Serikali ya Awamu ya Nane (8) itaendelea kuboresha miundombimnu ya upatikanaji wa huduma mbali mbali ikiwemo huduma za Afya nchini ikiwa ni azma ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya mwaka 1964 ya kutoa huduma bora za Afya kwa kila mwananchi bila ya malipo na ubaguzi wa aina yoyote.
Akifungua Hospitali ya Wilaya ya Kati iliyopo Mwera Pongwe , Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe Hemed Suleiman Abdulla amesema kupitia ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2020-2025, Dira ya Maendeleo ya Zanzibar ya mwaka 2050, Sera na Mikakati mbali mbali Serikali imeweza kujenga hospitali kumi (10) za Wilaya kwa Unguja na Pemba ambazo zina vifaa tiba pamoja na magari ya kubebea wagonjwa pindi dharura itakapotokea.
Mhe. Hemed amesema miradi hii ya maendeleao inayofanywa na Serikali inaakisi malengo ya Mapinduzi ambayo ndio fikra na mawazo ya waasisi wa Mapinduzi matukufu ya mwaka 1964 hivyo Serikali itaendelea kuimarisha huduma bora kwa jamii kwa kuhakikisha upatikanaji wa dawa, vifaa tiba, TEHAMA,wafamasia, wauguzi pamoja na madaktari wakutosha katika hospitali na vituo vya Afya nchini.
Aidha Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar ameuagiza Uongozi wa Wizara ya Afya kuhakikisha wanaisimamia vyema hosptiali hio na hospitali nyengine ili kuweza kufikia malengo yaliyokusudiwa na Serikali kwa kuwapatia wananchi huduma bora bila ya ubaguzi wa aina yoyote.
Amesema Wiza ya Afya ina wajibu wa kuhakikisha hospitali hizi zinatunzwa na kufanyiwa ukarabati wa majengo na vitendea kazi mara kwa mara ili kuviwezesha kuwa endelevu katika utoaji wa huduma na kuwataka wafanyakazi waliopangiwa katika hospital ya Mwera Pongwe
Mhe. Hemed amezitaka kampuni ya Lancet na Saifee amabazo zimepewa mkataba wa kutoa huduma hospitalini hapo kuhakikisha huduma zote zinapatikana kwa wakati na kwa ubora wa hali ya juu kama makubaliano yanavyoelekeza.
Sambamba na hayo amewataka wahudumu na madaktari kuendelea kutumia lugha nzuri na kufuata maadili yao ya kazi wakati wanapowahudumia wagonjwa wanaofika kupatiwa huduma hospitalini hapo pamoja na kuwataka wananchi kutoa ushirikiano kwa madaktari na wahudumu sambamba na kuilinda miundombinu iliyomo hospitalini ili iweze kudumu na kutumika kwa muda mrefu.
Nae Waziri wa Afya Mhe Nassor Ahmed Mazurui amesema hudu za Afya zimeimarika zaidi Zanzibar ndani ya miaka mitatu (3) ya Uongozi wa Rais Dk Mwinyi kwa kujengwa mahospitali ya Wilaya, Mkoa na zile za Rufaa pamoja na kufanyiwa maboresho makubwa baadhi ya vituo vya Afya.
Amesema kuwa hospitali na vituo vya Afya vilivyojengwa vimekidhi viwango na ubora, pamoja na kuwepo vifaa tiba vya kutosha kulingana na uhitaji sambamba na utolewaji wa huduma za matibabu kwa wananchi wote bila ya ubaguzi na kufikia zile fikra na mawazo ya waasisi wa mapinduzi akiwemo rais wa kwanza wa Zanzibar Marehemu Sheikh ABEID AMANI KARUME.
Akitoa Taarifa ya Kitaalamu kuhusu ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Kati ya Mwera Ponge Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Amour Suleiman amesema Jumla ya shilingi Bilioni 9.7 zimetumika katika Ujenzi wa Mradi wa Hospital hiyo ambapo kwa wakati mmoja ina uwezo wa kulaza zaidi ya wagonjwa mia moja(100) na kupatiwa matibabu hospitalini hapo.
Amesema kuwa hospitali hiyo ya Wilaya inatoa huduma mbali mbali ikiwemo Huduma ya mama na mtoto, huduma ya maabara, huduma ya magojwa ya dharura hivyo amewataka wananchi kuendelea kuitumia vizuri hospitali hiyo kwa kutoa ushirikiano kwa madaktari na watoa huduma hospitalini hapo ili kuweza kufikia malengo ya mapinduzi matukufu ya mwaka 1964 ya kutoa huduma bora kwa kila mwnanchi.
𝐂𝐂𝐌 𝐘𝐀𝐓𝐇𝐈𝐁𝐈𝐓𝐈𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐒𝐈𝐍𝐆𝐈 𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐇𝐔𝐃𝐔𝐌𝐈𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐕𝐘𝐀𝐌𝐀 𝐓𝐀𝐖𝐀𝐋𝐀 𝐀𝐅𝐑𝐈𝐊𝐀
22-07-2026
𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐍𝐀𝐈𝐅𝐔𝐍𝐆𝐔𝐀 𝐄𝐍𝐙𝐈 𝐌𝐏𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐆𝐎𝐌𝐀!
22-07-2026
🚆 𝐓𝐔𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐄 𝐊𝐈𝐆𝐎𝐌𝐀!
