RAIS WA ZANZIBAR DKT HUSSEN ALI MWINYI AMESEMA SERIKALI IMEWEKA MKAZO MKUBWA KATIKA KUHAKIKISHA MAENEO YA URITHI YANAPEWA KIPAUMBELE ILI KUENDANA NA MAKUBALIANO YA MKATABA WA KIMATAIFA WA UNESCO WA MWAKA 1972.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe Dkt Hussen Ali Mwinyi amesema Serikali ya Awamu ya Nane (8) imeweka mkazo mkubwa katika kuhakikisha maeneo ya urithi yanapewa kipaumbele hususan Mji Mkongwe ili kuendana na makubaliano ya Mkataba wa Kimataifa wa UNESCO wa mwaka 1972.
Ameyasema hayo katika Hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe Hemed Suleiman Abdulla kwenye sherehe ya siku ya Mji Mkongwe iliyofanyika katika Viwanja vya Bustani ya Forodhani Zanzibar.
Rais Dkt Mwinyi amesema pato kubwa la nchi yetu linategemea sana Sekta ya Utalii hivyo kuna umuhimu mkubwa wa kuutunza Mji Kongwe ili kutanua wigo wa vyanzo vya utalii ikiwemo utalii wa maeneo ya historia ambao unaonekana kushamiri zaidi duniani katika miaka ya hivi karibuni.
Amefahamisha kuwa katika kuhakikisha azma hiyo inafikiwa, Serikali imepanga kuchukua hatua mbali mbali ikiwemo kuyafanyia ukarabati majengo yote makongwe katika eneo la Mji Mkongwe sambamba na kuboresha maeneo yote ya wazi ikijumuisha Bustani ya Jamhui Garden, Victoria Garden, African House pamoja na maeneo ya maegesho ya magari.
Aidha Dkt Mwinyi amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imekusudia kutandaza upya Mfumo wa Maji na Umeme chini ya ardhi ili kuondokana na mabomba ya maji na waya zilizotapakaa kila sehemu ambazo zinaondoa haiba ya Mji Mkongwe.
Rais Dkt Mwinyi amesema Serikali imekuwa ikiiagiza Wizara pamoja na Mamlaka ya Hifadhi na Uendelezaji wa Mji Mkongwe kuhakikisha wanaleta mapinduzi makubwa ya uhifadhi wa Mji huo kwa kuupanga upya katika kudumisha usafi, kuziboresha bustani zote za Mji Mkongwe, uondoaji wa biashara katika maeneo yasiyo rasmi pamoja na kuhakikisha usalama wa wageni.
Sambamba na hayo Dkt Mwinyi amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inaendelea kuimarisha mazingira bora kwa wafanyakazi na wajasiriamali kwa kuimarisha maeneo ya biashara kwa kujenga masoko ya kisasa na kujipanga ili kuweka Mabasi maalum yatakayotoa huduma ya usafiri katika eneo la Mji Mkongwe kwa lengo la kupunguza msongamano wa vyombo vya usafiri ambao unahatarisha usalama wa Majengo na kuleta usumbufu kwa watalii na jamii kwa ujumla.
Nae Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale Mhe. SIMAI MOHAMMED SAID amesema wataendelea kushirikiana na wananchi na wakaazi wa Mji Mkongwe katika kuuendeleza Mji huo kwa kupanga na kutatua changamoto ili kuzidi kuupa hadhi Mji Mkongwe wa Zanzibar.
Amesema kuwa Serikali Kupitia Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale imejipanga kuiboresha Bustani ya Forodhani ambayo imekuwa ni kivutio kikubwa cha muda mrefu kwa watalii wanaofika Zanzibar ili iweze kuwa Bustani ya Mfano ndani na nje ya zanzibar.
Sambamba na hayo Mhe Simai amesema wizara itahakikisha Vivutio vyote vya Utalii vya Unguja na Pemba vitaendelea kuboreshwa na kuendelezwa kwa maslahi mapana ya nchi na vizazi vijavyo.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mamlaka ya Uhifadhi na Undelezaji wa Mji Mkongwe Muhandisi ALI SAID BAKAR amesema Mamlaka imejipanga kuhakikisha Mji Mkongwe wa Zanzibar unaendana na hadhi ya Urithi wa Miji Mkongwe ya Dunia sambamba na kulinda Utamaduni wa Zanzibari ili uendane na Matakwa ya UNESCO
Akizungumza kwa niaba ya Mwakilishi Mkaazi wa UNESCO Tanzanian Bibi NANCY MWAISAKA amesema UNESCO inaamini kuwa Urithi wa Mji Mkongwe umeleta maendeleo makubwa na kukuza kipato kwa wanannchi.
Aamefahamisha kuwa Taifa lolote lisilo na utambulisho wa aina yoyote ile Taifa hilo hukosa maendeleo hivyo ameiomba serikali ya mapinduzi ya Zanzibar kuulinda, kuuhifadhi na kuuendeleza Utamaduni na Urithi wa Mji Mkongwe kwa maslahi ya Taifa la Tanzania.
Nancy ameihakikishia Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuwa UNESCO itaendelea kufanya kazi bega kwa bega na Serikali katika kulinda Utamaduni wa Zanzibar na wapo tayari kutoa ushirikano katika kufanikisha Matakwa ya Kimataifa juu ya Uhifadhi na Urithi wa Mji Mkongwe
MAFURIKO YA WANANCHI WA SIHA KWENYE MKUTANO MKUBWA WA HADHARA
30-05-2026
MAPOKEZI YA KATIBU MWENEZI WA CCM NDUGU KENANI L KIHONGOSI MKOANI KILIMANJARO
30-05-2026
🔰 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐒𝐇𝐈𝐍𝐃𝐎 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
30-05-2026
CCM INAWATAKIA HERI YA SIKUKUU YA EID AL ADHA
30-05-2026
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
30-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
30-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
30-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
30-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
30-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
30-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
30-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
30-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
30-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
30-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
30-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
30-05-2026
𝗞𝗜𝗦𝗛𝗜𝗡𝗗𝗢 𝗖𝗛𝗔 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗖𝗛𝗔𝗣𝗢𝗞𝗘𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗛𝗔𝗡𝗚𝗪𝗘 𝗗𝗔𝗥 𝗘𝗦 𝗦𝗔𝗟𝗔𝗔𝗠
30-05-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
30-05-2026
𝗩𝗜𝗝𝗔𝗡𝗔 𝗧𝗨𝗜𝗟𝗜𝗡𝗗𝗘 𝗔𝗠𝗔𝗡𝗜 𝗬𝗔 𝗡𝗖𝗛𝗜 𝗬𝗘𝗧𝗨 - 𝗠𝗪𝗘𝗡𝗘𝗭𝗜 𝗞𝗘𝗡𝗔𝗡𝗜
30-05-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
30-05-2026