Makao Makuu - Dodoma
#CCM Imetimia KaziIendelee

Habari na Matukio Mbalimbali


DKT SAMIA AMELETA MAPINDUZI MAKUBWA SEKTA YA ELIMU - CPA MAKALLA 

alternative

Shule za High School zilikuwa chache lakini leo zipo kila Mkoa, Miongoni mwao za Wasichana zikiwa na Michepuo ya Sayansi

Katibu wa NEC-Itikadi Uenezi na Mafunzo wa CCM Taifa Ndugu Amos Makalla leo Septemba 05, 2024 amekagua Ujenzi katika Sekondari ya Samia ya Wasichana Mchepuo wa Sayansi iliyopo Wilayani Longido Mkoani Arusha.

CPA. Makalla akiambatana na Viongozi wa Serikali na Chama cha Mapinduzi (CCM) amezungumza na Wanafunzi na Walimu kwenye Sekondari hiyo, ambapo amesema Rais na Mwenyekiti wa Chama hicho Dkt Samia Suluhu Hassan amefanikiwa kuleta mapinduzi Makubwa Kwenye Sekta ya Elimu hapa nchini.

"Nataka niwaambie kitu kimoja kuwa, tumefika hapa kwa Sababu enzi hizo nasi tulisoma kama Ninyi, kwa hiyo mnapaswa kuongeza Jitihada kwenye masomo ili nanyi muwe Viongozi Bora kwa Siku zinazokuja"

"Pongezi nyingi zimuendee Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuleta Mapinduzi makubwa kwenye sekta ya Elimu, kwa Sababu Zamani high school zilikuwa Chache, lakini Rais Dkt Samia amefanya mapinduzi kwenye Elimu, ambapo kwa Sasa Kila Mkoa unayo shule ya Mfano ya Wasichana Mchepuo wa Sayansi, hayo ni maono yake na Sisi kama Chama hatuna budi kupongeza na kuunga mkono Jitihada zake" amesema CPA. Makalla. 

🗓️05 Septemba,2024.
📍 Longido Samia girls Secondary school 

 

alternative alternative alternative alternative
Habari Nyingine

Nukuu za Viongozi