Makao Makuu - Dodoma
#CCM Imetimia KaziIendelee

Habari na Matukio Mbalimbali


BALOZI NCHIMBI AONYA VIONGOZI KUTOA KAULI ZA KIBAGUZI
 

alternative

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi amewataka viongozi na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuepuka kutoa kauli au kufanya vitendo vyenye taswira inayoweza kutafsiriwa kuwa baadhi yao wanashabikia ukandamizaji wa haki za wananchi.

Katibu Mkuu Balozi Dkt. Nchimbi amesisitiza kuwa maneno na vitendo vya wana-CCM wakati wote lazima yaakisi dhamana ambayo chama kimepewa na wananchi ya kuwatumikia, ikiwemo kusimamia haki, bila ubaguzi wala dhuluma ya aina yoyote .

Balozi Nchimbi amesema hayo akiwa Chuo cha Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Ihemi, mkoani Iringa, alipokuwa akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo watendaji na viongozi wa jumuiya hiyo wa ngazi za mikoa na wilaya zote, nchi nzima, leo Alhamis, 11 Julai 2024. 

Awali akimkaribisha Balozi Nchimbi, Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Komredi Mohammed Ali Mohammed (Kawaida), amekishukuru Chama chini ya Mwenyekiti wa CCM, Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa jinsi kinavyoendelea kuwalea na kuwaamini vijana kukitumikia Chama na jumuiya zake na nchi kwa ujumla.

Nae Katibu Mkuu wa UVCCM, Komredi Joketi Urban Mwegelo akitoa taarifa kuhusu maandalizi ya mafunzo hayo, amesema yatawasaidia viongozi na watendaji wa jumuiya hiyo kwenye mikoa, wilaya na hatimae kushuka ngazi zingine nchi nzima kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi unaohitajika.

alternative alternative alternative alternative alternative alternative alternative
Habari Nyingine

Nukuu za Viongozi