SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR IMEAMUA KUWEKA MFUMO WA RUFAA KWA HOSPITALI ZOTE ZA WILAYA NCHINI.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi aliyasema hayo kwenye ziara ya kuutembelea mkoa wa Kaskazini Unguja alipozindua hospitali ya Wilaya, Kivunge. Alisema, Serikali imeweka utaratibu huo kwa lengo la kuimarisha huduma bora za Afya ziwe za uhakika zikiwemo Maabara, X-ray, ultrasound mashine za kisasa na dawa na nyengine kwa maradhi yote ya kawaida ikiwemo uzazi, huduma za uchunguzi na mengine ili kupunguza msongamano kwenye hospitali kuu ya Mnazi Moja. Aidha, aliwataka wananchi wote kurejesha imani zao kwa hospitali za Serikali kwani sasa zinatoa huduma bora na zina dirisha maalum za mfuko wa bima ya afya na kuwasisitiza watoa huduma kwenye hospitali hizo kuharakisha huduma zao sio kuweka misongamano ya wagonjwa. Pia, Rais Dk. Mwinyi aliwatoa hofu watumishi wa Serikali na ajira zao na kuwaeleza licha ya Serikali kushirikisha sekta binafsi kwenye hospitali hizo ajira zao zitaendelea kuwa salama.
Vilevile, Dk. Mwinyi alihimiza umuhimu wa kuweka kambi maalumu na wataamu wa maradhi mbalimbali ikiwemo macho, moyo, meno na mifupa.
Naye, Waziri wa Afya, Nassor Ahmed Mazrui alisifu juhudi za Rais Dk. Mwinyi kuimarisha miundombinu ya sekta ya Afya kwa ujenzi wa hospitali 10 za Wilaya Unguja na Pemba pamoja na hospitali moja ya Mkoa.
Akiwa ziarani Mkoa wa Kaskazini Unguja, Rais Dk. Mwinyi aliweka jiwe la msingi kwenye ujenzi wa Skuli ya msingi ya ghorofa mbili Donge, itakayokuwa na madarasa 29, ofisi za walimu, mwalimu mkuu, vyumba vya maktaba, maabara, vyumba vya TEHAMA (ICT), vyoo, stoon na chumba cha kusalia.
Pia, Rais Dk. Mwinyi alisifu juhudi za maendeleo zilizofikiwa na sekta ya elimu, Zanzibar kupita malengo ya ilani ya uchaguzi ya CCM ya 2020 – 2025 ikiwemo kukamilika kwa skuli za kisasa za ghorofa na madarasa yatakayochukua wanafunzi 45 kwa mkondo mmoja tuu.
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali, Lela Muhamed Mussa, alipongeza juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kuimarisha miundombinu ya kisasa kwenye sekta ya elimu ndani ya kipindi cha miaka mitatu ya uongozi wa Dk. Mwinyi kwa kuwa na miradi ya kimkakati ya skuli za kisasa.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja, Ayoub Mahmoud alieleza mafaniko ya mkoa huo ikiwemo kuimarika sekta za miundombinu ya barabara, bandari pamoja na huduma za jamiii, maji safi, vituo vya afya, kukamilika kwa soko la kisasa Donge Mtambile litakalotosheleza mahitaji wa wananchi wa eneo hilo na maeneo jirani.
Alisema, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imetoa michango mkubwa kutekeza miradi mikubwa ya maendeleo ya mkoani humo. Ziara ya Rais Dk. Mwinyi Mkoa wa Kaskazini Unguja ni mwendelezo wa ziara zake za kukagua miradi ya maendeleo ikiwa ni kuanza shamrashamra na sherehe za mafaniko ya uongozi wake unaotimiza miaka mitatu.
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
09-12-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
09-12-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
09-12-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
09-12-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
09-12-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
09-12-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
09-12-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
09-12-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
09-12-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
09-12-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
09-12-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
09-12-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
09-12-2025
TAARIFA KWA UMMA
09-12-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
09-12-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
09-12-2025