RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi amesifu fursa kubwa ya biashara iliyopo baina ya Tanzania ikiwemo Zanzibar na Visiwa vya Comoro.
Rais Dk. Mwinyi ameyaeleza hayo Ikulu Zanzibar, alipozungumza na Balozi mpya wa Tanzania nchini Comoro Mhe. Said Othman Yakoub aliefika kumuaga baada ya kuteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Dk. Samia Suluhu Hassan tarehe 13 April, mwaka huu.
Katika mazungumzo yao wamegusia kuendeleza makubaliano yaliyopo baina ya Zanzibar na Comoro hasa kwenye nyanja za Elimu kupitia Chuo Kikuu cha Zanzibar (SUZA) na vyuo vya Comoro, sekta ya Usafirishaji, Afya, Biashara na vyombo vya habari kupitia Shirika la Utangazaji la Zanzibar (ZBC) na Shirika la Utangazaji la Comoro.
Alisema, ishara ya uhusiano mzuri baina ya pande hizo mbili ni utekelezaji wa Makubaliano ambayo awali yaliazimiwa na pande mbili hizo sambamba na uhusiano wa damu uliopo baina ya Zanzibar na Comoro.
Rais Dk. Mwinyi alisema, sekta ya biashara ni fursa adhimu kwa Zanzibar kunufaika na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Shirika la Meli tayari imeagiza meli mbili zitakazofanya safari zake ikiwemo visiwa vya Comoro sambamba na meli ya MV Mapinduzi ambayo imefanyiwa matengezo makubwa na inatarajiwa kujeresha safari zake visiwani Comoro.
Akizungumzia suala la usafirishaji na ufanisi hasa kwa bandari za Zanzibar, Rais Dk. Mwinyi alisema, Serikali inazifanyia maboresho makubwa ili kurejesha ufanisi wa handari hizo. Pia Rais Dk. Mwinyi alieleza kuhusu usafiri wa anga kwamba utakuwa na tija kubwa kwa fursa za biashara baina ya Zanzibar na Comoro.
Dk. Mwinyi pia aligusia sekta ya Afya, akimweleza Balozi Said kwamba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ina nia ya kukuza Utalii wa matibabu nchini kupitia hospitali ya Mkoa ya Lumumba iliyopo Mkoa wa Mjini Magharibi inayotarajiwa kupokea watalii wengi wa matibabu kutoka mataifa mbalimbali ya dunia ikiwemo visiwa vya Comoro.
Hata, hivyo Rais Dk. Mwinyi alieleza uhusiano baina ya Zanzibar na Comoro ni maalum ni wa damu na undugu na amemuahidi Balozi Said kwamba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kushirikiana na Serikali ya Comoro wataangalia uwezekano wa kuanzisha ubalozi mdogo wa Comoro Zanzibar na kuahidi Serikali itatoa ushirikiano wa hali ya juu kwenye eneo hilo ilkiwemo kuwasaidia jengo la ubalozi huo.
Pia Rais Dk. Mwinyi ametumia fursa hiyo kumpongeza Balozi Saidi kwa kuteuliwa kuiwakilisha Tanzania kwenye visiwa vya Comoro na kumuahidi kumpa ushirikiano wa hali ya juu kwenye majukumu yake ya kuitangaza na kuitekeleza kwa vitendo Diplomasia ya Uchumi ya Tanzania.
Kwa upande wake, Balozi Said amemshukuru Rais Dk. Mwinyi kwa nasaha na maelekezo yake na kumuahidi kuitangaza vyema nchi na kuzitumia fursa zinazopatikana Comoro kwa maslahi ya Tanzania ikiwemo Zanzibar.
Alisema Kariakoo, Dar es Salaam na Zanzibar ni vitovu vya biashara baina ya Tanzania na Comoro ambako awali wafanyabiashara wengi waliingia nchini na kufanya vizuri zaidi kwenye Sekta ya biashara.
Alisema hadi mwaka jana Soko la Kariako, Dar es Salaam lilikusanya zaidi dola milioni 54 sawa na bilioni 145 kwa mwaka.
Kuhusu Sekta ya Afya, Balozi Said alisema Comoro ni fursa adhimu ya Tanzania kuendelea kunufaika nayo kwani inaleta watalii wengi wa matibabu nchini.
Alisema kwa mwaka jana zaidi ya wagonjwa 14, 300 raia wa Comoro waliingia nchini kwaajili ya matibabu, sawa na wastani wa wagonjwa 12,000 kwa mwezi, wagonjwa 300 kwa wiki na 42 kwa siku ambao hutibiwa Tanzania.
Balozi Saidi alisema, kuanzishwa kwa hospitali ya Mkoa ya Lumumba, Zanzibar ni fursa adhimu kwa Sekta ya Afya Zanzibar kupitia uhusiano wa kindugu uliopo baina ya Comoro na Zanzibar.
Aidha, Balozi Saidi alipongeza juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kudhamiria kuongeza meli mbili zitakazoleta tija na kuimarisha uhusiano uliopo baina ya Comoro na Zanzibar hasa kwenye sekta ya usafirishaji na biashara na kuwataka Watanzania hususani Wazanzibari kuitumia fursa hiyo adhimu ya kukuza uchumi wa nchi.
