TUMEFURAHISHWA NA MAFUNZO
Viongozi na watendaji wa CCM na jumuiya zake katika Mkoa wa Lindi, wamesema wamefurahishwa na hatua iliyochukuliwa na Chama ya kuwapatia mafunzo ya falsafa, itikadi na sera za CCM .
Wamesema hayo kwa nyakati tofauti, jana Oktoba 16 na leo Oktoba 17, 2023, walipokuwa wakitoa salamu za pongezi kwa Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Ndg. Sophia Mjema, ambaye Idara anayoiongoza ndiyo inayoratibu mafunzo hayo yaliyoanza kutolewa mkoani humo Oktoba 11 hadi 16, 2023.
Katibu wa CCM wa Mkoa wa Lindi, Ndg. Barnabas Esau, amesema mafunzo hayo yamekuwa ni elimu muafaka kwa viongozi na watendaji wa CCM na jumuiya zake.
"Sasa kila mmoja anajua wajibu wake barabara, tunashukuru sana kwa uamuzi wa kutuletea mafunzo mpaka huku ngazi za chini," amesema.
Kiongozi mstaafu, Ndg. Benigno Matei Makwinya, amesema ni miaka mingi imepita tangu kupatiwa mafunzo ya aina hiyo.
Ndg. Makwinya, ambaye ni mwenyekiti wa CCM wa mkoa mstaafu, na aliwahi kuwa diwani na mwenyekiti wa Halmashauri ya Mtama, amesema enzi za TANU mafunzo kama hayo yalikuwa yakitolewa kwa wanachama.
"Uamuzi huu wa kutoa mafunzo kwa viongozi na wanachama unapaswa kuendelea, toeni mafunzo nchini kote, sisi wanachama wa TANU tulikuwa tunafundishwa," amesema.
Ndg. Makwinya amemtuma Ndg. Mjema kufikisha salamu za shukurani kwa Mwenyekiti wa CCM, Rais Samia Suluhu Hassan, kwa kupatiwa mafunzo hayo.
Mapema, Ndg. Mjema alisema mafunzo hayo yalizinduliwa mkoani Dar es Salaam na yamepangwa kufanyika nchini kote, ikiwa ni utekelezaji wa moja ya maazimio ya Mkutano Mkuu wa 10 wa CCM uliofanyika 2022.
Ndg. Mjema amesema ni matarajio baada ya mafunzo viongozi na watendaji wa Chama na Jumuiya zake, wataimarika kwa kila mmoja kuelewa kwa ufasaha kazi na majukumu yake ndani na nje ya Chama.
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
08-01-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
08-01-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
08-01-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
08-01-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
08-01-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
08-01-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
08-01-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
08-01-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
08-01-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
08-01-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
08-01-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
08-01-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
08-01-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
08-01-2026
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
08-01-2026
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
08-01-2026
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
08-01-2026
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
08-01-2026
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
08-01-2026
TAARIFA KWA UMMA
08-01-2026