Makao Makuu - Dodoma
#CCM Imetimia KaziIendelee

Habari na Matukio Mbalimbali


BALOZI NCHIMBI MSIBANI KWA TIXON NZUNDA
 

alternative

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk Emmanuel John Nchimbi amejumuika pamoja na waombolezaji wengine, kutoa heshima za mwisho na kuaga mwili wa aliyekuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mhe. Tixon Nzunda, shughuli iliyofanyika nyumbani kwa marehemu, Goba jijini Dar Es Salaam. 

Balozi Dk Nchimbi, ambaye alisoma pamoja na marehemu Nzunda Chuo Kikuu Mzumbe, pia aliwapatia pole familia ya marehemu kwa msiba huo, baada ya kusaini kitabu cha maombolezo.

Mwili wa marehemu Nzunda, ambaye alifariki kwa ajali ya gari Juni 18, 2024 huko wilayani Hai, unatarajiwa kuzikwa nyumbani kwao, mkoani Songwe, Juni 22, 2024.

alternative alternative alternative alternative
Habari Nyingine

Nukuu za Viongozi