Makao Makuu - Dodoma
#CCM Imetimia KaziIendelee

Habari na Matukio Mbalimbali


CCM HAITASHIKA DOLA KWA MABAVU WALA BUNDUKI BALI KWA DEMOKRASIA - NDG. GAVU

alternative

> Awataka wana CCM kutumia uchaguzi wa serikali za mitaa kutuma salamu za ushindi mkubwa kwa Rais Samia katika uchaguzi wa mwaka 2025 

Katibu wa NEC - Oganaizesheni Ndugu. Issa Haji Gavu , amesema kuwa Chama Cha Mapinduzi kama ilivyo kawaida yake kamwe hakitashika dola kwa mabavu wala kutumia bunduki bali kitashika dola kwa hali ya kidemokrasia.

Ndugu. Gavu ameyasema hayo wakati akizungumza kwenye mkutano uliokutanisha Viongozi wa Chama, Serikali, Taaisis ziziso za kiserikali, Viongozi wa Dini, Wazee na Machifu.

"Hatutashika dola kwa mabavu wala bunduki bali tutashika dola kwa hila za kidemokrasia"

"Msingi wa demokrasia ni kupiga kura, ili mwanadamu ashawishike basi una wajibu wa kumshawishi kabla ya kupiga kura"

"Tuhakikishe tunaendelea kuhamasisha na kuchapa kazi kwakuwa ndio kitu pekee kitakachoendelea kutupa thamani kwa wananchi kuendelea kutuamini"

"Tutumie uchaguzi wa serikali za mitaa kama salamu za ushindi atakaokwenda  kuupta Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ifikapo mwaka 2025"

🗓️16 Aprili, 2024
📍Mbozi - Songwe

alternative alternative alternative alternative
Habari Nyingine

Nukuu za Viongozi