CCM - Chama Cha Mapinduzi
Muda Wa Kazi: 24/7

Habari na Matukio Mbalimbali


ZIARA YA CHONGOLO YAACHA NEEMA KILOSA.

alternative

ZIARA ya Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Daniel Chongolo mkoani Morogoro, imeachaneema kwa wakazi wa Wilaya Kilosa baada ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kutangaza gharama yauunganishaji umeme wilayani humo sasa ni sh. 27,000 tu.


Hatua hiyo imetangazwa leo Januari 30, 2023 baada yaKatibu Mkuu Chongolo Meneja wa TANESCO Mkoa waMorogoro Fadhili Chilombe kutoa ufafanuzi dhidi yamalalamiko ya wananchi waliolalamikia kuunganishiwaumeme kwa sh. 310,000.


Akijibu changamoto hiyo baada ya Katibu MkuuChongolo kumtaka afanye hivyo, Chilombealiwahakikishia wananchi kuwa kuanzia leo umemekatika vijiji vya Kilosa ikiwemo Kata ya Dumilautaunganishwa kwa gharama ya sh. 27,000 tu na sio sh. 310,000.


Pia, amemuhakikishia Katibu Mkuu Chongolo kuwa nawananchi kuwa, hadi Aprili mwaka huu, vijiji vyote vyaKilosa vitakuwa vimefikishiwa umeme. 


Ufafanuzi huo ulitokana na taarifa  ya Katibu wa ShinaNamba 10 Dumila, Zainabu Ajili Ally ambaye ameesemakata hiyo inakabiliwa na changamoto mbalimbali ambazozimekuwa adha kwa wananchi, ikiwamo gharama kubwaza uunganishaji wa umeme majumbani.

Chongolo yupo katika ziara ya kikazi mkoani Morogoroakiwa ameongozana na na Katibu wa Halmashauri Kuuya Taifa (NEC) ya CCM, Itikadi na Uenezi, Sophia Mjema na Katibu wa NEC Oganaizesheni, Issa Haji(Gavu).

alternative alternative alternative alternative

Maoni & Mawasiliano

Unaweza kuwasiliana na CCM, kwa kutumia anuani hapo chini kwa Maswali yoyote na Maoni.
Chama Cha Mapinduzi, Kuu Street, P.O.Box 50, Dodoma-TZ.
Barua Pepe
Muda Wa Kazi
24/7
Anuani
P.O.Box 50