RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema huduma za uhamiaji kwa Mkoa wa Mjini Magharibi zinahitaji kuwekewa mazingatio maalumu ya kuimarishwa wake.
Rais Dk. Mwinyi ameyasema hayo alipoweka jiwe la Msingi la ujenzi wa Ofisi za Jeshi la Uhamiaji kwa Mkoa wa Mjini Magharibi, maeneo ya Mazizini Wilaya ya Mjini.
Alisema, Mkoa huo una vituo vya uingiaji na utokaji wa watu vikiwemo, bandari ya Malindi ambayo kwa mwaka hupokea zaidi ya watalii wa Kimataifa 20,000 na Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume pia hupokea zaidi ya watalii 500,000 kwa mwaka.
“Tunahitaji kuwa na jengo kubwa na la kisasa kama hili, lenye vifaa na uwezo wa kuhudumia ongezeko la wageni wanaokuja nchini kwa dhamira tofauti ikiwemo uwekezaji kwenye sekta mbalimbali za Uchumi”. Alifafanua Rais Dk. Mwinyi.
Alisema, kukamilika kwa ujenzi wa jengo hilo kutaongeza na kuimarisha ari na kasi ya utoaji wa huduma bora za Uhamiaji, kwa Mkoa wa Mjini Magharibi na Manispaa zake tatu.
Alisema, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea kuimarisha miundo mbinu imara na huduma bora za jamii zikiwemo barabara, maji Safi na Salama, Skuli za kisasa na hospitali kubwa zenye huduma bingwa kwa Unguja na Pemba ili kuweka mazingira bora ya utoaji huduma sambamba na kuboresha teknolojia ya Mifumo ya Utoaji Huduma kwa njia ya Kielektroniki.
Pia, Dk. Mwinyi alieleza kwa kipindi cha miaka 60 ya Muungano wa Tanzania, taifa limeshuhudia mafankio makubwa ikiwemo kuimarika kwa miundombinu ya utoaji wa huduma bora hasa kupitia Jeshi la Uhamiaji Zanzibar ikiwemo ujenzi wa Ofisi za Kisasa kwa mikoa yote ya Unguja na Pemba, sambamba na baadhi ya Wilaya za Unguja na Pemba.
Alisema mafanikio hayo ni miongoni mwa matunda ya Muungano wa Tanzaniaa ambapo wananchi wa Zanzibar wananufaika kupitia Muungano huo.
Rais Dk. Mwinyi amewapongeza Watanzania wote kwa mafanikio makubwa yaliyopatika kwa sekta zote za maendeleo ndani ya kipindi cha miaka 60 ya Muungano wa Tanzania pamoja na kuwashukuru viongozi wa Awamu mbalimbali za Serikali ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kusimamia, kudumisha na kuimarisha Muungano huo kwa faida ya pande zote mbili za Muungano.
“Kwa dhati kabisa nimpongeze Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa dhamira yake ya dhati ya kuimarisha shughuli na Taasisi zote za Muungano ziliopo hapa Zanzibar, zikiwemo Idara ya Uhamiaji kwa uimarishaji wa miundombinu ya kisasa, vitendea kazi, Majengo mazuri na Mifumo ya Kielektroniki katika kurahisisha utoaji wa huduma kwa Wananchi na Wageni”. Alipongeza Rais Dk. Mwinyi.
Vilevile, Rais Dk. Mwinyi aliiongeza Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, kwa hatua mbalimbali ilizozichukua kwa kuendelea kuimarisha huduma zinazotolewa na jeshi la Uhamiaji kwa pande zote mbili za Muungano, kuimarisha majukumu ya jeshi hilo, kuimarisha majengo, utoaji wa mafunzo kwa watumishi, kusimamia Stahiki za watumishi wote pamoja na kuendelea kuzifanyia maboresho ya mara kwa mara Sheria na Kanuni za Uhamiaji nchini.
Rais Dk. Mwinyi alieleza, juhudi za Serikali zote mbili za SMZ na SMT ni kubwa kwa kuhakikisha Watanzania na Wageni wanaoitembelea Tanzania wanapata huduma bora za uhamiaji.
Alisema, ni wajibu wa kila Mtanzania kushirikiana na Serikali katika kuulinda, kuumirasha, kuuendeleza na kuudumisha Muungano huo kwa dhamira ile ile
ya Waasisi wa Taifa la Tanzania ili ulete mafanikio zaidi kwa kizazi kiliopo sasa na wale watakaokuja baadae sambamba na kutunza Miuondombinu ya miradi yore ya maendeleo ili kudumu kwenye ubora wake kwa malengo yaliyokusudiwa wani watu wa pande zote mbili za Muungano ni wanufaika na Muungano huo.
Akizungumza kwenye hafla hiyo, Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Mhandisi Hamad Yussuf Masauni alisema mbali na mafanikio mengi yaliyopatikana ndani ya miaka 60 ya Muungano wa Tangantika na Zainabar ni pamoja na Jeshi la Uhamiaji kupanda ngazi ya juu kutoka ilikokua ‘Idara ya Uhamiaji’ hadi sasa kuwa ‘Jeshi la Uhamiaji’ pamoja na kupandishwa hadhi na vyemo kwa makamanda wa jeshi hilo kutoka ndazi za chini pamoja na wa ndazi za juu kupanda maradufu.
Kwa upande wake Kamisha Generali wa Uhamiaji Tanzania Dk. Anna Peter Makakala alisema ujenzi wa jengo la ghorofa tano la ofisi za Uhamiaji Mkoa wa Mjini Magharibi utagharimu fedha za kitanzania shilingi bilioni 19.9 hadi kukamilika kwake mwezi Ogasti mwakani ambapo kwasasa limefikia hatua ya silimia 53 ya ujenzi wake.
