Dk.Hussein Ali Mwinyi amesema atahakikisha Chama Cha Mapinduzi kuwa na uchumi wa uhakika utaowezesha watumishi kulipwa posho hususan mabalozi.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi amesema atahakikisha Chama Cha Mapinduzi(CCM) Zanzibar kina kuwa na uchumi wa uhakika ambao utawawezesha watumishi kulipwa posho hususan mabalozi.
Kauli hiyo ameitoa jana wakati akizungumza na mabalozi, wajumbe wa Halmashauri kuu za, Majimbo, wilaya na Mkoa wa Kaskazini Pemba katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi uliopo Wete. Alisema endapo rasilimali zilizopo ndani ya chama zikiwekezwa vizuri CCM itajiendesha bila wasi wasi wowote. Pia, alisema kupitia Uwekezaji huo wa rasilimali hizo itarahisisha chama kuwalipa posho watumishi wake ili waweze kufanya kazi vizuri. "Ninatambua kuwa watendaji wengine katika ngazi ya Mkoa na wilaya wanalipwa lakini haitoshi lazima twende chini zaidi twende jimbo,wadi,matawi na hatimaye tuwafikie mabalozi,"alisema
Alisema hatua hiyo itasaidia kufanya kazi vizuri na kwamba katika jambo hilo amewaomba wanachama wa CCM kumpa ushirikiano ili kujenga uchumi mzuri wa chama. Rais Dk.Mwinyi alisema kuna kila sababu ya kuijenga CCM kiuchumi kutokana na kuwa shughuli nyingi za kisiasa zinahitaji fedha. "Ili kazi zote za chama zifanyike Kwa maana tuwe na ofisi nzuri na vitendea kazi ikiwemo vyombo vya usafiri lazima tujenge uchumi wetu wa chama chetu,"alisema. Alisema katika ziara ambazo amezifanya Kwa Unguja na Pemba amejionea miradi mingi ya chama na kwamba endapo itatumika vizuri kitaweza kujiendesha chenyewe. "Ahadi yangu kwenu wanachama wa Mapinduzi nitatafuta mbinu za kuziendesha rasilimali zetu za chama vizuri tupate mapato mazuri tujenge ofisi zetu nzuri,tujenge ukumbi wa mikutano, tuwe na vyombo vya usafiri,"alisema
Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Mohammed Said Mohammed 'Dimwa' alisema maagizo yote aliyoyatoa Rais Dk.Mwinyi ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar chama kishaanza kufanyiwa kazi. "Tushaanza kuyafanyia kazi ikiwemo kutoa mafunzo Kwa watendaji Kwa upande wa Unguja ambapo ikitoka huko tutafanya Pemba,"alisema. Alisema agizo lingine la Rais Dk.Mwinyi ambapo limeanza kutekelezwa ni ugawaji wa vitambulisho kwa mabalozi. "Unguja tushaanza kuwapatia vitambulisho mabalozi hao na kila balozi atapata kitambulisho chake pamoja na Mambo yetu yataanza kuratibu,"alisema
Naye Katibu wa Idara ya Siasa,Uhusiano na Kimataifa CCM, Mbarouk Nassoro Mbarouk alisema katika kipindi cha miaka miwili cha Rais Dk.Mwinyi amekuwa akitangaza kipaumbele chake ni serikali ya umoja wa kitaifa. "Sasa hivi tunaona matunda yake ya kuwepo kwa hali ya amani ambapo wawekezaji wengi wamekuwa wakivutiwa kuja kuwekeza hapa Zanzibar,"alisema. Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kaskazini Pemba Mberwa Hamad Mberwa alisema Kaskazini Pemba ipo salama na kwamba chama na Serikali kinashirikiana kwa karibu. "Tumefanya uchaguzi kwa ngazi ya Uwakikishi na Ubunge pamoja na chama ambapo katika uchaguzi huo ulijitokeza baadhi ya changamoto na baada ya uchaguzi huo kwa sasa hali nzuri na tumekuwa na umoja ndani ya chama chetu ,"alisema
Mwenyekiti huyo alisema chama kina unga mkono jitihada za serikali ya awamu ya nane katika azma yake ya kujenga bandari ya Wete.
Akimkabidhi kadi ya CUF kwa Rais Dk.Mwinyi, Mbarouk Ali Mbarouk ambaye ni Katibu wa Jimbo la Tumbe alisema amehamia CCM kwa kutokana na kazi nzuri zinazofanywa na Serikali. "Baada ya kukaa na Katibu wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana(UVCCM) wilaya ya Micheweni Shakira Mohamed Hija nikahamasika na baadaye nikawashawishi vijana zaidi 300 Jimbo la Tumbe kujiunga na CCM na Leo wapo hapa mbele,"alisema. Alisema kutokana na utendaji wa serikali ya awamu ya nane hatoishia hapo na badala ya atahakikisha anawahamisha wazee kujiunga na CCM. "Kwa ridhaa yangu wala sijalazimisha kuhamia CCM nina kabidhi kadi yangu hii ya CUF kwako Mheshimiwa Makamu Mwenyekiti wa CCM ambaye ni Rais wa Zanzibar Dk.Mwinyi,"alisema
Nae Kombo Mkadamu Khatibu ambaye ni mwanachama wa CUF alisema kwa upande wake anampongeza Rais Dk.Mwinyi Kwa uchapakazi wake. "Hakuna chama chochote cha siasa hapa Zanzibar kitakacholeta kiongozi mcha Mungu kama Rais Dk.Mwinyi kutoka CCM,"alisema . Alisema kutokana na maendeleo yanayoonekana kupitia serikali ya awamu ya nane yeye na watoto wake wanahamia CCM.
