CCM - Chama Cha Mapinduzi
Muda Wa Kazi: 24/7

Habari na Matukio Mbalimbali


Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Tanzania Bara Ndg.Christina Mndeme ameendelea na Ziara yake ya siku nne  Mkoani Kigoma

alternative

Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Tanzania Bara Ndg.Christina Mndeme ameendelea na Ziara yake ya siku nne  Mkoani Kigoma ambapo Leo ametembelea Wilaya ya Uvinza na kukagua ujenzi wa tenki la maji katika Kata ya Kandaga katika kijiji cha Mlela ambapo amewaagiza Shirika la Umeme Tanesco Mkoani Kigoma kufunga mara moja transfoma la Umeme ndani ya siku Tano ili kuwezesha mtambo WA maji kuanza kufanya kazi.


Sambamba na hilo amefanya Mkutano Wa hadhara na wananchi wa Kata ya Nguluka huku akiwataka wananchi hao kujitokeza Kwa wingi tarehe  28 Agosti,2022  kuhesabiwa katika zoezi la Sensa ya watu na makazi.

Ameyasema hayo Leo tarehe 06 Agosti,2022 Wilayani uvinza Mkoani Kigoma.

Maoni & Mawasiliano

Unaweza kuwasiliana na CCM, kwa kutumia anuani hapo chini kwa Maswali yoyote na Maoni.
Chama Cha Mapinduzi, Kuu Street, P.O.Box 50, Dodoma-TZ.
Barua Pepe
Muda Wa Kazi
24/7
Anuani
P.O.Box 50