MAKALLA AVALIA NJUGA CHANGAMOTO ZA BARABARA, WANYAMAPORI NA UMEME LIWALE
• Awaelekeza mawaziri kutoka katika Wizara husika kufika na kutatua changamoto hizo.
LINDI: KATIBU wa Halmashauri Kuu (NEC), Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), CPA Amos Makalla amesema katika Wilaya ya Liwale mkoani Lindi wananchi wanachangamoto kubwa ya barabara, wanyamapori pamoja na umeme unaosababisha kukwama kwa shughuli za kiuchumi katika wilaya hiyo.
Makalla amesema ili kuweza kutatua changamoto hizo mawaziri wa wizara husika akiwemo Waziri wa Ujenzi na Maliasili na Utalii kufika katika Wilaya hiyo ili kuona namna wanaweza kusaidia utatuzi wa changamoto hizo katika wilaya hiyo.
Makalla ameeleza hayo leo Aprili 11,2025 wakati akizungumza na wananchi wa wilaya ya Liwale mkoani Lindi, ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya siku 10 katika mikoa ya Lindi na Mtwara.
Katika kushirikisha wananchi juu ya utatuzi wa changamoto zao Makalla alipiga simu kwa Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega ili aweze kuzungumza kuhusu utatuzi wa changamoto ya barabara katika wilaya hiyo na kumtaka afike katike katika wilaya hiyo
Akitoa ufafanuzi juu ya changamoto za wananchi wa Wilaya hiyo Makalla alimtaka Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Pindi Chana kufika katika Wilaya hiyo ili aweze kuona namna wanaweza kutatua changamoto hiyo ya Tembo katika Wikaya ya Liwale kwani wanyama hao ni hatari na wanasababisha vifo kwa wananchi.
“Mheshimiwa Mbunge ameeleza amesema kuhusu TANAPA amesema TAWA nimemwambia walifanya kazi juzi namna walivyofanya kitaalamu kusogeza na kudhibiti Tembo katika maeneo mbalimbali, nimemtaka waziri mwenyewe na timu yake waje hapa Liwale mumpokee mumueleze vizuri,” amesema Makalla.
Akizungumza na wananchi hao kwa njia ya simu Ulega alisema kuwa katika nchi nzima miongoni mwa maeneo ambayo hayajaunywa vizuri katika barabara ni mkoa wa lindi na wilaya ambayo ipo katika changamoto kubwa ni wilaya ya Liwale, hivyo alisema amepokea maelekezo na atafika Liwale.
Aliongeza kuwa katika bajeti atakayoisoma katika wiki mbili zijazo aliwahakikishia kuwa barabara hiyo itakuwa ni moja wapo kuanzia Nangurukuru mpaka Liwale yenye umbali wa kilometa 231 na kutoka Liwale hadi Nachingwea ambayo itakuwa na kilometa 50 za kuwekwa lami kutokana na maagizo ya Rais Samia Suluhu Hassan.
“Hii barabara inayokwenda Nachingwea inawaunganisha majirani zao wa Nachingwea mpaka Masasi lakini tutawapa kipaumbele watu wa Liwale kwa sababu upande wao ndo kwenye uzalishaji mkubwa wa Korosho zinazotakikana kufika sokoni,” amesema Ulega
Ameongeza kuwa hayo ni mapenzi ya Rais Samia ya kuinua wilaya zilizopo pembezoni ambazo zinafanya uzalishaji mkubwa wa kiuchumi ikiwemo wilaya hiyo inayozalisha Korosho na ufuta kwa wingi ili yaweze kuinuka kiuchumi.
Katika hatua nyingine Makalla amesema amezungumza na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk Dotto Biteko ili aweze kuonana namna ya umeme uvutwe kutoka Dar es salaam kupitia Rifiji hadi Somanga ili uweze kuwasaidia na shughuli za uzalishaji katika migodi badala ya kusubiri wa kutoka Ruvuma kupitia Mtwara kutoka katika gridi ya taifa.
Makalla alisema kufanya hivyo itasaidia kuongeza uzalishaji na kuvutia uwekezaji katika shughuli za kiuchumi zinazohitaji umeme katika wilaya hiyo na mkoa wa Lindi kwa ujumla.
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
07-11-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
07-11-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
07-11-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
07-11-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
07-11-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
07-11-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
07-11-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
07-11-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
07-11-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
07-11-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
07-11-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
07-11-2025
TAARIFA KWA UMMA
07-11-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
07-11-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
07-11-2025
MONGELLA AONGOZA MAZISHI YA KADA WA CCM JIJINI MWANZA
07-11-2025
ASIYETII SHERIA, KATIBA NA KUWA TAYARI KUUA KWA MASLAHI BINAFSI HUO NI UGAIDI’
07-11-2025
πππ π¬ππ¦ππ¦ππ§πππ πͺπππ’π πππ ππ¨πππππππͺπ ππͺπ ππ¨πππ‘πππ§ππ π¨πͺπππ’, π¨πππππ‘ππ’ π‘π π¨πππππππ¨, π¬ππππ ππ π πππ¨π‘ππ - πππ. πππ©π¨
07-11-2025
KAENI KIMYA KAMA HAMJUI NCHI ILIKOTOKA - WASIRA
07-11-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amefungua kiwanda cha kutengeneza mabomba ya maji na uchakataji pamba cha MOLI Oil Mills Co. Ltd kilichopo Bariadi Mkoani Simiyu tarehe 16 Juni, 2025.
07-11-2025