ALICHOSEMA KATIBU MKUU WA CCM SAKATA LA CHADEMA KUSHIKILIWA POLISI
“Nimesikia kule Mbeya kulikuwa na tafrani kidogo kati ya Chadema na Polisi, na sisi kwa staili ya Rais wetu Samia Suluhu Hassan, anapenda sana mambo yawe yanamalizwa kwa kuzungumzwa, badala ya kukimbizana kimbizana kila mahali.
“Kwa hiyo nilifanya jitihada za kuwatafuta viongozi wenzangu wa vyama vingine ili nizungumze nao makatibu wenzangu, lakini nikaambiwa yule mmoja wa Chadema ni katika waliokamatwa.
“Sasa nikasema kwa kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani uko hapa, mambo ya sheria, siyo ya kutolea maelekezo Kiongozi wa Chama cha siasa, au siyo? Lakini nitumie nafasi hii, mwambie Waziri wako, kwamba tunaomba, muone uwezekano wale viongozi wa vyama vya siasa waachiliwe.
“Ili mtupate nafasi ya kuzungumza nao. Waachiliwe tupate nafasi ya kuzungumza nao, kwa sababu tunajenga taifa moja. Tunapenda kuwa na taifa tulivu.
“Kama kuna mahali wamekosea wao au tumekosea sisi, tukae tuzungumze. Tuijenge nchi yetu. Kwa hiyo huu ni ujumbe, mwambie Waziri wako kwamba Chama Cha Mapinduzi kinaamini kwamba kuzungumza ni jambo zuri zaidi.
“Kabla vyombo vya sheria havijafanya mambo ya sheria basi mtupe nafasi kidogo sisi wanasiasa kwanza tuzumgumze," Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, Katibu Mkuu wa CCM.
Balozi Nchimbi amezungumza hayo leo Agosti 12, 2024, kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Uwanja wa CCM Katoro, mkoani Geita akiwa kwenye mwendelezo wa ziara yake ya siku 3, mkoani humo, aliyoanza Agosti 11, 2024.
Katibu Mkuu wa CCM huyo, katika ziara yake hiyo aliyoanzia Mkoa wa Kigoma, kisha Kagera na sasa yuko mkoani Geita, ameambatana na Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Ndugu Issa Haji Usi Gavu, Katibu wa NEC - Oganaizesheni, Ndugu Amos Gabriel Makalla, Katibu wa NEC - Itikadi, Uenezi na Mafunzo na Ndugu Rabia Hamid Abdalla, Katibu wa NEC - Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, ambapo kesho anatarajiwa kuzungumza na wananchi Mjini Geita, kwenye mkutano mkubwa wa hadhara utakaofanyika katika Uwanja wa Nyankumbu.
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
09-12-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
09-12-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
09-12-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
09-12-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
09-12-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
09-12-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
09-12-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
09-12-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
09-12-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
09-12-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
09-12-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
09-12-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
09-12-2025
TAARIFA KWA UMMA
09-12-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
09-12-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
09-12-2025