CCM - Chama Cha Mapinduzi
Muda Wa Kazi: 24/7

Habari na Matukio Mbalimbali


MKUTANO MKUU MAALUM WA CCM JIMBO LA BUKOMBE MKOA WA GEITA

alternative

Katibu Mkuu wa CCM Ndg. Daniel Chongolo ambae pia ni  Mgeni Rasmi katika Mkutano Mkuu maalum wa CCM Jimbo la Bukombe Mkoa wa Geita amepokea taarifa ya Utekelezaji wa Ilani ya CCM 2020 -2025 Jimbo la Bukombe. 

Aidha Ndg. Chongolo ameweka jiwe la Msingi na Uzinduzi  wa Jengo la Ukumbi wa CCM wilaya pamoja na Nyumba ya kulala wageni katika eneo la CCM wilaya ya Bukombe Mkoa wa Geita.

Akiwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Ilani ya CCM Jimbo la Bukombe Ndg Dotto Mashaka Biteko Mbunge wa Jimbo la Bukombe na Waziri wa Madini amewaondoa mashaka wanachama wa CCM na kuwasihi waendelee kukiamini Chama Cha Mapinduzi, ambapo jimbo la Bukombe lipo salama na maendeleo yaliopo bukombe yanaletwa na wanabukombe wenyewe.

Katibu Mkuu wa CCM Ndg Daniel Chongolo ameambatana na katibu wa NEC Idara ya Organaizesheni na Mlezi wa Mkoa wa Geita Ndg. Issa Haji Ussi Gavu ambapo ametambulishwa Rasmi leo katika wilaya ya Bukombe Mkoa wa Geita na Mgeni Rasmi katika Mkutano Mkuu maalum wa CCM Jimbo la Bukombe.
 

alternative alternative alternative alternative

Maoni & Mawasiliano

Unaweza kuwasiliana na CCM, kwa kutumia anuani hapo chini kwa Maswali yoyote na Maoni.
Chama Cha Mapinduzi, Kuu Street, P.O.Box 50, Dodoma-TZ.
Barua Pepe
Muda Wa Kazi
24/7
Anuani
P.O.Box 50