CCM - Chama Cha Mapinduzi
Muda Wa Kazi: 24/7

Habari na Matukio Mbalimbali


KINANA AWATAKA WAISLAM KUZINGATIA MAADILI MEMA.

alternative

Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Kanali Mstaafu Abdulrahman Kinana, amewataka Waislamu kuzingatia mafundisho ya Mtume Muhammad (SAW) hususan kuhusu uchamungu na tabia njema.

Kinana ameyasema hayo leo Machi 25, 2023 wakati wa hafla ya mashindano ya Kuraani tukufu yaliyoandaliwa na Taasisi ya Faraja Foundation ya jijini Dar es Salaam.

""Tunaagizwa na Kuraani, pia tunaagizwa na Mtume wetu (Muhammad - S A.W) kuwa kila Mwislamu anapaswa kuzingatia mambo mawili lakwanza 'takwa' (uchamungu) na lapili 'akhlaki' tabia njema).

"Kwahiyo ukizingatia 'takwa' ukazingatia na maadili mema hakuna namna utapotoka, itakuwa hakuna haja hata ya sisi kuwa na wasiwasi kwamba maadili mabaya yanaweza yakatupitia," amesema Kinana.

Aidha, aliwahamasisha Waislamu nchini kuwapeleka watoto wao madrasa wakajifunze imani na maadili ya dini yao na kumjua Mwenyezi Mungu.

alternative alternative alternative

Maoni & Mawasiliano

Unaweza kuwasiliana na CCM, kwa kutumia anuani hapo chini kwa Maswali yoyote na Maoni.
Chama Cha Mapinduzi, Kuu Street, P.O.Box 50, Dodoma-TZ.
Barua Pepe
Muda Wa Kazi
24/7
Anuani
P.O.Box 50