KATIBU MKUU CCM AWEKA WAZI NEEMA KUMALIZA ADHA YA USAFIRI ZIWA TANGANYIKA, MBOLEA NA MALIPO YA WAKULIMA WA MAHINDI RUKWA
KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Komredi Daniel Godfrey Chongolo ameeleza hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Serikali, kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2020 – 2025, kwa vitendo, kuboresha huduma za uchukuzi, usafiri na usafirishaji katika Ziwa Tanganyika, ambapo kufikia mwezi Disemba, 2023, wananchi wataanza kupata nafuu, kuelekea kumalizika kwa adha kubwa iliyopo sasa.
Unafuu huo utatokana na kukamilika kwa matengenezo ya moja ya meli, kati ya mbili zilizopo sasa, Mv Mwongozo na Mv Liemba, ambazo zote zinafanyiwa matengenezo, ikiwa ni mojawapo ya mikakati ya muda mfupi, wa kati na mrefu, pamoja na kutengeneza meli mpya, kwa ajili ya shughuli za kiuchumi na wananchi kwa ujumla, ambazo hatimae zitaondoa na kumaliza kabisa changamoto ya usafiri na usafirishaji katika maeneo ya mwambao wa Ziwa Tanganyika, kuunganisha hadi nchi jirani za DR Congo na Zambia.
Katibu Mkuu wa CCM, Komredi Chongolo ametangaza mikakati hiyo alipokuwa akizungumza na wananchi wa maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Kalambo, Jumatatu Oktoba 9, 2023, ambapo anaendelea na ziara yake katika Mkoa wa Rukwa, yenye malengo ya kuhamasisha uhai wa CCM, kusikiliza changamoto za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi na kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM ya 2020 – 2025, kwa kutembelea miradi ya maendeleo.
“Wote ni mashahidi hizi meli (Mv Liemb ana Mv Mwongozo) zimetengenezwa miaka mingi, ingawa Mwongozo sio ya miaka mingi sana kama Liemba. Juzi nikiwa Katavi nimezungumza na Waziri wa Uchukuzi, tumekubaliana mambo kadhaa ikiwa ni maelekezo ya Ilani ya Uchaguzi ya CCM na maelekezo ya Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan.”
“Kuhakikisha wanachukua hatua za haraka ili MV Mwongozo au MV Liemba mojawapo ianze kazi wakati nyingine inaendelea kufanyiwa marekebisho. Makubaliano tuliyokubaliana tayari wameanza kuyatekekeleza. Sasa hivi tunavyoongea meli ya Mwongozo imewekwa kwenye chelezo pale Kigoma mjini,” amesema Chongolo.
Ndugu Chongolo amesema kuwa kwa sasa meli hiyo inakaguliwa kwa ajili ya kuona matengenezo yanayotakiwa kufanyika ikifika Desemba mwaka huu iwe tayari kurudishwa kwenye maji Ziwa Tanganyika ili ianze kufanya safari, huku akiongeza kuwa kwa upande wa MV Liemba ambayo yenyewe inahitaji matengenezo makubwa zaidi kutokana na ukongwe wake, tayari wizara yenye dhamana imetangaza mkandarasi wa kuifanyia marekebisho.
“Kwa sababu meli hii imeshafanya kazi zaidi ya miaka 100, hivyo itafanyiwa marekebisho makubwa na Serikali imeshatenga fedha kwa ajili ya kufanya kazi hiyo na uhakika wa kufanya hivyo ni asilimia 100,” amesema Chongolo.
Aidha amesema Serikali imejenga bandari za mwambao wa Ziwa Tanganyika, ambapo kuna Bandari ya Kabwe, Bandari ya Kasanga zilizoko mkoani Rukwa, Bandari ya Karema ambayo iko Katavi, pamoja na Bandari ya Kigoma, huku akibainisha kuwa hata bandari zingine ndogo ndogo zinawekewa mipango ili zifanye kazi ya kurahisisha shughuli za usafiri, usafirishaji na uchukuzi ili wananchi wajitafutie maendeleo yatakayoboresha maisha yao na kuwawezesha wananchi kujitengenezea uchumi wao.
“Ili zifanye kazi Serikali imefanya uamuzi tayari. Wiki hii tuliyonayo, pale Kigoma watasaini mkataba na mkandarasi atayejenga karakana ya meli Kigoma na kwa maana hiyo kabla ya mwaka huu kuisha mkandarasi atakuwa ameshakusanya vifaa vyake kwa ajili ya kujenga karakana na hiyo karakana itakuwa ya kudumu.
“Lengo ni kwamba karakana hiyo ikikamilika itajengwa meli ya mizigo zaidi ya tani 3500 ambayo itakuwa na uwezo wa kubeba magari marefu (malori) 100 kwa wakati mmoja. Maana yake muda si mrefu watu watakuwa na njia mbadala na kuepuka kwa msongamano wa njia ya Tunduma kwenda DRC (Congo) kwa kulazimika kupitia Zambia.
