RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi ameikaribisha Ufaransa kuja Zanzibar kuangalia fursa za uwekezaji kwenye sekta za Utalii, Uvuvi na ufugaji wa samaki, Bandari, Mafuta na Gesi pamoja na Sekta ya usafirishaji wa majini.
Rais Dk. Mwinyi aliyasema hayo kwenye Kongamano la kwanza la biashara lililojumuisha wadau wakubwa wa biashara na wawekezaji, Wamiliki wa viwanda kutoka Ufaransa na Jumuiya za wafanyabiashara wa Zanzibar, kwenye Ukumbi wa hotel ya Park Hayatt iliyopo Shangani, Mji Mkongwe Wilaya ya Mjini, Mkoa wa Mjini Magharibi.
Dk. Mwinyi aliueleza ugeni huo ulioongozwa na Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa, Mhe. Ali Jabir Mwadini pamoja na Balozi wa Ufaransa nchini, Mhe. Nabil Hajlaoui kwamba Utalii wa Zanzibar una mchango mkubwa kwa Uchumi wa nchi.
Alisema, Utalii unaochangia asilimia 30 ya pato la taifa ambao unajumuisha utalii wa fukwe, Urithi, michezo, pamoja na utalii mpya wa afya na mikutano ya kimataifa.
Akizichambua sekta nyengine za maendeleo, Rais Dk. Mwinyi aliwaeleza wafanyabiashara na wawekezaji hao kutoka Ufaransa kwamba Zanzibar pia imejikita kwenye sekta ya Uchumi wa Buluu, ambayo imejipambanua kwenye maeneo muhimu yakiwemo Uvuvi na ufugaji wa vifaranga vya Samaki, ukulima wa mwani na Utalii.
Pia alisema, sekta ya Uvuvi na ufugaji wa Samaki, hutoa fursa nyingi kwa wavuvi na ajira za mtu mmoja mmoja wanaojihusisha na shughuli za maboti na majahazi, kilimo cha Mwani kilichobeba asilimia kubwa ya kina mama wanaoongoza kuzalisha mwani mzuri Afrika.
Rais Dk. Mwinyi akieleza fursa nyengine za Uchumi wa buluu, aliiueleza ugeni huo kuwa Zanzibar inanufaika na Sekta ya Bandari zikiwemo Bandari jumuishi ya Mangapwani iliyo kwenye matengenezo makubwa, yenye nia ya kusafirisha na kuingiza makontena ya wafanyabiasaha walio wengi wa ndani na nje.
Alisema, bandari ya Malindi, Mkokotoni na bandari ya Fumba zinaendeleza uchumi wa nchi ili kukidhi mahitaji ya uchumi wa watu kama vituo muhimu vya usafirishaji, usambazaji wa bidhaa kutoa huduma na kufanyia biashara ikiwemo kupokelea mizigo, kusafirishia mazao, na mahitaji mbalimbali kama mafuta, nafaka, na kukuza uchumi wa nchi.
Alisema, sekta hiyo pia inaimarisha biashara na uchumi kupitia bandari za Zanzibar, Pemba, Tanga, Dar es Salaam na Mtwara kusafirisha maeneo mengine ikiwemo Msumbiji, visiwa vya Comoro na kwengineko.
Hata hivyo, Rais Dk. Mwinyi amewakaribisha wafanyabiashara hao kutenga muda na kutembelea vivutio vya utalii vilivyomo, ukiwemo Mji Mkongwe wa Zanzibar ambao ni utithi wa Kimataifa, fukwe nzuri za bahari pamoja na vivutio vyengine.
Akizungumza kwenye hafla hiyo, Balozi wa Ufaransa nchini, Mhe. Nabil Hajlaoui amesifu ushirikiano uliopo baina ya Serikali za Tanzania na Ufaransa, wafanyabiashara wa pande mbili hizo za Diplomasia pamoja na kukua kwa jamii za nchini mbili hizo.
Akigusia, Ushirikiano baina ya Serikali hizo, alisifu uhusiano mzuri uliopo baina yao ni wa historia.
Aidha, alisema Ufaransa na Tanzania ikiwemo Zanzibar zimeimarisha ushirikiano kwa jamii na kubadilisha uzoefu wa masuala mbaliumbali ikiwemo kujifunza tamaduni za pande mbili za ushirikiano, kuimarisha masuala ya elimu kwa kuweka mikakati mizuri ya kuzifanya jamii za pande mbili hizo kunufaika kitaaluma.
