RAIS SAMIA KUJA NA "PROGRAM" YA KUSIKILIZA MWANANCHI MMOJA MMOJA.
Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ndg. Samia Suluhu Hassan ametangaza kutenga siku moja kila mwezi ili kusikiliza na kuzitafutia ufumbuzi kero za mwananchi mmoja mmoja.
Hatua hii imetangazwa na Katibu wa NEC Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM Ndg. Paul Makonda wakati akizungumza na wanahabari kwenye Ofisi Ndogo za CCM jijini Dar es Salaam.
"Hatua ya Rais inakuja ili kudhihirisha kwa vitendo tamanio lake la kuwataka watendaji wa serikali kutenga muda zaidi kusikiliza wananchi na kutatua kero zao mbalimbali." asema Makonda.
Sambamba na hayo CCM imewaelekeza viongozi wote wa serikali kutatua changamoto za wananchi kwa wakati kwakua kutofanya hivyo ni kuwachonganisha na Serikali yao.
"Maelekezo ya CCM kwa kila aliye na nafasi katika uongozi wa serikali ana wajibu wa kutatua changamoto za wananchi na afahamu kuwa ofisi si yake bali ni ya umma, kutotatua changamoto za wananchi ni kuwafanya wananchi kuichukia serikali yao na kukichukia Chama Cha Mapinduzi kinachoongozwa na mwenyekiti na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan." asema Makonda.
Pia, Makonda ametoa tathmini ya ziara mikoani ambapo hadi kufikia sasa Idara ya Itikadi, Uenezi na Mafunzo imefika mikoa 23 na kufanya mikutano 247 na kukutana na changamoto zaidi ya 2000.
"CCM tunawashukuru sana waandishi wa habari kwa namna ambavyo mmekuwa bega kwa bega kuhabarisha umma juu ya mambo mengi mema yanayofanywa na serikali ya awamu ya sita inayotokana na chama Cha Mapinduzi inayoongozwa na Mwenyekiti na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan."
Ndg. Paul Makonda amefanya Mkutano na waandishi wa habari leo Machi 5, 2024 katika ofisi ndogo za CCM Lumumba jijini Dar es Salaam.
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
09-12-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
09-12-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
09-12-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
09-12-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
09-12-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
09-12-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
09-12-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
09-12-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
09-12-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
09-12-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
09-12-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
09-12-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
09-12-2025
TAARIFA KWA UMMA
09-12-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
09-12-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
09-12-2025