RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema huduma za uhamiaji kwa Mkoa wa Mjini Magharibi zinahitaji kuwekewa mazingatio maalumu ya kuimarishwa wake.
Rais Dk. Mwinyi ameyasema hayo alipoweka jiwe la Msingi la ujenzi wa Ofisi za Jeshi la Uhamiaji kwa Mkoa wa Mjini Magharibi, maeneo ya Mazizini Wilaya ya Mjini.
Alisema, Mkoa huo una vituo vya uingiaji na utokaji wa watu vikiwemo, bandari ya Malindi ambayo kwa mwaka hupokea zaidi ya watalii wa Kimataifa 20,000 na Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume pia hupokea zaidi ya watalii 500,000 kwa mwaka.
“Tunahitaji kuwa na jengo kubwa na la kisasa kama hili, lenye vifaa na uwezo wa kuhudumia ongezeko la wageni wanaokuja nchini kwa dhamira tofauti ikiwemo uwekezaji kwenye sekta mbalimbali za Uchumi”. Alifafanua Rais Dk. Mwinyi.
Alisema, kukamilika kwa ujenzi wa jengo hilo kutaongeza na kuimarisha ari na kasi ya utoaji wa huduma bora za Uhamiaji, kwa Mkoa wa Mjini Magharibi na Manispaa zake tatu.
Alisema, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea kuimarisha miundo mbinu imara na huduma bora za jamii zikiwemo barabara, maji Safi na Salama, Skuli za kisasa na hospitali kubwa zenye huduma bingwa kwa Unguja na Pemba ili kuweka mazingira bora ya utoaji huduma sambamba na kuboresha teknolojia ya Mifumo ya Utoaji Huduma kwa njia ya Kielektroniki.
Pia, Dk. Mwinyi alieleza kwa kipindi cha miaka 60 ya Muungano wa Tanzania, taifa limeshuhudia mafankio makubwa ikiwemo kuimarika kwa miundombinu ya utoaji wa huduma bora hasa kupitia Jeshi la Uhamiaji Zanzibar ikiwemo ujenzi wa Ofisi za Kisasa kwa mikoa yote ya Unguja na Pemba, sambamba na baadhi ya Wilaya za Unguja na Pemba.
Alisema mafanikio hayo ni miongoni mwa matunda ya Muungano wa Tanzaniaa ambapo wananchi wa Zanzibar wananufaika kupitia Muungano huo.
Rais Dk. Mwinyi amewapongeza Watanzania wote kwa mafanikio makubwa yaliyopatika kwa sekta zote za maendeleo ndani ya kipindi cha miaka 60 ya Muungano wa Tanzania pamoja na kuwashukuru viongozi wa Awamu mbalimbali za Serikali ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kusimamia, kudumisha na kuimarisha Muungano huo kwa faida ya pande zote mbili za Muungano.
“Kwa dhati kabisa nimpongeze Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa dhamira yake ya dhati ya kuimarisha shughuli na Taasisi zote za Muungano ziliopo hapa Zanzibar, zikiwemo Idara ya Uhamiaji kwa uimarishaji wa miundombinu ya kisasa, vitendea kazi, Majengo mazuri na Mifumo ya Kielektroniki katika kurahisisha utoaji wa huduma kwa Wananchi na Wageni”. Alipongeza Rais Dk. Mwinyi.
Vilevile, Rais Dk. Mwinyi aliiongeza Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, kwa hatua mbalimbali ilizozichukua kwa kuendelea kuimarisha huduma zinazotolewa na jeshi la Uhamiaji kwa pande zote mbili za Muungano, kuimarisha majukumu ya jeshi hilo, kuimarisha majengo, utoaji wa mafunzo kwa watumishi, kusimamia Stahiki za watumishi wote pamoja na kuendelea kuzifanyia maboresho ya mara kwa mara Sheria na Kanuni za Uhamiaji nchini.
Rais Dk. Mwinyi alieleza, juhudi za Serikali zote mbili za SMZ na SMT ni kubwa kwa kuhakikisha Watanzania na Wageni wanaoitembelea Tanzania wanapata huduma bora za uhamiaji.
Alisema, ni wajibu wa kila Mtanzania kushirikiana na Serikali katika kuulinda, kuumirasha, kuuendeleza na kuudumisha Muungano huo kwa dhamira ile ile
ya Waasisi wa Taifa la Tanzania ili ulete mafanikio zaidi kwa kizazi kiliopo sasa na wale watakaokuja baadae sambamba na kutunza Miuondombinu ya miradi yore ya maendeleo ili kudumu kwenye ubora wake kwa malengo yaliyokusudiwa wani watu wa pande zote mbili za Muungano ni wanufaika na Muungano huo.
