CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar kimempongeza Mwenyekiti wa CCM Taifa ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kutunukiwa Shahada ya juu ya Udaktari wa heshima ya uchumi na Chuo Kikuu cha Ankara nchini Uturuki
Pongezi hizo zimetolewa na Katibu wa Kamati Maalum ya NEC,Idara ya Itikadi,Uenezi na Mafunzo CCM Zanzibar Khamis Mbeto Khamis, wakati akizungumza katika mahojiano maalum huko Afisi kwake Kisiwandui Zanzibar.
Amesema heshima hiyo ni kubwa na inadhihirisha uhodari,uchapakazi,ubunifu na ueledi wa Rais Dkt.Samia katika kupaisha uchumi wa Tanzania katika nchi za Afrika zinazopiga hatua kubwa za maendeleo kiuchumi.
Mbeto,alisema CCM Zanzibar imepokea kwa furaha kubwa taarifa za kupewa heshima hiyo kubwa ya shahada ya Juu na Chuo chenye hadhi kubwa ya kufundisha fani za masuala ya uchumi duniani kilichofanya utafti wa kina na kikajiridhisha na kutoa heshima hiyo kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
“Chama Cha Mapinduzi tunampongeza kwa dhati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kupewa heshima hii ya Shahada ya Juu ya Phd hakika utendaji wako uliotukuka umeonekana hata kwa mataifa ya mbali hivyo nasi wananchi wake tuendelee kumpa moyo na kumuunga mkono.”,alisema Mbeto.
Katika maelezo yake Mbeto,amefafanua kuwa mara nyingi heshima hiyo ya udaktari hutolewa kwa mtu au kiongozi aliyeonyesha juhudi na mchango mkubwa katika Taifa lake katika kuivusha nchi katika mambo magumu yanayobeba maslahi mapana ya taifa kwa ujumla.
Alisema maono,busara na falsafa za Rais Dkt.Samia za kufungua milango ya diplomasia ya kiuchumi kwa mataifa mbalimbali kuja nchini kutembea na kufanya uwekezaji huru na wenye tija vinaendelea kumg’arisha kiuchumi katika anga za kimataifa.
Katibu huyo wa NEC, Mbeto, alitoa wito kwa Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi na Wananchi kwa ujumla kuendelea kumuombea dua ili Mwenyezi Mungu ampe Rais Dkt.Samia nguvu,ujasiri na maamuzi sahihi ya kufanikisha mipango ya kuwaletea wananchi wote maendeleo endelevu ya kiuchumi na kijamii.
Sambamba na hayo Mbeto, alikumbusha kwamba Dkt.Samia tayari ametunukiwa shahada nne za heshima toka ameingia madarakani Machi 19,2021 ambazo ni Shahada ya kwanza ya heshima ya udaktari,aliyotunukiwa na Chuo Kikuu cha Dar es saalam(UDSM) mwaka Novemba 30,2022.
Nyingine ni Shahada ya heshima ya Udaktari wa Falsafa kutoka Chuo Kikuu cha Jawaharlal Nehru nchini India, Oktoba 10,2023, heshima ya Udaktari ya usimamizi wa Utalii na Masoko ya Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA) Disemba 28, 2023 pamoja na aliyoipata jana ya Chuo Kikuu cha Ankara nchini Uturuki.
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
18-11-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
18-11-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
18-11-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
18-11-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
18-11-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
18-11-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
18-11-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
18-11-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
18-11-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
18-11-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
18-11-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
18-11-2025
TAARIFA KWA UMMA
18-11-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
18-11-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
18-11-2025
MONGELLA AONGOZA MAZISHI YA KADA WA CCM JIJINI MWANZA
18-11-2025
ASIYETII SHERIA, KATIBA NA KUWA TAYARI KUUA KWA MASLAHI BINAFSI HUO NI UGAIDI’
18-11-2025
πππ π¬ππ¦ππ¦ππ§πππ πͺπππ’π πππ ππ¨πππππππͺπ ππͺπ ππ¨πππ‘πππ§ππ π¨πͺπππ’, π¨πππππ‘ππ’ π‘π π¨πππππππ¨, π¬ππππ ππ π πππ¨π‘ππ - πππ. πππ©π¨
18-11-2025
KAENI KIMYA KAMA HAMJUI NCHI ILIKOTOKA - WASIRA
18-11-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amefungua kiwanda cha kutengeneza mabomba ya maji na uchakataji pamba cha MOLI Oil Mills Co. Ltd kilichopo Bariadi Mkoani Simiyu tarehe 16 Juni, 2025.
18-11-2025