KIPINDI MAALUMU
09-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐒𝐈𝐌𝐀𝐌𝐈𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐒𝐀𝐅𝐀𝐑𝐀 𝐊𝐔𝐒𝐀𝐋𝐈𝐌𝐈𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐍𝐀 𝐊𝐈𝐉𝐈𝐖𝐄 𝐂𝐇𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐃𝐄𝐌𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈
09-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐊𝐈𝐓𝐔𝐎 𝐂𝐇𝐀 𝐀𝐅𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐋𝐎𝐋𝐄𝐍𝐈, 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈
09-06-2026
𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐘𝐀𝐀𝐌𝐁𝐈𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐂𝐇𝐀𝐆𝐔𝐀 𝐌𝐀𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐎 𝐁𝐀𝐃𝐀𝐋𝐀 𝐘𝐀 𝐌𝐀𝐀𝐍𝐃𝐀𝐌𝐀𝐍𝐎
09-06-2026
𝐌𝐀𝐏𝐎𝐊𝐄𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐓𝐈𝐁𝐔 𝐖𝐀 𝐍𝐄𝐂, 𝐈𝐓𝐈𝐊𝐀𝐃𝐈, 𝐔𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐍𝐀 𝐌𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐎 𝐂𝐂𝐌, 𝐍𝐃𝐔𝐆𝐔 𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐋𝐀𝐁𝐀𝐍 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈, 𝐎𝐅𝐈𝐒𝐈 𝐙𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈
09-06-2026
𝐒𝐀𝐒𝐀 𝐍𝐈 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈, 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐃𝐎 𝐌𝐃𝐔𝐍𝐃𝐎!
09-06-2026
𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔 𝐘𝐀𝐒𝐈𝐊𝐈𝐀 𝐖𝐈𝐓𝐎 𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐋𝐈𝐍𝐃𝐀 𝐌𝐀𝐀𝐃𝐈𝐋𝐈 𝐍𝐀 𝐇𝐀𝐊𝐈 𝐙𝐀 𝐖𝐀𝐓𝐎𝐓𝐎
09-06-2026
𝐊𝐄𝐍𝐀𝐍𝐈 𝐀𝐒𝐀𝐌𝐁𝐀𝐙𝐀 𝐔𝐏𝐄𝐍𝐃𝐎 𝐖𝐀 𝐀𝐆𝐀𝐏𝐄 𝐊𝐖𝐄𝐍𝐘𝐄 𝐊𝐈𝐉𝐈𝐖𝐄 𝐂𝐇𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐃𝐄𝐌𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔
09-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐀𝐍𝐙𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐊𝐀𝐆𝐔𝐀 𝐔𝐇𝐀𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐌𝐀
09-06-2026
𝐌𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐎 𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐀 𝐖𝐀 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐀𝐑𝐀𝐓𝐔 - 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐀𝐑𝐔𝐒𝐇𝐀
09-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐓𝐔𝐍𝐔𝐊𝐈𝐖𝐀 𝐒𝐇𝐀𝐇𝐀𝐃𝐀 𝐘𝐀 𝐇𝐄𝐒𝐇𝐈𝐌𝐀 𝐔𝐑𝐔𝐒𝐈
09-06-2026
𝐀𝐑𝐔𝐌𝐄𝐑𝐔, 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐀𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀!
09-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐑𝐀𝐒𝐌𝐈 𝐔𝐑𝐔𝐒𝐈, 𝐀𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐀 𝐍𝐀 𝐏𝐔𝐓𝐈𝐍
09-06-2026
𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎, 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐊𝐔𝐉𝐀
09-06-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐌𝐎𝐒𝐂𝐎𝐖, 𝐔𝐑𝐔𝐒𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀
09-06-2026
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐒𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐈𝐑𝐎 𝐊𝐖𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐊𝐀𝐙𝐈
09-06-2026
𝐅𝐔𝐍𝐆𝐀 𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐍𝐘𝐀𝐑𝐀 𝐋𝐄𝐎!!!
09-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐓𝐄𝐌𝐁𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐀 𝐍𝐀. 𝟐 𝐊𝐀𝐓𝐀 𝐘𝐀 𝐁𝐎𝐍𝐆𝐀
09-06-2026
𝐁𝐀𝐁𝐀𝐓𝐈 𝐌𝐉𝐈𝐍𝐈 𝐋𝐄𝐎 𝐓𝐔𝐍𝐀𝐈𝐅𝐔𝐍𝐈𝐊𝐀!!!
09-06-2026
𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐀 𝐍𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐇𝐀𝐍𝐀𝐍𝐆, 𝐀𝐒𝐈𝐊𝐈𝐋𝐈𝐙𝐀 𝐍𝐀 𝐊𝐔𝐓𝐀𝐓𝐔𝐀 𝐊𝐄𝐑𝐎 𝐙𝐀𝐎
09-06-2026