RAIS WA ZANZIBAR MHE.DK.HUSSEIN MWINYI AZUNGUMZA NA KAIMU BALOZI WA SAUDI ARABIA NCHINI TANZANIA IKULU ZANZIBAR JULY 24
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema sekta za Afya, Maji na Elimu ni muhimu kwa ustawi wa watu wa Zanzibar.
Dk. Mwinyi aliyasema hayo Ikulu, Zanzibar alipozungumza na Kaimu Balozi wa Saudi Arabia nchini, Fahad Alharbi aliefika kumtembelea. Rais Dk. Mwinyi alisema, licha ya sekta hizo kuwepo kwa kiwango kikubwa nchini lakini zinahitaji kuimarishwa zaidi ili kuwaondoshea wananchi changamoto zinazozikabili sekta hizo, hivyo aliiomba Serikali ya Saudi Arabia kuongeza ushirikiano zaidi kwenye sekta hizo. Aidha, Dk. Mwinyi aliishukuru Serikali ya Saudi kwa zawadi ya tende, tani 25 iliyoletwa kwa ajili ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na kueleza Serikali inaweka utaratibu mzuri ili iwafikie walengwa. Aidha, Rais Dk. Mwinyi ameeleza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imekua na ushirikiano wa karibu wa maendeleo na taasisi mbalimbali za kimataifa za umma na binafsi, hivyo alizikaribisha taasisi nyengine kutoka Saudi Arabia kuisaidia Zanzibar.
Naye, Kaimu Balozi wa Saudi Arabia, Fahad Alharbi akiambatana na ujumbe wa watu wanne kutoka Taasisi ya misaada ya kibinaadamu ya King Salman wa Saudi Arabia, aliahidi kuendelea kuudumisha ushirikiano wa Diplomasia uliopo baina ya Zanzibar na Saudi Arabia ambao ni wa historia. Alieleza, Serikali ya nchi hiyo imekua ikitoa misaada kwa sekta mbalimbali kwa mataifa mengi duniani. Pia Kaimu Balozi huyo, alitumia fursa hiyo kumfikisha Rais Dk. Mwinyi salamu za Mfalme wa Saudi Arabia, Salman bin Abdulazizi Al Saud nakueleza kuwa salamu za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar pia atazifikisha kwa Mfalme huyo.
Mapema, ujumbe kutoka Taasisi ya misaada ya kibinaadamu ya King Salman wa Saudi Arabia, ulikutana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora, Mhe. Haroun Ali Suleiman ofisini kwake Mazizini na kumkabidhi katuni 1,200 za tende sawa na tani 25 kwa ajili ya zawadi kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
09-12-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
09-12-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
09-12-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
09-12-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
09-12-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
09-12-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
09-12-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
09-12-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
09-12-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
09-12-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
09-12-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
09-12-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
09-12-2025
TAARIFA KWA UMMA
09-12-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
09-12-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
09-12-2025