Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla ameutaka Mfuko wa Fidia kwa wafanyakazi (WCF) na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) kuendeleza ushirikiano katika kazi utakaoleta manufaa makubwa katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku
Akifungua kikao kazi kati ya Mahakama ya Tanzania, Mfuko wa hifadhi ya Jamii Zanzibar na Mfuko wa Fidia kwa wafanyakazi kilichofanyika katika Ukumbi wa Hotel ya Zanzibar Beach Resort, Mhe. Hemed amesema Taasisi hizo zinapaswa kuwa na maazimio ya pamoja katika kuzifanya maboresho mbali mbali sheria zote zinazohusiana na malipo ya fidia kwa wafanyakazi na taratibu zote zinazotumika katika kutoa huduma hio.
Mhe. Hemed amesema waajiri wote Tanzania Bara na Zanzibar wanapaswa kubeba dhamana kwa wafanyakazi wao pindi wanapopata majanga yatokanayo na kazi kwa kuchukua hatua za haraka ikiwemo kutoa taarikwa kwa WCF na ZSSF ndani ya muda uliowekwa kisheria ili wafanyakazi au wategemezi wao waweze kupata mafao stahiki kwa wakati.
Aidha Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesema uwepo wa Majaji wa Mahkama Kuu kwa pande zote mbili za Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania katika kikao kazi hicho kinatoa fursa kwao kujifunza namna ya kufanya kazi na WCF pamoja na ZSSF hasa katika kuboresha huduma za kimahakama kwa kutambua hatua mbali mbali katika uchakataji wa madai ya wafanyakazi waliopata madhila yatokanayo na kazi wanzozifanya.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amewahakikishia washiriki wa kikao kazi hicho kuwa Serikali zote mbili zitaendelea kutoa ushirikiano utakaohitajika katika kuboresha mahusiano yenye lengo la kuleta ustawi wa wafanyakazi pindi wanapokuwa kazini.
Kwa upande wake Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Vijana na watu wenye ulemavu MERY MAGANGA amesema vikao kazi kama hivi vinaumuhimu mkubwa sana katika kudumisha Muungano wa Tanzania pamoja na kuimarisha utendaji kazi kwa wafaanyakazi jambo ambalo huleta tija kubwa kwa Taifa.
MAGANGA amesema kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu itaendelea kufanya kazi kwa ushirikiano kati ya pande zote mbili za Muungano kwa kuhakikisha sheria ya fao la Fidia linatekelezwa kwa haki na usawa kwa wafanyakazi wote sambamba na kuwataka washiriki wote wa kikao hicho kwenda kuyafanyia kazi kwa vitendo yale ambayo watakubaliana katika mkutano huo.
Nae Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu Tanzania Mhe. MUSTAPHER SIYANI amesema lengo kuu la kikao kazi hicho kufanyika Zanzibar ni kudumisha Muungno na kuweka mazingira bora na rafiki yenye kuvutia wawekezaji hasa pakiwa na mfumo Imara wa utowaji na upatikaniji wa haki nchini.
SIYANI amesema kikao hiki kitawakumbusha Majaji, watendaji wa mahakama na wadau wa haki juu ya utekelezaji wa nguzo ya pili ya upatikanaji wa haki na kuwasaidia katika kutafuta utatuzi wa migogoro ya kazi katika Taasisi mbali mbali zilizopo nchini.
Mapema Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) Dkt. JOHN MDUMA amesema Utiaji wa saini wa makubaliano ya kufanya kazi kwa pamoja kati ya WCF na ZSSF unathibitisha mahusiano imara waliyonayo kwa muda mrefu yanayodhihirisha utayari wa kuwasaidi wafanyakazi hasa pale wanapopata majanga wakiwa kazini.
Dkt. MDUMA amesema WCF wameona ipo haja na umuhimu wa kuwajengea uwezo Wazanzibari katika kuzifahamu vyema huduma za mafao ya fidia kazini ili kuweza kutoa haki kwa mfanyakazi ama wategemezi wao pindi mfanyakazi atakapopata ajali akiwa kazini.