Amesema kuwa wasafiri na wote wanaohusika na shughuli za usafirishaji na uchukuzi wataweza kutumia njia ya Kasanga, watavuka kwa meli kwenda upande wa pili, ambako pia meli zitakuwa zinasafirisha watu na mizigo kuja upande mwingine, akiweka wazi kuwa maneno hayo yatawekwa katika vitendo vinavyoendelea kutafsiri dhamira ya dhati ya CCM kuendelea kuongoza nchi na kuwatumikia wananchi, kwa kuisimamia Serikali ili iweze kutengeneza mazingira na fursa za wananchi kujikwamua kimaisha na kubadili hali zao, kupitia shughuli za kiuchumi.
Kuhusu upatikanaji wa mbolea kwa msimu ujao wa kilimo na malipo ya fedha za mahindi waliyouza msimu huu, Katibu Mkuu Chongolo, akizungumza katika maeneo hayo, ikiwemo Singiwe, Kasanga, Kisumba, Chisenga na Matai, amesema kuwa wanakwenda kuielekeza Serikali, kupitia Wizara ya Kilimo, kuhakikisha inaondoa hofu ya wananchi, kwa kuhakikisha mbolea inauzwa kwa bei elekezi kama ambavyo Serkali imeelekeza na ipatikane kwa wingi na ihakikishe wakulima wanalipwa malipo yao haraka.
Kuhusu ujenzi wa Barabara ya Matai – Kasesya yenye kilometa 50, Ndugu Chongolo amesema kuwa mradi huo wa kimkakati utakuwa mkombozi mwingine katika kufanya biashara na kuyafikia masoko ya nchi jirani ambapo ikikamilika magari, yakiwemo malori yanayokwenda nchi jirani yataweza kuchagua ama kupitia Tunduma au Rukwa, Kalambo.
Naye Mbunge wa Jimbo hilo, Josephat Kandege mbali ya kumuomba Katibu Mkuu Chongolo awafikishie salaam za shukrani kwa Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa jinsi ambavyo Serikali anayoiongoza inavyoshirikiana na wakazi wa jimbo hilo kutengeneza mazingira mazuri ya wananchi kupata huduma na kujitafutia maendeleo kutokana na miradi mingi ya maendeleo inayotekelezwa jimboni humo, pia alizungumzia uwepo wa Skimu ya Umwagiliaji ya Singiwe, ambao umetengewa fedha za kuuboresha ili uongeze manufaa kwa wananchi wa kata hiyo na maeneo mengine, katika kilimo.
Amesisitiza mradi huo ni mkubwa lakini unahitaji maboresho kidogo ili uweze kufanya kazi vizuri huku akitumia nafasi hiyo kueleza kuna kila sababu ya Wilaya ya Kalambo kufufua zao la Kahawa ambalo miaka ya zamani lililimwa kwa wingi na kahawa yake ilikuwa bora.
Katika ziara yake wilayani Kalambo Ndugu Chongolo alishiriki Mkutano wa Shina Namba 6, Singiwe, kutembelea na kukagua ujenzi wa hospitali ya wilaya, kutembelea na kukagua Bandari ya Kasanga, kukagua ujenzi wa Barabara ya Matai – Kasesya na kuzungumza na wananchi katika maeneo yote hayo, ikiwemo na Kisumba.
𝐂𝐂𝐌 𝐘𝐀𝐓𝐇𝐈𝐁𝐈𝐓𝐈𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐒𝐈𝐍𝐆𝐈 𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐇𝐔𝐃𝐔𝐌𝐈𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐕𝐘𝐀𝐌𝐀 𝐓𝐀𝐖𝐀𝐋𝐀 𝐀𝐅𝐑𝐈𝐊𝐀
22-07-2026
𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐍𝐀𝐈𝐅𝐔𝐍𝐆𝐔𝐀 𝐄𝐍𝐙𝐈 𝐌𝐏𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐆𝐎𝐌𝐀!
22-07-2026
🚆 𝐓𝐔𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐄 𝐊𝐈𝐆𝐎𝐌𝐀!
