CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar kimesema kitaendelea kutunza,kuthamini na kuenzi hazi na ya wazee waliohudumu kwa uadilifu mkubwa katika nafasi mbalimbali za utumishi ndani ya Chama na Serikalini kwa ujumla.
Hayo ameyasema Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dkt.Mohamed Said Dimwa,katika ziara yake ya kuwatembelea wazee mbalimbali wa Chama hicho katika maeneo mbalimbali ya Unguja.
Alisema maendeleo yaliyopatikana nchini yalijengewa misingi imara na wazee hao enzi za utumishi wao hivyo wana mchango mkubwa katika mafanikio yaliyofikiwa hivi sasa ndani ya Chama Cha Mapinduzi na Serikali zake zote mbili zikiwemo ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Zanzibar.
Katika maelezo yake Naibu Katibu Mkuu huyo Dkt.Dimwa, alieleza kuwa Chama Cha Mapinduzi kinajivunia kwa kuwa na wazee mbalimbali wenye uzoefu na upeo mkubwa wa maarifa ya kushauri mambo mbalimbali yenye kuleta tija.
“Watu wengi wanajiuliza kwa nini CCM kila siku inazidi kuimarika ni kutokana na uwepo wa Wazee awa ambao wengi wao walifanya kazi kubwa ya utumishi katika maeneo mbalimbali ya Chama na Serikali na wanaendelea kutushauri mambo mema yanayoleta ufanisi ndani ya taasisi yetu.”, alisema Dkt.Dimwa.
Kupitia ziara hiyo aliwasisitiza Viongozi na Watendaji mbalimbali wa Chama na Jumuiya zake Zanzibar kuendeleza utamaduni wa kuwatembelea wazee na makundi mengine yenye mahitaji maalum ili nao wajione bado wanakumbukwa na kuthaminiwa juu ya kazi kubwa waliofanya katika kuimarisha maendeleo ya nchi.
Dkt.Dimwa, amewatembelea wazee mbalimbali wakiwemo Kadhi Mkuu wa Zanzibar mstaafu Sheikh Khamis Haji Khamis,kada wa CCM ndugu Waalidi Psinarie Kavishe, aliyekuwa Mkuu wa Mkoa Kusini Pemba ndugu Salum Juma Tindwa na aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Wanawake na Watoto Zanzibar ndugu Msham Abdallah Khamis katika ziara hiyo pia alitoa sadaka mbalimbali kwa ajili ya kuwafariji.
Akitoa shukrani zake kada wa CCM ambaye ni miongoni mwa Wazee waliotembelewa ndugu Waalidi Kavishe, amempongeza Naibu Katibu Mkuu huyo Dkt. Dimwa kwa ziara yake hiyo iliyojenga matumaini na upendo kwa wazee hao ambao nao wamejiona wanakumbukwa na viongozi wa sasa.
Ndugu Kavishe,alitoa wito kwa viongozi,watendaji na wanachama wa CCM nchini kuhakikisha Chama Cha Mapinduzi kinashinda kwa kura nyingi katika uchaguzi mkuu ujao wa dola wa mwaka 2025.
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
09-12-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
09-12-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
09-12-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
09-12-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
09-12-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
09-12-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
09-12-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
09-12-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
09-12-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
09-12-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
09-12-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
09-12-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
09-12-2025
TAARIFA KWA UMMA
09-12-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
09-12-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
09-12-2025