Balozi Saidi pia amesifu ushirikiano uliopo baina ya Comoro na Tanzania hasa kwenye usafiri wa anga kwa kuwepo safari mbili kwa siku baina ya Tanzania na Comoro kupitia ndege za “Precian Air” na Air Tanzania ambazo pia alizieleza kuwa ni fursa lukuki kwa wa Tanzania kuwanufaisha kiuchumi na kijamii.
Uhusiano wa Diplomasia baina ya Tanzania na Comoro ni wa kihistoria, ambapo Comoro ilifungua ubalozi wake Dar es Salaam mwaka 2013 na mwaka mmoja baadae Tanzania ilifungua ubalozi wake jijini Moroni, Comoro mwaka 2014. Mwaka jana 2023, pande mbili hizo za Diplomasia zilianzisha Tume ya kudumu ya pamoja (JPC) ambapo mwezi Julai mwaka huu inatarajiwa kufanya mkutano wa pamoja utakaotoa wawakilishi baina yao.
KIPINDI MAALUMU
09-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐒𝐈𝐌𝐀𝐌𝐈𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐒𝐀𝐅𝐀𝐑𝐀 𝐊𝐔𝐒𝐀𝐋𝐈𝐌𝐈𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐍𝐀 𝐊𝐈𝐉𝐈𝐖𝐄 𝐂𝐇𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐃𝐄𝐌𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈
09-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐊𝐈𝐓𝐔𝐎 𝐂𝐇𝐀 𝐀𝐅𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐋𝐎𝐋𝐄𝐍𝐈, 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈
09-06-2026
𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐘𝐀𝐀𝐌𝐁𝐈𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐂𝐇𝐀𝐆𝐔𝐀 𝐌𝐀𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐎 𝐁𝐀𝐃𝐀𝐋𝐀 𝐘𝐀 𝐌𝐀𝐀𝐍𝐃𝐀𝐌𝐀𝐍𝐎
09-06-2026
𝐌𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐓𝐈𝐁𝐔 𝐖𝐀 𝐍𝐄𝐂, 𝐈𝐓𝐈𝐊𝐀𝐃𝐈, 𝐔𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐍𝐀 𝐌𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐎 𝐂𝐂𝐌, 𝐍𝐃𝐔𝐆𝐔 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐋𝐀𝐁𝐀𝐍 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈, 𝐎𝐅𝐈𝐒𝐈 𝐙𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈
09-06-2026
𝐒𝐀𝐒𝐀 𝐍𝐈 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈, 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐃𝐎 𝐌𝐃𝐔𝐍𝐃𝐎!
09-06-2026
𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔 𝐘𝐀𝐒𝐈𝐊𝐈𝐀 𝐖𝐈𝐓𝐎 𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐋𝐈𝐍𝐃𝐀 𝐌𝐀𝐀𝐃𝐈𝐋𝐈 𝐍𝐀 𝐇𝐀𝐊𝐈 𝐙𝐀 𝐖𝐀𝐓𝐎𝐓𝐎
09-06-2026
𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐒𝐀𝐌𝐁𝐀𝐙𝐀 𝐔𝐏𝐄𝐍𝐃𝐎 𝐖𝐀 𝐀𝐆𝐀𝐏𝐄 𝐊𝐖𝐄𝐍𝐘𝐄 𝐊𝐈𝐉𝐈𝐖𝐄 𝐂𝐇𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐃𝐄𝐌𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔
09-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐀𝐍𝐙𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐊𝐀𝐆𝐔𝐀 𝐔𝐇𝐀𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐌𝐀
09-06-2026
𝐌𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐎 𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐀 𝐖𝐀 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐑𝐀𝐓𝐔 - 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀
09-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐓𝐔𝐍𝐔𝐊𝐈𝐖𝐀 𝐒𝐇𝐀𝐇𝐀𝐃𝐀 𝐘𝐀 𝐇𝐄𝐒𝐇𝐈𝐌𝐀 𝐔𝐑𝐔𝐒𝐈
09-06-2026
𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔, 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐀𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀!
09-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐑𝐀𝐒𝐌𝐈 𝐔𝐑𝐔𝐒𝐈, 𝐀𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐀 𝐍𝐀 𝐏𝐔𝐓𝐈𝐍
09-06-2026
𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎, 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀
09-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐌𝐎𝐒𝐂𝐎𝐖, 𝐔𝐑𝐔𝐒𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀
09-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐒𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐈𝐑𝐎 𝐊𝐖𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐊𝐀𝐙𝐈
09-06-2026
𝐅𝐔𝐍𝐆𝐀 𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐍𝐘𝐀𝐑𝐀 𝐋𝐄𝐎!!!
09-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐍𝐀. 𝟐 𝐊𝐀𝐓𝐀 𝐘𝐀 𝐁𝐎𝐍𝐆𝐀
09-06-2026
𝐁𝐀𝐁𝐀𝐓𝐈 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈 𝐋𝐄𝐎 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐈𝐅𝐔𝐍𝐈𝐊𝐀!!!
09-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐀 𝐍𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐇𝐀𝐍𝐀𝐍𝐆, 𝐀𝐒𝐈𝐊𝐈𝐋𝐈𝐙𝐀 𝐍𝐀 𝐊𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐀 𝐊𝐄𝐑𝐎 𝐙𝐀𝐎
09-06-2026