STAKABADHI GHALANI INA FAIDA KWA MKULIMA- MAKALLA
•Elimu iendelee kutolewa
DUMILA-KILOSA: Katibu wa Halmashauri Kuu (NEC), Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama cha Mapinduzi (CCM), CPA Amos Makalla amesema elimu itolewe juu ya matumizi ya mfumo wa kuangalia bei za mazao ili wakulima wawe wanajua bei za mazao wasiweze kudhulumiwa.
Pia Makalla amesema mtu anayepinga suala la stakabadhi ghalani anatakiwa kuelemishwa kwa sababu huo ni mfumo ambayo upo kwa ajili ya kuwasaidia wakulima.
Makalla ameeleza hayo leo Mei 16,2025 aliposimama kusalimia wananchi katika Kata ya Dumila Wilaya ya Kilosa wakati akielekea katika Wilaya ya Gairo kwa ajili ya mkutano wa mwisho kukamilisha ziara yake katika Mkoa wa Morogoro.
Awali, Makalla alitoa nafasi kwa ajili ya wananchi wa eneo hilo kuzungumza changamoto zinazowakabili ili kufanyiwa ufumbuzi.
Moja ya wananchi ambaye ni Mkulima, Said Khatibu Mohamed alisema changamoto yake kubwa na kwa wananchi wengine ni kuhusu suala la stakabadhi ghalani katika mazao ya ufuta na mbaazi kwamba wanapeleka mazao bila kuwekwa wazi bei ya mazao hayo.
Akijibu hoja hiyo Makalla amesema ikitokea mtu anapinga kuhusu suala la stakabadhi ghalani anahitaji kuelimishwa, kwa sababu stakabadhi ghalani ni ushindani badala ya watu kutumia madalali na kupiga debe na kudhulumiwa wanatumia stakabadhi ghalani kushindani kwa bei.
“Nataka niwaambie mtu anayepinga stabadhi ghalani akajitokeza hadharani labda aseme pesa zinachelewa tunaweza kusema ni changamoto lakini anayepinga suala la stakabadhi ghalani anahitaji kuelemishwa,” amesema Makalla.
Ameongeza ikitikea wakulima wamepeleka mazao yameuzwa na wakachelewa kupata frdha zao ndipo wanapoingia Mkuu wa Mkoa na Wilaya kuhakikisha wananchi wanalipwa stahiki zao haraka inavyowezekana.
Aidha ameongeza yeye akiwa kama Mwenezi ameahidi kuzibebe na kuwa balozi wa kuwasemea wananchi wa Dumila katika changamoto zinazowakabili ikiweko ukamilishaji wa ujenzi wa barabara, mradi wa maji na changamoto nyingine zinazowakabili wananchi wa kata hiyo na Wilaya ya Kilosa kwa ujumla.
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
09-12-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
09-12-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
09-12-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
09-12-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
09-12-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
09-12-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
09-12-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
09-12-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
09-12-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
09-12-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
09-12-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
09-12-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
09-12-2025
TAARIFA KWA UMMA
09-12-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
09-12-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
09-12-2025