CHONGOLO: MAWAZIRI 3 KUHUSIKA FIDIA MRADI WA UMEME TABORA - KATAVI
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), amesema atakutana na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Wizara ya Nishati na Wizara ya Fedha, kwa ajili ya kutatua changamoto ya malipo ya fidia ya wananchi ambao ardhi yao imechukuliwa kwa ajili ya kutekeleza Mradi wa Ujenzi wa Msongo wa Umeme kutoka Tabora hadi Katavi.
Katibu Mkuu Ndugu Chongolo amesema hayo leo Oktoba 5, 2023, wakati akizungumza na wananchi wa Inyonga, wilayani Mlele, Mkoa wa Katavi, kuhusu mradi huo wa msongo wa umeme ambao utauwezesha mkoa huo sasa kuunganishwa katika gridi ya taifa, hivyo kumaliza kabisa changamoto ya nishati hiyo katika maeneo hayo.
“Nikirudi Dar es Salaam nitakaa na pande zote zinazohusiana na ulipaji fidia wakiwemo Wizara ya Nishati, Wizara ya Fedha na Wizara ya Ardhi pamoja na wadau wengine ili watuambie wanaendaje na nini kifanyike kusukuma suala la fidia ili walipwe haraka.
Ndugu Chongolo amewahikishia wananchi wa Mkoa wa Katavi kuwa katika kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2020 - 2025, kuunganisha Mkoa wa Katavi kwenye gridi ya taifa, ni mojawapo ya vipaumbele vya muhimu kwa Serikali.
Chongolo ambaye yupo katika mkoa huo kwa ziara ya kuhamaisha uhai wa Chama, kukagua utekelezaji wa Ilani pamoja na kusikiliza changamoto za wananchi na kuzitafutia majawabu, amesema Serikali tayari imeshatenga fedha kwa ajili ya kutekeleza mradi huo.
“Na huu mradi sio mradi tu bali ni mradi wenye lengo mahususi la kutafuta majawabu kwa wananchi wa Katavi lakini pia kuinua shughuli za uchumi wao na wakazi wa jirani kama Sikonge na maeneo mengine.
“Mmeeleza vizuri uwezo wa kituo hapa ni megawati 1.4 na mahitaji sasa hivi yaweza kuwa yamefika megawati mbili lakini ukipeleka Majimoto kuna viwanda zaidi ya 20 au 30 vya mpunga vile viwanda vyote vinahitaji umeme.
“Ukipiga hesabu utakuta Majimoto nao wanahitaji megawati mbili mpaka tatu, kwa hiyo zinahitajika karibia megawati tano kwa wilaya ya Mlele. Ukienda Mpanda shughuli zao zinaunganisha mpaka Kalema na kalema tuna bandari." Amesema.
Ameongeza ili kubadilisha kwenda kwenye uhalisia ni kutekeleza huo mradi huku akitumia nafasi hiyo kuzungumzia suala la fidia kwa watakaopitisha mradi huo.
“Nikirudi Dar es Salaam nitakaa na pande zote zinazohusiana na ulipaji fidia wakiwemo Wizara ya Nishati,Wizara ya Fedha na Wizara ya Ardhi pamoja na wadau wengine ili watuambie wanaendaje na nini kifanyike kusukuma suala la fidia ili walipwe haraka.
Ameongeza fidia ikishalipwa itabaki kusubiri ujenzi wa laini ya umeme na kushauri watekelezaji wa mradi huo kuanzia shughuli za za awali za utekelezaji wa mradi huo kwa kuandaa mazingira.
“Wakati huu ungekuwa wakati muafaka wa kuanza kujenga nguzo kwenye maeneo yale yenye majimaji ili wakati wa masika ujenzi usimame maeneo hayo.Tunaomba mradi huu uangaliwe kwa uzito wake.
“Tukifungua na kuleta umeme kwa wananchi wa Katavi naamini mchango wao katika kukuza uchumi wa nchi hii utakwenda juu kwani kwa sasa hata ujenzi wa viwanda vikiwemo vya kuchakata tumbaku na migodi ya madini, umesimama kwasababu ya changamoto ya umeme,” amesema Ndugu Chongolo.
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
25-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
25-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
25-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
25-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
25-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
25-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
25-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
25-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
25-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
25-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
25-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
25-05-2026
𝗞𝗜𝗦𝗛𝗜𝗡𝗗𝗢 𝗖𝗛𝗔 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗖𝗛𝗔𝗣𝗢𝗞𝗘𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗛𝗔𝗡𝗚𝗪𝗘 𝗗𝗔𝗥 𝗘𝗦 𝗦𝗔𝗟𝗔𝗔𝗠
25-05-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
25-05-2026
𝗩𝗜𝗝𝗔𝗡𝗔 𝗧𝗨𝗜𝗟𝗜𝗡𝗗𝗘 𝗔𝗠𝗔𝗡𝗜 𝗬𝗔 𝗡𝗖𝗛𝗜 𝗬𝗘𝗧𝗨 - 𝗠𝗪𝗘𝗡𝗘𝗭𝗜 𝗞𝗘𝗡𝗔𝗡𝗜
25-05-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
25-05-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
25-05-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
25-05-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
25-05-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
25-05-2026