Akizungumza kwenye hafla hiyo, Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Mhandisi Hamad Yussuf Masauni alisema mbali na mafanikio mengi yaliyopatikana ndani ya miaka 60 ya Muungano wa Tangantika na Zainabar ni pamoja na Jeshi la Uhamiaji kupanda ngazi ya juu kutoka ilikokua ‘Idara ya Uhamiaji’ hadi sasa kuwa ‘Jeshi la Uhamiaji’ pamoja na kupandishwa hadhi na vyemo kwa makamanda wa jeshi hilo kutoka ndazi za chini pamoja na wa ndazi za juu kupanda maradufu.
Kwa upande wake Kamisha Generali wa Uhamiaji Tanzania Dk. Anna Peter Makakala alisema ujenzi wa jengo la ghorofa tano la ofisi za Uhamiaji Mkoa wa Mjini Magharibi utagharimu fedha za kitanzania shilingi bilioni 19.9 hadi kukamilika kwake mwezi Ogasti mwakani ambapo kwasasa limefikia hatua ya silimia 53 ya ujenzi wake.
Kamisha wa Uhamiaji Zanzibar, Hassan Ali Hassan aliiomba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuwapatia eneo la ujenzi wa ofisi za Uhamiaji kwa maeneo ya Fumba Wilaya ya Magharibi B kwani eneo hilo kwasasa lina mahitaji makubwa ya huduma za jeshi hilo kutokana na kasi kukuwa kwa sekta za utalii na Uchumi wa Buluu kulikochangiwa na kuwepo kwa bandari kwenye eneo hilo na uwekezaji mkubwa wa utalii.
Sherehe za miaka 60 ya Muungano wa Tanzania chini ya kaulimbiu, “Tumeshikamana na Tumeimarika kwa Maendeleo ya Taifa Letu”, zinaashiria kuanza rasmi kwa shughuli mbalimbali za kijamii ikiwemo upandaji wa miti, usafi wa mazingira na ushiriki wa wananchi na viongozi kwenye matukio ya uzinduzi wa miradi ya maendeleo na uwekaji wa mawe ya msingi kwa maeneo mbalimbali ya Tanzania.
Kilele cha sherehe hizo ni tarehe 26 Aprili, 2024 kwenye viwanja vya Uhuru, Dar es Salaam ambapo Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Dk. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈 𝐘𝐀𝐌𝐏𝐀 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐌𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐇𝐈𝐒𝐓𝐎𝐑𝐈𝐀
24-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐙𝐈𝐍𝐃𝐔𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐋𝐀 𝐖𝐀𝐊𝐄𝐑𝐄𝐊𝐄𝐓𝐖𝐀 𝐌𝐋𝐀𝐍𝐃𝐄𝐆𝐄, 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐒𝐀-𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀
24-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐍𝐀. 𝟏𝟎 𝐌𝐀𝐅𝐈𝐅𝐈, 𝐀𝐒𝐈𝐒𝐈𝐓𝐈𝐙𝐀 𝐀𝐌𝐀𝐍𝐈, 𝐔𝐌𝐎𝐉𝐀 𝐍𝐀 𝐌𝐒𝐇𝐈𝐊𝐀𝐌𝐀𝐍𝐎
24-06-2026
𝐌𝐑𝐀𝐃𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐎 𝐘𝐀 𝐔𝐅𝐔𝐍𝐃𝐈 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎 𝐊𝐔𝐅𝐔𝐍𝐆𝐔𝐀 𝐅𝐔𝐑𝐒𝐀 𝐙𝐀 𝐀𝐉𝐈𝐑𝐀 𝐊𝐖𝐀 𝐕𝐈𝐉𝐀𝐍𝐀
24-06-2026
𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎, 𝐙𝐀𝐌𝐔 𝐘𝐄𝐍𝐔 𝐍𝐈 𝐋𝐄𝐎!
24-06-2026
𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀: 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐒𝐔𝐋𝐔𝐇𝐔 𝐇𝐀𝐒𝐒𝐀𝐍 𝐍𝐈 𝐌𝐓𝐄𝐊𝐄𝐋𝐄𝐙𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐀𝐇𝐈𝐑𝐈 𝐖𝐀 𝐀𝐇𝐀𝐃𝐈 𝐙𝐀 𝐂𝐂𝐌
24-06-2026
𝐒𝐈𝐌𝐔 𝐈𝐌𝐄𝐈𝐓𝐀, 𝐍𝐄𝐄𝐌𝐀 𝐘𝐀 𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐙𝐈 𝐊𝐈𝐋𝐎𝐋𝐎!
24-06-2026
𝐑𝐔𝐀𝐇𝐀 𝐌𝐁𝐔𝐘𝐔𝐍𝐈 𝐘𝐀𝐅𝐔𝐑𝐈𝐊𝐀; “𝐂𝐇𝐈𝐄𝐅 𝐂𝐇𝐎𝐆𝐀𝐕𝐀𝐓𝐀𝐌𝐁𝐔𝐋𝐄” 𝐀𝐊𝐈𝐓𝐄𝐊𝐀 𝐌𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐎 𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐀!