Katika kikao hicho Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar ameshuhudia utiaji wa saini kati ya WCF na ZSSF ya makubaliano ya kufanya kazi kwa ushirikiano jambo ambalo litaleta tija na mafanikio makubwa kwa wafanya kazi wa pande zote mbili za jamuhuri ya muungano wa Tanzania
𝐒𝐀𝐒𝐀 𝐍𝐈 𝐙𝐀𝐌𝐔 𝐘𝐀 𝐏𝐖𝐀𝐍𝐈; 𝐀𝐑𝐃𝐇𝐈 𝐘𝐀 𝐇𝐈𝐒𝐓𝐎𝐑𝐈𝐀, 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐀𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀!!!!!
27-06-2026
𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈 𝐘𝐀𝐌𝐏𝐀 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐌𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐇𝐈𝐒𝐓𝐎𝐑𝐈𝐀
27-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐙𝐈𝐍𝐃𝐔𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐋𝐀 𝐖𝐀𝐊𝐄𝐑𝐄𝐊𝐄𝐓𝐖𝐀 𝐌𝐋𝐀𝐍𝐃𝐄𝐆𝐄, 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐒𝐀-𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀
27-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐍𝐀. 𝟏𝟎 𝐌𝐀𝐅𝐈𝐅𝐈, 𝐀𝐒𝐈𝐒𝐈𝐓𝐈𝐙𝐀 𝐀𝐌𝐀𝐍𝐈, 𝐔𝐌𝐎𝐉𝐀 𝐍𝐀 𝐌𝐒𝐇𝐈𝐊𝐀𝐌𝐀𝐍𝐎
27-06-2026
𝐌𝐑𝐀𝐃𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐎 𝐘𝐀 𝐔𝐅𝐔𝐍𝐃𝐈 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎 𝐊𝐔𝐅𝐔𝐍𝐆𝐔𝐀 𝐅𝐔𝐑𝐒𝐀 𝐙𝐀 𝐀𝐉𝐈𝐑𝐀 𝐊𝐖𝐀 𝐕𝐈𝐉𝐀𝐍𝐀
27-06-2026
𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎, 𝐙𝐀𝐌𝐔 𝐘𝐄𝐍𝐔 𝐍𝐈 𝐋𝐄𝐎!
27-06-2026
𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀: 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐒𝐔𝐋𝐔𝐇𝐔 𝐇𝐀𝐒𝐒𝐀𝐍 𝐍𝐈 𝐌𝐓𝐄𝐊𝐄𝐋𝐄𝐙𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐀𝐇𝐈𝐑𝐈 𝐖𝐀 𝐀𝐇𝐀𝐃𝐈 𝐙𝐀 𝐂𝐂𝐌
27-06-2026
𝐒𝐈𝐌𝐔 𝐈𝐌𝐄𝐈𝐓𝐀, 𝐍𝐄𝐄𝐌𝐀 𝐘𝐀 𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐙𝐈 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎!
27-06-2026
𝐑𝐔𝐀𝐇𝐀 𝐌𝐁𝐔𝐘𝐔𝐍𝐈 𝐘𝐀𝐅𝐔𝐑𝐈𝐊𝐀; “𝐂𝐇𝐈𝐄𝐅 𝐂𝐇𝐎𝐆𝐀𝐕𝐀𝐓𝐀𝐌𝐁𝐔𝐋𝐄” 𝐀𝐊𝐈𝐓𝐄𝐊𝐀 𝐌𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐎 𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐀!
