Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema ujio wa nyota maarufu wa filamu nchini China, Jin Dong, utaendelea kuifungulia Zanzibar soko la Utalii kutoka China.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema ujio wa nyota maarufu wa filamu nchini China, Jin Dong, utaendelea kuifungulia Zanzibar soko la Utalii kutoka China.
Dk. Mwinyi ameyasema hayo Ikulu, Zanzibar alipotembelewa na msanii huyo ambaye yupo Zanzibar kwa kazi ya kutengeneza filamu.
Alisema, ujio wake ni fursa adhimu kwa Zanzibar kutangazwa kimataifa hasa kupitia Sekta ya Utalii ambayo ni Sekta mama ya uchumi wa Taifa.
Rais Dk. Mwinyi alimueleza mgeni wake huyo, kwamba Zanzibar ina vivutio vingi vya Utalii, ukiwemo Utalii wa fukwe safi nyeupe zinazovutia wengi duniani, Utalii wa utamaduni, Utalii wa Mji mkongwe, Utalii wa michezo, Utalii wa visiwa pamoja na wa Mikutano.
Aidha, alimkaribisha mgeni huyo kuitumia fursa ya kuwepo kwake Zanzibar kutembelea maeneo muhimu ya Utalii likiwemo shamba la viungo vya Zanzibar, Kisiwa cha Mnemba, Kaskazini Unguja pamoja na Mji Mkongwe wa Zanzibar.
Naye, nyota huyo wa Filamu nchini China, Jin Dong, alimueleza Rais Dk. Mwinyi furaha yake ya kufika Afrika kwa mara ya kwanza tena ndani ya visiwa vya Zanzibar kwa nchi za Afrika Mashariki.
Alisema, mbali na Safari ya Sanaa hapa Zanzibar lakini pia ujio wake unaimarisha uhusiano wa undugu na urafiki uliopo baina ya China na Tanzania ikiwemo Zanzibar.
Aliahidi kuwa balozi mzuri wa kuitangaza Zanzibar kwa Utalii na alieleza imani yake ya kuwavutia Wachina wengi kuja kutalii visiwa vya Zanzibar.
Miongoni mwa maeneo ya Utalii aliyotembezwa msanii huyo ni kisiwa cha Mnemba, Mji Mkongwe maeneo ya Forodhani na Ngome Kongwe.
Jin Dong ni nyota mkubwa China mwenye wafuasi wa mitandao ya kijamii zaidi ya milioni 15. Mbali na kazi za Sanaa pia ni Mwanasiasa nai Naibu Mkurugenzi wa kikundi cha Sanaa cha serikali cha utamaduni.
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
09-12-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
09-12-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
09-12-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
09-12-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
09-12-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
09-12-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
09-12-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
09-12-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
09-12-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
09-12-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
09-12-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
09-12-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
09-12-2025
TAARIFA KWA UMMA
09-12-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
09-12-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
09-12-2025