RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi ameikaribisha Ufaransa kuja Zanzibar kuangalia fursa za uwekezaji kwenye sekta za Utalii, Uvuvi na ufugaji wa samaki, Bandari, Mafuta na Gesi pamoja na Sekta ya usafirishaji wa majini.
Rais Dk. Mwinyi aliyasema hayo kwenye Kongamano la kwanza la biashara lililojumuisha wadau wakubwa wa biashara na wawekezaji, Wamiliki wa viwanda kutoka Ufaransa na Jumuiya za wafanyabiashara wa Zanzibar, kwenye Ukumbi wa hotel ya Park Hayatt iliyopo Shangani, Mji Mkongwe Wilaya ya Mjini, Mkoa wa Mjini Magharibi.
Dk. Mwinyi aliueleza ugeni huo ulioongozwa na Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa, Mhe. Ali Jabir Mwadini pamoja na Balozi wa Ufaransa nchini, Mhe. Nabil Hajlaoui kwamba Utalii wa Zanzibar una mchango mkubwa kwa Uchumi wa nchi.
Alisema, Utalii unaochangia asilimia 30 ya pato la taifa ambao unajumuisha utalii wa fukwe, Urithi, michezo, pamoja na utalii mpya wa afya na mikutano ya kimataifa.
Akizichambua sekta nyengine za maendeleo, Rais Dk. Mwinyi aliwaeleza wafanyabiashara na wawekezaji hao kutoka Ufaransa kwamba Zanzibar pia imejikita kwenye sekta ya Uchumi wa Buluu, ambayo imejipambanua kwenye maeneo muhimu yakiwemo Uvuvi na ufugaji wa vifaranga vya Samaki, ukulima wa mwani na Utalii.
Pia alisema, sekta ya Uvuvi na ufugaji wa Samaki, hutoa fursa nyingi kwa wavuvi na ajira za mtu mmoja mmoja wanaojihusisha na shughuli za maboti na majahazi, kilimo cha Mwani kilichobeba asilimia kubwa ya kina mama wanaoongoza kuzalisha mwani mzuri Afrika.
Rais Dk. Mwinyi akieleza fursa nyengine za Uchumi wa buluu, aliiueleza ugeni huo kuwa Zanzibar inanufaika na Sekta ya Bandari zikiwemo Bandari jumuishi ya Mangapwani iliyo kwenye matengenezo makubwa, yenye nia ya kusafirisha na kuingiza makontena ya wafanyabiasaha walio wengi wa ndani na nje.
Alisema, bandari ya Malindi, Mkokotoni na bandari ya Fumba zinaendeleza uchumi wa nchi ili kukidhi mahitaji ya uchumi wa watu kama vituo muhimu vya usafirishaji, usambazaji wa bidhaa kutoa huduma na kufanyia biashara ikiwemo kupokelea mizigo, kusafirishia mazao, na mahitaji mbalimbali kama mafuta, nafaka, na kukuza uchumi wa nchi.
Alisema, sekta hiyo pia inaimarisha biashara na uchumi kupitia bandari za Zanzibar, Pemba, Tanga, Dar es Salaam na Mtwara kusafirisha maeneo mengine ikiwemo Msumbiji, visiwa vya Comoro na kwengineko.
Hata hivyo, Rais Dk. Mwinyi amewakaribisha wafanyabiashara hao kutenga muda na kutembelea vivutio vya utalii vilivyomo, ukiwemo Mji Mkongwe wa Zanzibar ambao ni utithi wa Kimataifa, fukwe nzuri za bahari pamoja na vivutio vyengine.
Akizungumza kwenye hafla hiyo, Balozi wa Ufaransa nchini, Mhe. Nabil Hajlaoui amesifu ushirikiano uliopo baina ya Serikali za Tanzania na Ufaransa, wafanyabiashara wa pande mbili hizo za Diplomasia pamoja na kukua kwa jamii za nchini mbili hizo.
Akigusia, Ushirikiano baina ya Serikali hizo, alisifu uhusiano mzuri uliopo baina yao ni wa historia.
Aidha, alisema Ufaransa na Tanzania ikiwemo Zanzibar zimeimarisha ushirikiano kwa jamii na kubadilisha uzoefu wa masuala mbaliumbali ikiwemo kujifunza tamaduni za pande mbili za ushirikiano, kuimarisha masuala ya elimu kwa kuweka mikakati mizuri ya kuzifanya jamii za pande mbili hizo kunufaika kitaaluma.
Naye, Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa Mhe. Ali Jabir Mwadini amesema uhusiano mzuri wa Dipolomasia uliopo baina ya Tanzania na Ufaransa umekuwa na mafanikio makubwa kwa nchi mbili hizi kufanikiwa kusaini makubaliano yenye tija kwa Uchumi na fursa za maendeleo.
Aidha, alisema moja ya faida kubwa iliyopatikana kwenye ushirikiano uliopo mbali na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan kuzuru mara mbili taifa la Ufansa ikiwemo Mwezi Febuari mwaka 2022 na wiki chache zilizopita, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kuzuru Ufaransa kwa ziara za kikazi, kupata mialiko kadhaa ya wadau wa pande mbili hizo kutembeleana wakiwemo wafanyabiasha na wawekezaji ni tija na fursa adhimu za ushirikiano uliopo.
