibu huyo Dkt.Dimwa, alisema CCM inaendelea kuamini mfumo wa ujamaa na kujitegemea hivyo ni muhimu Wanachama wake wafanye siasa na uchumi kwa kubuni na kuendeleza miradi ya kuwapatia kipato cha kila siku.
Aliwapongeza Viongozi wa majimbo ya Wilaya hiyo wakiwemo Wabunge,Wawakilishi na madiwani kwa kazi nzuri ya kuanzisha miradi ya ujasirimali inayowasaidia vijana wengi kujiajiri wenyewe ili kutimiza ahadi ya kutimiza ajira 300,000 kufikia mwaka 2025 iliyoanishwa katika Ilani ya CCM ya mwaka 2020/2025.
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
07-01-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
07-01-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
07-01-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
07-01-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
07-01-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
07-01-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
07-01-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
07-01-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
07-01-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
07-01-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
07-01-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
07-01-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
07-01-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
07-01-2026
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
07-01-2026
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
07-01-2026
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
07-01-2026
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
07-01-2026
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
07-01-2026
TAARIFA KWA UMMA
07-01-2026