27-06-2026
𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐎 𝐂𝐇𝐀 𝐔𝐌𝐖𝐀𝐆𝐈𝐋𝐈𝐀𝐉𝐈 𝐍𝐈 𝐔𝐅𝐔𝐍𝐆𝐔𝐎 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐏𝐈𝐍𝐃𝐔𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐔𝐂𝐇𝐔𝐌𝐈 𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈: 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈
27-06-2026
𝐂𝐂𝐌 𝐘𝐀𝐔𝐍𝐆𝐀 𝐌𝐊𝐎𝐍𝐎 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐖𝐀 𝐍𝐉𝐎𝐌𝐁𝐄 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐙𝐀 𝐔𝐙𝐀𝐋𝐈𝐒𝐇𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐀𝐋𝐈
27-06-2026
𝐀𝐌𝐀𝐍𝐈 𝐍𝐈 𝐌𝐒𝐈𝐍𝐆𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐎: 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈
27-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐑𝐀𝐒𝐌𝐈 𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀!!
27-06-2026
𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀 𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐋𝐄𝐖𝐀 𝐍𝐉𝐎𝐌𝐁𝐄, 𝐀𝐇𝐈𝐌𝐈𝐙𝐀 𝐕𝐈𝐎𝐍𝐆𝐎𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐊𝐔𝐈𝐒𝐇𝐈 𝐃𝐇𝐀𝐍𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐍𝐀 𝐔𝐓𝐔 𝐊𝐖𝐀 𝐕𝐈𝐓𝐄𝐍𝐃𝐎
27-06-2026
𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀: 𝐂𝐂𝐌 𝐇𝐀𝐈𝐓𝐀𝐕𝐔𝐌𝐈𝐋𝐈𝐀 𝐔𝐙𝐄𝐌𝐁𝐄, 𝐕𝐈𝐎𝐍𝐆𝐎𝐙𝐈 𝐖𝐀𝐖𝐀𝐉𝐈𝐁𝐈𝐊𝐄 𝐊𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐍𝐆𝐀𝐌𝐎𝐓𝐎 𝐙𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈
27-06-2026
𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀𝐀𝐀, 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐀𝐍𝐙𝐈𝐀 𝐑𝐔𝐀𝐇𝐀 𝐌𝐁𝐔𝐘𝐔𝐍𝐈!
27-06-2026
𝐌𝐈𝐊𝐎𝐏𝐎 𝐘𝐀 𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈𝐌𝐈𝐀 𝟏𝟎% 𝐘𝐀𝐂𝐇𝐎𝐂𝐇𝐄𝐀 𝐔𝐂𝐇𝐔𝐌𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐊𝐔𝐍𝐃𝐈 𝐌𝐀𝐀𝐋𝐔𝐌
27-06-2026
𝐍𝐃𝐆 𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀 𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐋𝐄𝐖𝐀 𝐑𝐔𝐕𝐔𝐌𝐀, 𝐀𝐇𝐈𝐌𝐈𝐙𝐀 𝐔𝐌𝐎𝐉𝐀 𝐍𝐀 𝐌𝐒𝐇𝐈𝐊𝐀𝐌𝐀𝐍𝐎 𝐍𝐃𝐈𝐎 𝐍𝐆𝐔𝐕𝐔 𝐘𝐀 𝐂𝐂𝐌
27-06-2026
𝐊𝐇𝐄𝐑𝐈 𝐘𝐀 𝐒𝐈𝐊𝐔 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐌𝐀𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐘𝐀 𝐌𝐓𝐎𝐓𝐎 𝐖𝐀 𝐀𝐅𝐑𝐈𝐊𝐀
27-06-2026
𝐌𝐇𝐄. 𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐀𝐍𝐀𝐖𝐀𝐏𝐄𝐍𝐃𝐀 𝐒𝐀𝐍𝐀 𝐖𝐀𝐓𝐀𝐍𝐙𝐀𝐍𝐈𝐀, 𝐖𝐀𝐓𝐔𝐌𝐈𝐒𝐇𝐈 𝐖𝐀 𝐔𝐌𝐌𝐀 𝐓𝐈𝐌𝐈𝐙𝐄𝐍𝐈 𝐖𝐀𝐉𝐈𝐁𝐔 𝐖𝐄𝐍𝐔 𝐊𝐈𝐊𝐀𝐌𝐈𝐋𝐈𝐅𝐔: 𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀
27-06-2026