Kwa upande wake, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwekezaji, Shariff Ali Shariff amepongeza hatua kubwa ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ya kuboresha mazingira salama ya uwekezaji ikiwemo kuimarisha miundombinu ya barabara na mawasiliano nchi nzima na kuboresha sehemu za utalii.
Kongamano hilo la wafabiashara baina ya Ufaransa na Tanzania ikiwemo Zanzibar lilijadili masuala mbalimbali ya biasahara na uwekezaji ikiwemo nishati, Miundombinu, Utalii, Uchumi wa Buluu, masuala ya maendeleo ya teknolojia, Usafi wa mazingira na mambo mengine.
Limetayarishwa na kudhaminiwa na hizo mbili, Mtandao wa wafanyabiashara wakubwa kutoka Ufaransa unaohusisha wafanyabiashara, wawekezaji, wadau wa biashara kutoka kampuni kubwa za Ufaransa, Jumuiya za wafanyabiasha Zanzibar (Zanzibar National Chamber of Commerce “ZNCC” za Ufaransa na Zanzibar).
KIPINDI MAALUMU
09-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐒𝐈𝐌𝐀𝐌𝐈𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐒𝐀𝐅𝐀𝐑𝐀 𝐊𝐔𝐒𝐀𝐋𝐈𝐌𝐈𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐍𝐀 𝐊𝐈𝐉𝐈𝐖𝐄 𝐂𝐇𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐃𝐄𝐌𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈
09-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐊𝐈𝐓𝐔𝐎 𝐂𝐇𝐀 𝐀𝐅𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐋𝐎𝐋𝐄𝐍𝐈, 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈
09-06-2026
𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐘𝐀𝐀𝐌𝐁𝐈𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐂𝐇𝐀𝐆𝐔𝐀 𝐌𝐀𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐎 𝐁𝐀𝐃𝐀𝐋𝐀 𝐘𝐀 𝐌𝐀𝐀𝐍𝐃𝐀𝐌𝐀𝐍𝐎
09-06-2026
𝐌𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐓𝐈𝐁𝐔 𝐖𝐀 𝐍𝐄𝐂, 𝐈𝐓𝐈𝐊𝐀𝐃𝐈, 𝐔𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐍𝐀 𝐌𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐎 𝐂𝐂𝐌, 𝐍𝐃𝐔𝐆𝐔 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐋𝐀𝐁𝐀𝐍 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈, 𝐎𝐅𝐈𝐒𝐈 𝐙𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈
09-06-2026
𝐒𝐀𝐒𝐀 𝐍𝐈 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈, 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐃𝐎 𝐌𝐃𝐔𝐍𝐃𝐎!
09-06-2026
𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔 𝐘𝐀𝐒𝐈𝐊𝐈𝐀 𝐖𝐈𝐓𝐎 𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐋𝐈𝐍𝐃𝐀 𝐌𝐀𝐀𝐃𝐈𝐋𝐈 𝐍𝐀 𝐇𝐀𝐊𝐈 𝐙𝐀 𝐖𝐀𝐓𝐎𝐓𝐎
09-06-2026
𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐒𝐀𝐌𝐁𝐀𝐙𝐀 𝐔𝐏𝐄𝐍𝐃𝐎 𝐖𝐀 𝐀𝐆𝐀𝐏𝐄 𝐊𝐖𝐄𝐍𝐘𝐄 𝐊𝐈𝐉𝐈𝐖𝐄 𝐂𝐇𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐃𝐄𝐌𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔
09-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐀𝐍𝐙𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐊𝐀𝐆𝐔𝐀 𝐔𝐇𝐀𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐌𝐀
09-06-2026
𝐌𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐎 𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐀 𝐖𝐀 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐑𝐀𝐓𝐔 - 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀
09-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐓𝐔𝐍𝐔𝐊𝐈𝐖𝐀 𝐒𝐇𝐀𝐇𝐀𝐃𝐀 𝐘𝐀 𝐇𝐄𝐒𝐇𝐈𝐌𝐀 𝐔𝐑𝐔𝐒𝐈
09-06-2026
𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔, 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐀𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀!
09-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐑𝐀𝐒𝐌𝐈 𝐔𝐑𝐔𝐒𝐈, 𝐀𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐀 𝐍𝐀 𝐏𝐔𝐓𝐈𝐍
09-06-2026
𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎, 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀
09-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐌𝐎𝐒𝐂𝐎𝐖, 𝐔𝐑𝐔𝐒𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀
09-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐒𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐈𝐑𝐎 𝐊𝐖𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐊𝐀𝐙𝐈
09-06-2026
𝐅𝐔𝐍𝐆𝐀 𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐍𝐘𝐀𝐑𝐀 𝐋𝐄𝐎!!!
09-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐍𝐀. 𝟐 𝐊𝐀𝐓𝐀 𝐘𝐀 𝐁𝐎𝐍𝐆𝐀
09-06-2026
𝐁𝐀𝐁𝐀𝐓𝐈 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈 𝐋𝐄𝐎 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐈𝐅𝐔𝐍𝐈𝐊𝐀!!!
09-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐀 𝐍𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐇𝐀𝐍𝐀𝐍𝐆, 𝐀𝐒𝐈𝐊𝐈𝐋𝐈𝐙𝐀 𝐍𝐀 𝐊𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐀 𝐊𝐄𝐑𝐎 𝐙𝐀𝐎
09-06-2026