22-07-2026
ZIARA YA RAIS WA MISRI-TANZANIA
22-07-2026
🔰 CCM NA ACT-WAZALENDO WASAINI MARIDHIANO YA PAMOJA YA KISIASA ZANZIBAR
22-07-2026
🎉 𝐇𝐄𝐑𝐈 𝐘𝐀 𝐒𝐈𝐊𝐔 𝐘𝐀 𝐊𝐔𝐙𝐀𝐋𝐈𝐖𝐀, 𝐃𝐊𝐓. 𝐀𝐒𝐇𝐀-𝐑𝐎𝐒𝐄 𝐌𝐈𝐆𝐈𝐑𝐎! 🔰
22-07-2026
🔰𝐍𝐀𝐈𝐁𝐔 𝐊𝐀𝐓𝐈𝐁𝐔 𝐌𝐊𝐔𝐔 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐁𝐀𝐑𝐀 𝐀𝐒𝐇𝐈𝐑𝐈𝐊𝐈 𝐊𝐈𝐊𝐀𝐎 𝐂𝐇𝐀 𝐇𝐀𝐋𝐌𝐀𝐒𝐇𝐀𝐔𝐑𝐈 𝐊𝐔𝐔 𝐘𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐌𝐖𝐀𝐍𝐙𝐀
22-07-2026
🔰𝐇𝐄𝐑𝐈 𝐘𝐀 𝐌𝐀𝐀𝐃𝐇𝐈𝐌𝐈𝐒𝐇𝐎 𝐘𝐀 𝐒𝐀𝐁𝐀 𝐒𝐀𝐁𝐀 𝟐𝟎𝟐𝟔!
22-07-2026
𝐒𝐀𝐒𝐀 𝐍𝐈 𝐙𝐀𝐌𝐔 𝐘𝐀 𝐏𝐖𝐀𝐍𝐈; 𝐀𝐑𝐃𝐇𝐈 𝐘𝐀 𝐇𝐈𝐒𝐓𝐎𝐑𝐈𝐀, 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐀𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀!!!!!
22-07-2026
𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈 𝐘𝐀𝐌𝐏𝐀 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐌𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐇𝐈𝐒𝐓𝐎𝐑𝐈𝐀
22-07-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐙𝐈𝐍𝐃𝐔𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐋𝐀 𝐖𝐀𝐊𝐄𝐑𝐄𝐊𝐄𝐓𝐖𝐀 𝐌𝐋𝐀𝐍𝐃𝐄𝐆𝐄, 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐒𝐀-𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀
22-07-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐍𝐀. 𝟏𝟎 𝐌𝐀𝐅𝐈𝐅𝐈, 𝐀𝐒𝐈𝐒𝐈𝐓𝐈𝐙𝐀 𝐀𝐌𝐀𝐍𝐈, 𝐔𝐌𝐎𝐉𝐀 𝐍𝐀 𝐌𝐒𝐇𝐈𝐊𝐀𝐌𝐀𝐍𝐎
22-07-2026
𝐌𝐑𝐀𝐃𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐎 𝐘𝐀 𝐔𝐅𝐔𝐍𝐃𝐈 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎 𝐊𝐔𝐅𝐔𝐍𝐆𝐔𝐀 𝐅𝐔𝐑𝐒𝐀 𝐙𝐀 𝐀𝐉𝐈𝐑𝐀 𝐊𝐖𝐀 𝐕𝐈𝐉𝐀𝐍𝐀
22-07-2026
𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎, 𝐙𝐀𝐌𝐔 𝐘𝐄𝐍𝐔 𝐍𝐈 𝐋𝐄𝐎!
22-07-2026
𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀: 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐒𝐔𝐋𝐔𝐇𝐔 𝐇𝐀𝐒𝐒𝐀𝐍 𝐍𝐈 𝐌𝐓𝐄𝐊𝐄𝐋𝐄𝐙𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐀𝐇𝐈𝐑𝐈 𝐖𝐀 𝐀𝐇𝐀𝐃𝐈 𝐙𝐀 𝐂𝐂𝐌
22-07-2026
𝐒𝐈𝐌𝐔 𝐈𝐌𝐄𝐈𝐓𝐀, 𝐍𝐄𝐄𝐌𝐀 𝐘𝐀 𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐙𝐈 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎!
22-07-2026
𝐑𝐔𝐀𝐇𝐀 𝐌𝐁𝐔𝐘𝐔𝐍𝐈 𝐘𝐀𝐅𝐔𝐑𝐈𝐊𝐀; “𝐂𝐇𝐈𝐄𝐅 𝐂𝐇𝐎𝐆𝐀𝐕𝐀𝐓𝐀𝐌𝐁𝐔𝐋𝐄” 𝐀𝐊𝐈𝐓𝐄𝐊𝐀 𝐌𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐎 𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐀!
22-07-2026
𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐎 𝐂𝐇𝐀 𝐔𝐌𝐖𝐀𝐆𝐈𝐋𝐈𝐀𝐉𝐈 𝐍𝐈 𝐔𝐅𝐔𝐍𝐆𝐔𝐎 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐏𝐈𝐍𝐃𝐔𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐔𝐂𝐇𝐔𝐌𝐈 𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈: 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈
22-07-2026
𝐂𝐂𝐌 𝐘𝐀𝐔𝐍𝐆𝐀 𝐌𝐊𝐎𝐍𝐎 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐖𝐀 𝐍𝐉𝐎𝐌𝐁𝐄 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐙𝐀 𝐔𝐙𝐀𝐋𝐈𝐒𝐇𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐀𝐋𝐈
22-07-2026
𝐀𝐌𝐀𝐍𝐈 𝐍𝐈 𝐌𝐒𝐈𝐍𝐆𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐎: 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈
22-07-2026