Kamisha wa Uhamiaji Zanzibar, Hassan Ali Hassan aliiomba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuwapatia eneo la ujenzi wa ofisi za Uhamiaji kwa maeneo ya Fumba Wilaya ya Magharibi B kwani eneo hilo kwasasa lina mahitaji makubwa ya huduma za jeshi hilo kutokana na kasi kukuwa kwa sekta za utalii na Uchumi wa Buluu kulikochangiwa na kuwepo kwa bandari kwenye eneo hilo na uwekezaji mkubwa wa utalii.
Sherehe za miaka 60 ya Muungano wa Tanzania chini ya kaulimbiu, “Tumeshikamana na Tumeimarika kwa Maendeleo ya Taifa Letu”, zinaashiria kuanza rasmi kwa shughuli mbalimbali za kijamii ikiwemo upandaji wa miti, usafi wa mazingira na ushiriki wa wananchi na viongozi kwenye matukio ya uzinduzi wa miradi ya maendeleo na uwekaji wa mawe ya msingi kwa maeneo mbalimbali ya Tanzania.
Kilele cha sherehe hizo ni tarehe 26 Aprili, 2024 kwenye viwanja vya Uhuru, Dar es Salaam ambapo Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Dk. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
KIPINDI MAALUMU
09-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐒𝐈𝐌𝐀𝐌𝐈𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐒𝐀𝐅𝐀𝐑𝐀 𝐊𝐔𝐒𝐀𝐋𝐈𝐌𝐈𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐍𝐀 𝐊𝐈𝐉𝐈𝐖𝐄 𝐂𝐇𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐃𝐄𝐌𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈
09-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐊𝐈𝐓𝐔𝐎 𝐂𝐇𝐀 𝐀𝐅𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐋𝐎𝐋𝐄𝐍𝐈, 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈
09-06-2026
𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐘𝐀𝐀𝐌𝐁𝐈𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐂𝐇𝐀𝐆𝐔𝐀 𝐌𝐀𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐎 𝐁𝐀𝐃𝐀𝐋𝐀 𝐘𝐀 𝐌𝐀𝐀𝐍𝐃𝐀𝐌𝐀𝐍𝐎
09-06-2026
𝐌𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐓𝐈𝐁𝐔 𝐖𝐀 𝐍𝐄𝐂, 𝐈𝐓𝐈𝐊𝐀𝐃𝐈, 𝐔𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐍𝐀 𝐌𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐎 𝐂𝐂𝐌, 𝐍𝐃𝐔𝐆𝐔 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐋𝐀𝐁𝐀𝐍 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈, 𝐎𝐅𝐈𝐒𝐈 𝐙𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈
09-06-2026
𝐒𝐀𝐒𝐀 𝐍𝐈 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈, 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐃𝐎 𝐌𝐃𝐔𝐍𝐃𝐎!
09-06-2026
𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔 𝐘𝐀𝐒𝐈𝐊𝐈𝐀 𝐖𝐈𝐓𝐎 𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐋𝐈𝐍𝐃𝐀 𝐌𝐀𝐀𝐃𝐈𝐋𝐈 𝐍𝐀 𝐇𝐀𝐊𝐈 𝐙𝐀 𝐖𝐀𝐓𝐎𝐓𝐎
09-06-2026
𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐒𝐀𝐌𝐁𝐀𝐙𝐀 𝐔𝐏𝐄𝐍𝐃𝐎 𝐖𝐀 𝐀𝐆𝐀𝐏𝐄 𝐊𝐖𝐄𝐍𝐘𝐄 𝐊𝐈𝐉𝐈𝐖𝐄 𝐂𝐇𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐃𝐄𝐌𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔
09-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐀𝐍𝐙𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐊𝐀𝐆𝐔𝐀 𝐔𝐇𝐀𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐌𝐀
09-06-2026
𝐌𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐎 𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐀 𝐖𝐀 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐑𝐀𝐓𝐔 - 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀
09-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐓𝐔𝐍𝐔𝐊𝐈𝐖𝐀 𝐒𝐇𝐀𝐇𝐀𝐃𝐀 𝐘𝐀 𝐇𝐄𝐒𝐇𝐈𝐌𝐀 𝐔𝐑𝐔𝐒𝐈
09-06-2026
𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔, 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐀𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀!
09-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐑𝐀𝐒𝐌𝐈 𝐔𝐑𝐔𝐒𝐈, 𝐀𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐀 𝐍𝐀 𝐏𝐔𝐓𝐈𝐍
09-06-2026
𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎, 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀
09-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐌𝐎𝐒𝐂𝐎𝐖, 𝐔𝐑𝐔𝐒𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀
09-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐒𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐈𝐑𝐎 𝐊𝐖𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐊𝐀𝐙𝐈
09-06-2026
𝐅𝐔𝐍𝐆𝐀 𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐍𝐘𝐀𝐑𝐀 𝐋𝐄𝐎!!!
09-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐍𝐀. 𝟐 𝐊𝐀𝐓𝐀 𝐘𝐀 𝐁𝐎𝐍𝐆𝐀
09-06-2026
𝐁𝐀𝐁𝐀𝐓𝐈 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈 𝐋𝐄𝐎 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐈𝐅𝐔𝐍𝐈𝐊𝐀!!!
09-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐀 𝐍𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐇𝐀𝐍𝐀𝐍𝐆, 𝐀𝐒𝐈𝐊𝐈𝐋𝐈𝐙𝐀 𝐍𝐀 𝐊𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐀 𝐊𝐄𝐑𝐎 𝐙𝐀𝐎
09-06-2026