CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar kimempongeza Mwenyekiti wa CCM Taifa ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kutunukiwa Shahada ya juu ya Udaktari wa heshima ya uchumi na Chuo Kikuu cha Ankara nchini Uturuki
Pongezi hizo zimetolewa na Katibu wa Kamati Maalum ya NEC,Idara ya Itikadi,Uenezi na Mafunzo CCM Zanzibar Khamis Mbeto Khamis, wakati akizungumza katika mahojiano maalum huko Afisi kwake Kisiwandui Zanzibar.
Amesema heshima hiyo ni kubwa na inadhihirisha uhodari,uchapakazi,ubunifu na ueledi wa Rais Dkt.Samia katika kupaisha uchumi wa Tanzania katika nchi za Afrika zinazopiga hatua kubwa za maendeleo kiuchumi.
Mbeto,alisema CCM Zanzibar imepokea kwa furaha kubwa taarifa za kupewa heshima hiyo kubwa ya shahada ya Juu na Chuo chenye hadhi kubwa ya kufundisha fani za masuala ya uchumi duniani kilichofanya utafti wa kina na kikajiridhisha na kutoa heshima hiyo kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
“Chama Cha Mapinduzi tunampongeza kwa dhati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kupewa heshima hii ya Shahada ya Juu ya Phd hakika utendaji wako uliotukuka umeonekana hata kwa mataifa ya mbali hivyo nasi wananchi wake tuendelee kumpa moyo na kumuunga mkono.”,alisema Mbeto.
Katika maelezo yake Mbeto,amefafanua kuwa mara nyingi heshima hiyo ya udaktari hutolewa kwa mtu au kiongozi aliyeonyesha juhudi na mchango mkubwa katika Taifa lake katika kuivusha nchi katika mambo magumu yanayobeba maslahi mapana ya taifa kwa ujumla.
Alisema maono,busara na falsafa za Rais Dkt.Samia za kufungua milango ya diplomasia ya kiuchumi kwa mataifa mbalimbali kuja nchini kutembea na kufanya uwekezaji huru na wenye tija vinaendelea kumg’arisha kiuchumi katika anga za kimataifa.
Katibu huyo wa NEC, Mbeto, alitoa wito kwa Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi na Wananchi kwa ujumla kuendelea kumuombea dua ili Mwenyezi Mungu ampe Rais Dkt.Samia nguvu,ujasiri na maamuzi sahihi ya kufanikisha mipango ya kuwaletea wananchi wote maendeleo endelevu ya kiuchumi na kijamii.
Sambamba na hayo Mbeto, alikumbusha kwamba Dkt.Samia tayari ametunukiwa shahada nne za heshima toka ameingia madarakani Machi 19,2021 ambazo ni Shahada ya kwanza ya heshima ya udaktari,aliyotunukiwa na Chuo Kikuu cha Dar es saalam(UDSM) mwaka Novemba 30,2022.
Nyingine ni Shahada ya heshima ya Udaktari wa Falsafa kutoka Chuo Kikuu cha Jawaharlal Nehru nchini India, Oktoba 10,2023, heshima ya Udaktari ya usimamizi wa Utalii na Masoko ya Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA) Disemba 28, 2023 pamoja na aliyoipata jana ya Chuo Kikuu cha Ankara nchini Uturuki.
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
25-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
25-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
25-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
25-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
25-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
25-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
25-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
25-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
25-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
25-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
25-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
25-05-2026
𝗞𝗜𝗦𝗛𝗜𝗡𝗗𝗢 𝗖𝗛𝗔 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗖𝗛𝗔𝗣𝗢𝗞𝗘𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗛𝗔𝗡𝗚𝗪𝗘 𝗗𝗔𝗥 𝗘𝗦 𝗦𝗔𝗟𝗔𝗔𝗠
25-05-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
25-05-2026
𝗩𝗜𝗝𝗔𝗡𝗔 𝗧𝗨𝗜𝗟𝗜𝗡𝗗𝗘 𝗔𝗠𝗔𝗡𝗜 𝗬𝗔 𝗡𝗖𝗛𝗜 𝗬𝗘𝗧𝗨 - 𝗠𝗪𝗘𝗡𝗘𝗭𝗜 𝗞𝗘𝗡𝗔𝗡𝗜
25-05-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
25-05-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
25-05-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
25-05-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
25-05-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
25-05-2026