RAIS SAMIA KUJA NA "PROGRAM" YA KUSIKILIZA MWANANCHI MMOJA MMOJA.
Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ndg. Samia Suluhu Hassan ametangaza kutenga siku moja kila mwezi ili kusikiliza na kuzitafutia ufumbuzi kero za mwananchi mmoja mmoja.
Hatua hii imetangazwa na Katibu wa NEC Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM Ndg. Paul Makonda wakati akizungumza na wanahabari kwenye Ofisi Ndogo za CCM jijini Dar es Salaam.
"Hatua ya Rais inakuja ili kudhihirisha kwa vitendo tamanio lake la kuwataka watendaji wa serikali kutenga muda zaidi kusikiliza wananchi na kutatua kero zao mbalimbali." asema Makonda.
Sambamba na hayo CCM imewaelekeza viongozi wote wa serikali kutatua changamoto za wananchi kwa wakati kwakua kutofanya hivyo ni kuwachonganisha na Serikali yao.
"Maelekezo ya CCM kwa kila aliye na nafasi katika uongozi wa serikali ana wajibu wa kutatua changamoto za wananchi na afahamu kuwa ofisi si yake bali ni ya umma, kutotatua changamoto za wananchi ni kuwafanya wananchi kuichukia serikali yao na kukichukia Chama Cha Mapinduzi kinachoongozwa na mwenyekiti na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan." asema Makonda.
Pia, Makonda ametoa tathmini ya ziara mikoani ambapo hadi kufikia sasa Idara ya Itikadi, Uenezi na Mafunzo imefika mikoa 23 na kufanya mikutano 247 na kukutana na changamoto zaidi ya 2000.
"CCM tunawashukuru sana waandishi wa habari kwa namna ambavyo mmekuwa bega kwa bega kuhabarisha umma juu ya mambo mengi mema yanayofanywa na serikali ya awamu ya sita inayotokana na chama Cha Mapinduzi inayoongozwa na Mwenyekiti na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan."
Ndg. Paul Makonda amefanya Mkutano na waandishi wa habari leo Machi 5, 2024 katika ofisi ndogo za CCM Lumumba jijini Dar es Salaam.
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
25-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
25-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
25-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
25-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
25-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
25-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
25-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
25-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
25-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
25-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
25-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
25-05-2026
𝗞𝗜𝗦𝗛𝗜𝗡𝗗𝗢 𝗖𝗛𝗔 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗖𝗛𝗔𝗣𝗢𝗞𝗘𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗛𝗔𝗡𝗚𝗪𝗘 𝗗𝗔𝗥 𝗘𝗦 𝗦𝗔𝗟𝗔𝗔𝗠
25-05-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
25-05-2026
𝗩𝗜𝗝𝗔𝗡𝗔 𝗧𝗨𝗜𝗟𝗜𝗡𝗗𝗘 𝗔𝗠𝗔𝗡𝗜 𝗬𝗔 𝗡𝗖𝗛𝗜 𝗬𝗘𝗧𝗨 - 𝗠𝗪𝗘𝗡𝗘𝗭𝗜 𝗞𝗘𝗡𝗔𝗡𝗜
25-05-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
25-05-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
25-05-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
25-05-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
25-05-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
25-05-2026