Wazazi na walezi wametakiwa kutoa ushirikiano kwa walimu wa madrasa na walimu wa skuli pamoja na kujua taarifa na mienendo ya watoto wao ili kupata wataalamu na wanazuoni wabobezi wa baabae.
Hayo yamesemwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Alhajj Hemed Suleiman Abdulla wakati akiwasalimia waumini wa Masjid IITISWAM uliopo TUNGUU KWA SHEMEGO Wilaya ya Kati Unguja mara baada ya kumaliza Ibada ya Sala ya Ijumaa.
Amesema kuwa kuwafatilia vijana katika suala zima la kupata elimu zote mbili kutapelekea kupata walaalamu watakao weza kulisaidia Taifa katika kusimamia miradi mbali mbali ya kimaendeleo pamoja na kupata wanazuoni watakao watakaoitetea dini ya kiislamu kwa ushahidi wa Qur-an na Sunna.
Alhajj Hemed amesema suala la wazazi na walezi kuwasiamamia vijana katika mambo mema yakiwemo suala la Elimu na Ibada ni suala la lazima kwani kufanya hivyo ni kutimiza wajibu wao na kujiweka huru na masuala mbele ya M.Mungu kwani kila mzazi ni mchunga juu ya mtoto wake.
Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar amesema kuwa maisha ya duniani ni mapito tu hivyo ni lazima kujiandaa kwa kufanya Ibada pamoja na kuwaandaa watoto katika suala zima la kuwapatia elimu yenye manufaa hapa duniani na kesho akhera.
Sambamba na hayo Alhajj Hemed amewataka wazazi na walezi kuwafuatilia watoto wao wanaoingia skuli katika mkondo wa jioni kwa skuli ambazo bado wanafanya hivyo kwani serikali ya awamu ya Nane (8) inayoongozwa na Dkt. Hussein Ali Mwinyi inahakikisha inaendelea kujenga skuli za ghorofa kila sehemu ili kuwawezesha wanafunzi kusoma mkondo mmoja tu na kupata elimu iliyobora kwa maslahi ya taifa.
Mapema akitoa Khutba katika Sala ya Ijumaa, Ustadh. RAJAB R’DHAN CHOUM amewaasa waumini wa Dini ya Kiislam hasa wale waliomo kwenye Ndoa kuacha tabia ya kutoa Talaka kiholela jambo ambalo linamkirihisha sana Allah (S.W) na kupelekea kuwasambaratisha watoto na kukosa malezi yaliyo bora kutoka kwa wazazi wawili.
Amesema kuwa kumekuwa na tabia kwa baadhi ya wazazi kususiana watoto wanapoachana huku wakijua kuwa kufanya hivyo ni kuwakosesha haki zao za msingi na kupelekea Taifa kuwa na watoto wengi wa mtaani na kuongezeka kwa mambo maovu na machafu baina yao.
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐌𝐏𝐀 𝐁𝐀𝐉𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐒𝐈𝐇𝐀 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐘𝐄 𝐔𝐋𝐄𝐌𝐀𝐕𝐔 𝐖𝐀 𝐌𝐈𝐆𝐔𝐔
31-05-2026
MAWENZI YAVUNJA REKODI: MITUNGI 3,313 YA OKSIJENI YAZALISHWA KWA MIEZI 6, ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 126 ZAOKOLEWA!
31-05-2026
MAFURIKO YA WANANCHI WA SIHA KWENYE MKUTANO MKUBWA WA HADHARA
31-05-2026
MAPOKEZI YA KATIBU MWENEZI WA CCM NDUGU KENANI L KIHONGOSI MKOANI KILIMANJARO
31-05-2026
🔰 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐒𝐇𝐈𝐍𝐃𝐎 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
31-05-2026
CCM INAWATAKIA HERI YA SIKUKUU YA EID AL ADHA
31-05-2026
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
31-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
31-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
31-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
31-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
31-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
31-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
31-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
31-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
31-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
31-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
31-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
31-05-2026
𝗞𝗜𝗦𝗛𝗜𝗡𝗗𝗢 𝗖𝗛𝗔 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗖𝗛𝗔𝗣𝗢𝗞𝗘𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗛𝗔𝗡𝗚𝗪𝗘 𝗗𝗔𝗥 𝗘𝗦 𝗦𝗔𝗟𝗔𝗔𝗠
31-05-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
31-05-2026