Naye, Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa Mhe. Ali Jabir Mwadini amesema uhusiano mzuri wa Dipolomasia uliopo baina ya Tanzania na Ufaransa umekuwa na mafanikio makubwa kwa nchi mbili hizi kufanikiwa kusaini makubaliano yenye tija kwa Uchumi na fursa za maendeleo.
Aidha, alisema moja ya faida kubwa iliyopatikana kwenye ushirikiano uliopo mbali na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan kuzuru mara mbili taifa la Ufansa ikiwemo Mwezi Febuari mwaka 2022 na wiki chache zilizopita, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kuzuru Ufaransa kwa ziara za kikazi, kupata mialiko kadhaa ya wadau wa pande mbili hizo kutembeleana wakiwemo wafanyabiasha na wawekezaji ni tija na fursa adhimu za ushirikiano uliopo.
Kwa upande wake, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwekezaji, Shariff Ali Shariff amepongeza hatua kubwa ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ya kuboresha mazingira salama ya uwekezaji ikiwemo kuimarisha miundombinu ya barabara na mawasiliano nchi nzima na kuboresha sehemu za utalii.
Kongamano hilo la wafabiashara baina ya Ufaransa na Tanzania ikiwemo Zanzibar lilijadili masuala mbalimbali ya biasahara na uwekezaji ikiwemo nishati, Miundombinu, Utalii, Uchumi wa Buluu, masuala ya maendeleo ya teknolojia, Usafi wa mazingira na mambo mengine.
Limetayarishwa na kudhaminiwa na hizo mbili, Mtandao wa wafanyabiashara wakubwa kutoka Ufaransa unaohusisha wafanyabiashara, wawekezaji, wadau wa biashara kutoka kampuni kubwa za Ufaransa, Jumuiya za wafanyabiasha Zanzibar (Zanzibar National Chamber of Commerce “ZNCC” za Ufaransa na Zanzibar).
𝐒𝐀𝐒𝐀 𝐍𝐈 𝐙𝐀𝐌𝐔 𝐘𝐀 𝐏𝐖𝐀𝐍𝐈; 𝐀𝐑𝐃𝐇𝐈 𝐘𝐀 𝐇𝐈𝐒𝐓𝐎𝐑𝐈𝐀, 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐀𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀!!!!!
24-06-2026
𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈 𝐘𝐀𝐌𝐏𝐀 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐌𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐇𝐈𝐒𝐓𝐎𝐑𝐈𝐀
24-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐙𝐈𝐍𝐃𝐔𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐋𝐀 𝐖𝐀𝐊𝐄𝐑𝐄𝐊𝐄𝐓𝐖𝐀 𝐌𝐋𝐀𝐍𝐃𝐄𝐆𝐄, 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐒𝐀-𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀
24-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐍𝐀. 𝟏𝟎 𝐌𝐀𝐅𝐈𝐅𝐈, 𝐀𝐒𝐈𝐒𝐈𝐓𝐈𝐙𝐀 𝐀𝐌𝐀𝐍𝐈, 𝐔𝐌𝐎𝐉𝐀 𝐍𝐀 𝐌𝐒𝐇𝐈𝐊𝐀𝐌𝐀𝐍𝐎
24-06-2026
𝐌𝐑𝐀𝐃𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐎 𝐘𝐀 𝐔𝐅𝐔𝐍𝐃𝐈 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎 𝐊𝐔𝐅𝐔𝐍𝐆𝐔𝐀 𝐅𝐔𝐑𝐒𝐀 𝐙𝐀 𝐀𝐉𝐈𝐑𝐀 𝐊𝐖𝐀 𝐕𝐈𝐉𝐀𝐍𝐀
24-06-2026
𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎, 𝐙𝐀𝐌𝐔 𝐘𝐄𝐍𝐔 𝐍𝐈 𝐋𝐄𝐎!
24-06-2026
𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀: 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐒𝐔𝐋𝐔𝐇𝐔 𝐇𝐀𝐒𝐒𝐀𝐍 𝐍𝐈 𝐌𝐓𝐄𝐊𝐄𝐋𝐄𝐙𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐀𝐇𝐈𝐑𝐈 𝐖𝐀 𝐀𝐇𝐀𝐃𝐈 𝐙𝐀 𝐂𝐂𝐌
24-06-2026
𝐒𝐈𝐌𝐔 𝐈𝐌𝐄𝐈𝐓𝐀, 𝐍𝐄𝐄𝐌𝐀 𝐘𝐀 𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐙𝐈 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎!
24-06-2026
𝐑𝐔𝐀𝐇𝐀 𝐌𝐁𝐔𝐘𝐔𝐍𝐈 𝐘𝐀𝐅𝐔𝐑𝐈𝐊𝐀; “𝐂𝐇𝐈𝐄𝐅 𝐂𝐇𝐎𝐆𝐀𝐕𝐀𝐓𝐀𝐌𝐁𝐔𝐋𝐄” 𝐀𝐊𝐈𝐓𝐄𝐊𝐀 𝐌𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐎 𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐀!