22-07-2026
ZIARA YA RAIS WA MISRI-TANZANIA
22-07-2026
🔰 CCM NA ACT-WAZALENDO WASAINI MARIDHIANO YA PAMOJA YA KISIASA ZANZIBAR
22-07-2026
🎉 𝐇𝐄𝐑𝐈 𝐘𝐀 𝐒𝐈𝐊𝐔 𝐘𝐀 𝐊𝐔𝐙𝐀𝐋𝐈𝐖𝐀, 𝐃𝐊𝐓. 𝐀𝐒𝐇𝐀-𝐑𝐎𝐒𝐄 𝐌𝐈𝐆𝐈𝐑𝐎! 🔰
22-07-2026
🔰𝐍𝐀𝐈𝐁𝐔 𝐊𝐀𝐓𝐈𝐁𝐔 𝐌𝐊𝐔𝐔 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐁𝐀𝐑𝐀 𝐀𝐒𝐇𝐈𝐑𝐈𝐊𝐈 𝐊𝐈𝐊𝐀𝐎 𝐂𝐇𝐀 𝐇𝐀𝐋𝐌𝐀𝐒𝐇𝐀𝐔𝐑𝐈 𝐊𝐔𝐔 𝐘𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐌𝐖𝐀𝐍𝐙𝐀
22-07-2026
🔰𝐇𝐄𝐑𝐈 𝐘𝐀 𝐌𝐀𝐀𝐃𝐇𝐈𝐌𝐈𝐒𝐇𝐎 𝐘𝐀 𝐒𝐀𝐁𝐀 𝐒𝐀𝐁𝐀 𝟐𝟎𝟐𝟔!
22-07-2026
𝐒𝐀𝐒𝐀 𝐍𝐈 𝐙𝐀𝐌𝐔 𝐘𝐀 𝐏𝐖𝐀𝐍𝐈; 𝐀𝐑𝐃𝐇𝐈 𝐘𝐀 𝐇𝐈𝐒𝐓𝐎𝐑𝐈𝐀, 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐀𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀!!!!!
22-07-2026
𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈 𝐘𝐀𝐌𝐏𝐀 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐌𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐇𝐈𝐒𝐓𝐎𝐑𝐈𝐀
22-07-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐙𝐈𝐍𝐃𝐔𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐋𝐀 𝐖𝐀𝐊𝐄𝐑𝐄𝐊𝐄𝐓𝐖𝐀 𝐌𝐋𝐀𝐍𝐃𝐄𝐆𝐄, 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐒𝐀-𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀
22-07-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐍𝐀. 𝟏𝟎 𝐌𝐀𝐅𝐈𝐅𝐈, 𝐀𝐒𝐈𝐒𝐈𝐓𝐈𝐙𝐀 𝐀𝐌𝐀𝐍𝐈, 𝐔𝐌𝐎𝐉𝐀 𝐍𝐀 𝐌𝐒𝐇𝐈𝐊𝐀𝐌𝐀𝐍𝐎
22-07-2026
𝐌𝐑𝐀𝐃𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐎 𝐘𝐀 𝐔𝐅𝐔𝐍𝐃𝐈 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎 𝐊𝐔𝐅𝐔𝐍𝐆𝐔𝐀 𝐅𝐔𝐑𝐒𝐀 𝐙𝐀 𝐀𝐉𝐈𝐑𝐀 𝐊𝐖𝐀 𝐕𝐈𝐉𝐀𝐍𝐀
22-07-2026
𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎, 𝐙𝐀𝐌𝐔 𝐘𝐄𝐍𝐔 𝐍𝐈 𝐋𝐄𝐎!
22-07-2026
𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀: 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐒𝐔𝐋𝐔𝐇𝐔 𝐇𝐀𝐒𝐒𝐀𝐍 𝐍𝐈 𝐌𝐓𝐄𝐊𝐄𝐋𝐄𝐙𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐀𝐇𝐈𝐑𝐈 𝐖𝐀 𝐀𝐇𝐀𝐃𝐈 𝐙𝐀 𝐂𝐂𝐌
22-07-2026
𝐒𝐈𝐌𝐔 𝐈𝐌𝐄𝐈𝐓𝐀, 𝐍𝐄𝐄𝐌𝐀 𝐘𝐀 𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐙𝐈 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎!
22-07-2026
𝐑𝐔𝐀𝐇𝐀 𝐌𝐁𝐔𝐘𝐔𝐍𝐈 𝐘𝐀𝐅𝐔𝐑𝐈𝐊𝐀; “𝐂𝐇𝐈𝐄𝐅 𝐂𝐇𝐎𝐆𝐀𝐕𝐀𝐓𝐀𝐌𝐁𝐔𝐋𝐄” 𝐀𝐊𝐈𝐓𝐄𝐊𝐀 𝐌𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐎 𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐀!
22-07-2026
𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐎 𝐂𝐇𝐀 𝐔𝐌𝐖𝐀𝐆𝐈𝐋𝐈𝐀𝐉𝐈 𝐍𝐈 𝐔𝐅𝐔𝐍𝐆𝐔𝐎 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐏𝐈𝐍𝐃𝐔𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐔𝐂𝐇𝐔𝐌𝐈 𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈: 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈
22-07-2026
𝐂𝐂𝐌 𝐘𝐀𝐔𝐍𝐆𝐀 𝐌𝐊𝐎𝐍𝐎 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐖𝐀 𝐍𝐉𝐎𝐌𝐁𝐄 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐙𝐀 𝐔𝐙𝐀𝐋𝐈𝐒𝐇𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐀𝐋𝐈
22-07-2026
𝐀𝐌𝐀𝐍𝐈 𝐍𝐈 𝐌𝐒𝐈𝐍𝐆𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐎: 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈
22-07-2026