24-06-2026
𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐎 𝐂𝐇𝐀 𝐔𝐌𝐖𝐀𝐆𝐈𝐋𝐈𝐀𝐉𝐈 𝐍𝐈 𝐔𝐅𝐔𝐍𝐆𝐔𝐎 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐏𝐈𝐍𝐃𝐔𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐔𝐂𝐇𝐔𝐌𝐈 𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈: 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈
24-06-2026
𝐂𝐂𝐌 𝐘𝐀𝐔𝐍𝐆𝐀 𝐌𝐊𝐎𝐍𝐎 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐖𝐀 𝐍𝐉𝐎𝐌𝐁𝐄 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐙𝐀 𝐔𝐙𝐀𝐋𝐈𝐒𝐇𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐀𝐋𝐈
24-06-2026
𝐀𝐌𝐀𝐍𝐈 𝐍𝐈 𝐌𝐒𝐈𝐍𝐆𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐎: 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈
24-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐑𝐀𝐒𝐌𝐈 𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀!!
24-06-2026
𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀 𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐋𝐄𝐖𝐀 𝐍𝐉𝐎𝐌𝐁𝐄, 𝐀𝐇𝐈𝐌𝐈𝐙𝐀 𝐕𝐈𝐎𝐍𝐆𝐎𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐊𝐔𝐈𝐒𝐇𝐈 𝐃𝐇𝐀𝐍𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐍𝐀 𝐔𝐓𝐔 𝐊𝐖𝐀 𝐕𝐈𝐓𝐄𝐍𝐃𝐎
24-06-2026
𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀: 𝐂𝐂𝐌 𝐇𝐀𝐈𝐓𝐀𝐕𝐔𝐌𝐈𝐋𝐈𝐀 𝐔𝐙𝐄𝐌𝐁𝐄, 𝐕𝐈𝐎𝐍𝐆𝐎𝐙𝐈 𝐖𝐀𝐖𝐀𝐉𝐈𝐁𝐈𝐊𝐄 𝐊𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐍𝐆𝐀𝐌𝐎𝐓𝐎 𝐙𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈
24-06-2026
𝐈𝐑𝐈𝐍𝐆𝐀 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀𝐀𝐀, 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐀𝐍𝐙𝐈𝐀 𝐑𝐔𝐀𝐇𝐀 𝐌𝐁𝐔𝐘𝐔𝐍𝐈!
24-06-2026
𝐌𝐈𝐊𝐎𝐏𝐎 𝐘𝐀 𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈𝐌𝐈𝐀 𝟏𝟎% 𝐘𝐀𝐂𝐇𝐎𝐂𝐇𝐄𝐀 𝐔𝐂𝐇𝐔𝐌𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐊𝐔𝐍𝐃𝐈 𝐌𝐀𝐀𝐋𝐔𝐌
24-06-2026
𝐍𝐃𝐆 𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀 𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐋𝐄𝐖𝐀 𝐑𝐔𝐕𝐔𝐌𝐀, 𝐀𝐇𝐈𝐌𝐈𝐙𝐀 𝐔𝐌𝐎𝐉𝐀 𝐍𝐀 𝐌𝐒𝐇𝐈𝐊𝐀𝐌𝐀𝐍𝐎 𝐍𝐃𝐈𝐎 𝐍𝐆𝐔𝐕𝐔 𝐘𝐀 𝐂𝐂𝐌
24-06-2026
𝐊𝐇𝐄𝐑𝐈 𝐘𝐀 𝐒𝐈𝐊𝐔 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐌𝐀𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐘𝐀 𝐌𝐓𝐎𝐓𝐎 𝐖𝐀 𝐀𝐅𝐑𝐈𝐊𝐀
24-06-2026
𝐌𝐇𝐄. 𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐀𝐍𝐀𝐖𝐀𝐏𝐄𝐍𝐃𝐀 𝐒𝐀𝐍𝐀 𝐖𝐀𝐓𝐀𝐍𝐙𝐀𝐍𝐈𝐀, 𝐖𝐀𝐓𝐔𝐌𝐈𝐒𝐇𝐈 𝐖𝐀 𝐔𝐌𝐌𝐀 𝐓𝐈𝐌𝐈𝐙𝐄𝐍𝐈 𝐖𝐀𝐉𝐈𝐁𝐔 𝐖𝐄𝐍𝐔 𝐊𝐈𝐊𝐀𝐌𝐈𝐋𝐈𝐅𝐔: 𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀
24-06-2026
𝐂𝐂𝐌 𝐇𝐀𝐈𝐓𝐎𝐑𝐔𝐃𝐈 𝐍𝐘𝐔𝐌𝐀 𝐊𝐔𝐋𝐈𝐍𝐃𝐀 𝐌𝐀𝐒𝐋𝐀𝐇𝐈 𝐘𝐀 𝐌𝐊𝐔𝐋𝐈𝐌𝐀 𝐖𝐀 𝐊𝐎𝐑𝐎𝐒𝐇𝐎: 𝐑𝐀𝐁𝐈𝐀
24-06-2026