24-06-2026
𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐎 𝐂𝐇𝐀 𝐔𝐌𝐖𝐀𝐆𝐈𝐋𝐈𝐀𝐉𝐈 𝐍𝐈 𝐔𝐅𝐔𝐍𝐆𝐔𝐎 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐏𝐈𝐍𝐃𝐔𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐔𝐂𝐇𝐔𝐌𝐈 𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈: 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈
24-06-2026
𝐂𝐂𝐌 𝐘𝐀𝐔𝐍𝐆𝐀 𝐌𝐊𝐎𝐍𝐎 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐖𝐀 𝐍𝐉𝐎𝐌𝐁𝐄 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐙𝐀 𝐔𝐙𝐀𝐋𝐈𝐒𝐇𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐀𝐋𝐈
24-06-2026
𝐀𝐌𝐀𝐍𝐈 𝐍𝐈 𝐌𝐒𝐈𝐍𝐆𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐎: 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈
24-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐑𝐀𝐒𝐌𝐈 𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀!!
24-06-2026
𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀 𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐋𝐄𝐖𝐀 𝐍𝐉𝐎𝐌𝐁𝐄, 𝐀𝐇𝐈𝐌𝐈𝐙𝐀 𝐕𝐈𝐎𝐍𝐆𝐎𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐊𝐔𝐈𝐒𝐇𝐈 𝐃𝐇𝐀𝐍𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐍𝐀 𝐔𝐓𝐔 𝐊𝐖𝐀 𝐕𝐈𝐓𝐄𝐍𝐃𝐎
24-06-2026
𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀: 𝐂𝐂𝐌 𝐇𝐀𝐈𝐓𝐀𝐕𝐔𝐌𝐈𝐋𝐈𝐀 𝐔𝐙𝐄𝐌𝐁𝐄, 𝐕𝐈𝐎𝐍𝐆𝐎𝐙𝐈 𝐖𝐀𝐖𝐀𝐉𝐈𝐁𝐈𝐊𝐄 𝐊𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐍𝐆𝐀𝐌𝐎𝐓𝐎 𝐙𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈
24-06-2026
𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀𝐀𝐀, 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐀𝐍𝐙𝐈𝐀 𝐑𝐔𝐀𝐇𝐀 𝐌𝐁𝐔𝐘𝐔𝐍𝐈!
24-06-2026
𝐌𝐈𝐊𝐎𝐏𝐎 𝐘𝐀 𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈𝐌𝐈𝐀 𝟏𝟎% 𝐘𝐀𝐂𝐇𝐎𝐂𝐇𝐄𝐀 𝐔𝐂𝐇𝐔𝐌𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐊𝐔𝐍𝐃𝐈 𝐌𝐀𝐀𝐋𝐔𝐌
24-06-2026
𝐍𝐃𝐆 𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀 𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐋𝐄𝐖𝐀 𝐑𝐔𝐕𝐔𝐌𝐀, 𝐀𝐇𝐈𝐌𝐈𝐙𝐀 𝐔𝐌𝐎𝐉𝐀 𝐍𝐀 𝐌𝐒𝐇𝐈𝐊𝐀𝐌𝐀𝐍𝐎 𝐍𝐃𝐈𝐎 𝐍𝐆𝐔𝐕𝐔 𝐘𝐀 𝐂𝐂𝐌
24-06-2026
𝐊𝐇𝐄𝐑𝐈 𝐘𝐀 𝐒𝐈𝐊𝐔 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐌𝐀𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐘𝐀 𝐌𝐓𝐎𝐓𝐎 𝐖𝐀 𝐀𝐅𝐑𝐈𝐊𝐀
24-06-2026
𝐌𝐇𝐄. 𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐀𝐍𝐀𝐖𝐀𝐏𝐄𝐍𝐃𝐀 𝐒𝐀𝐍𝐀 𝐖𝐀𝐓𝐀𝐍𝐙𝐀𝐍𝐈𝐀, 𝐖𝐀𝐓𝐔𝐌𝐈𝐒𝐇𝐈 𝐖𝐀 𝐔𝐌𝐌𝐀 𝐓𝐈𝐌𝐈𝐙𝐄𝐍𝐈 𝐖𝐀𝐉𝐈𝐁𝐔 𝐖𝐄𝐍𝐔 𝐊𝐈𝐊𝐀𝐌𝐈𝐋𝐈𝐅𝐔: 𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀
24-06-2026